Ng'ombe 20 wafa kwa kulishwa sumu na mwekezaji Monduli

Topi

Member
Feb 7, 2012
59
17
Ng'ombe 20 wamekufa baada ya kula majani iliyopigwa dawa na mwekezaji mmoja wilayani Monduli, pia watu zaidi ya 38 wamelazwa ktk hospital ya wilaya baada ya kula nyama ya ng'ombe hao, wanyamapori pia wameripotiwa kufa, pls wadau mtupe habari zaidi kwa mliopo maeneo hayo. Source ITV-taarifa ya habari
 
Ndio tatizo la watanzania ng'ombe amekufa hata hajui chanzo cha kifo chake mtu anakula nyama wengine wanapeleka hata buchani kuuzia watu wengine tuache tamaa ya hela matokeo yake ndio hayo.
 
Mungu awasaidie wagonjwa wapone haraka!!
Pia mwenye data zaidi akizileta itatupa mwanga wa kuchangia hoja!!
Maswali ya kujiuliza!
Je,Mwekezaji anamiliki hapo kihalali?
Je,aliweka dawa eneo lake,halafu wananchi wakavamia na mifugo kutafuta majani kutokana na ukame?
Au aliweka dawa makusudi kwenye eneo la wananchi?
 
Dawa ni jamii ya kimasai nao waungane wamvamie huyo mwekezaji. Tumeshachoka TV_24_20120423_220533.jpg TV_24_20120423_220624.jpg TV_24_20120423_220648.jpg TV_24_20120423_220803.jpg
 
Na alaaniwe huyu mwekezaji mpaka na kizazi chake!

Atawatowaje wanyama wasio na hatia uhai bure tu?

Hakika huyu ni muaji tena asiye na huruma hata chembe!
Halafu bado anaangaliwa kwa macho yote haya mawili kweli?

Huyu mwekezaji ningependa sana nimsikie kafikishana wapi na raia walengwa wa tukio!
Ila nina hofu ya kwmb EL atakuwa anamjua kwa namna moja ama nyingine!

Haya matatizo yote sisiem ndio chanzo!
 
Hapo NDUGU ZETU WA KABILA LA WAMASAI WALIOAPATWA NA JANGA HILI inawabibidi kufuata sheria ya JINO kwa JINO.

KULIPA KISASI ni MUHIMU KATKA TUKIO KAMA HILI.

UNYAMAA KABISA Huu!!!



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Hata kama ni eneo lake sheria haimuachi, maana alilenga kuweka sumu akijua wananchi watapitisha ng'ombe pale wale halafu wafe. Anatakiwa kufikishwa mahakamani huyu
 
serikali inafanya makosa sana kuwapa makaburu ardhi ili kuwekeza. na hapo utakuta kaburu anapewa hata miaka 50 hata 100 ili awekeze. ina maana viongozi wa CCm wamesahau ama hawaoni yanayotokea Afrika kusini na Zimbabwe? huko A. kusini tunaambiwa kaburu alikuja kama setla. sasa kang'ang'ania akidai '' South Africa is my motherland !'' tofauti ya kipato ni kubwa sana A kusini. mwenye mali haswa ni kaburu. Wengi walimwona Mugabe kama mtu mjinga sana alipowatimua makaburu nchini kwake, wanamcheka lakini matunda yake yatakuja kuonekana huko mbeleni. sasa sisi tunajifanya hatuoni, tunawapa migodi , ardhi mpaka wanyama, tena hakuna kitu kinaniuma kama kuwarusu hawa Makaburu kuuwa twiga zetu. hii ni nembo ya taifa ndio maana mpaka ikawekwa kwenye noti, Lazima Ilindwe!
sasa haya majitu yakishaua hawa wanyama yanapiga picha na kupost facebook, tunabaki kuchekwa tu kila uchao kwa sababu ya watu wachache tu wasio na uzalendo bali wapo kwa ajili ya matumbo yao. Jamani naombeni tubadilike
 
Mwekezaji ni kaka yake yule mama aliyempiga ngumi mwalimu mkuu wa shule fulani kule Arusha wilaya yaManyara (Mholansi au mdachi) hawa ndiyo babu zao makaburu wa afrika ya kusini kwani makaburu walitokea uholansi na lugha yao ya afrikaner ni kama lugha ya kidachi.
 
Mwekezaji ni kaka yake yule mama aliyempiga ngumi mwalimu mkuu wa shule fulani kule Arusha wilaya yaManyara (Mholansi au mdachi) hawa ndiyo babu zao makaburu wa afrika ya kusini kwani makaburu walitokea uholansi na lugha yao ya afrikaner ni kama lugha ya kidachi.

Mholanzi , mdachi , kaburu. wote hawa ni kitu kimoja na wanaongea lugha moja. wanasifika sana kwa ideology yao ya Unazi ( NAZISM), kwao ni kitu cha kawaida kabisa kumpiga risasi mtu mweusi. hivyo msishangae vitu kama hivi kutokea. hawa jamaa hawafai.
 
amerudi kama mpangaji aliyekuwa m'miliki kabla ya uhuru nchi imeuzwa jamani msishangae
 
Ng'ombe 20 wamekufa baada ya kula majani iliyopigwa dawa na mwekezaji mmoja wilayani Monduli, pia watu zaidi ya 38 wamelazwa ktk hospital ya wilaya baada ya kula nyama ya ng'ombe hao, wanyamapori pia wameripotiwa kufa, pls wadau mtupe habari zaidi kwa mliopo maeneo hayo. Source ITV-taarifa ya habari

Hivi nikweli?na bado huyo mwekezaji hajakamatwa?au ndio tumewekwa mfukoni?
 
kiyeuyeu>Tena mfuko wa nyuma, kwa taarifa ni kwamba mkaburu anaendelea na shughuli zake kama kawaida, hii inanitia hasira mno, jamani hakuna mu-al shabab humu mwenye knowledge ya mabomu ya kujilipua mimi nizame huko fasta.
 
Last edited by a moderator:
Aliweka dawa za halali kabisa za kuua manyasi na magugu zinazouzwa madukani.

Alishawaambia wanakijiji kabla na alisha ripoti polisi. Anaishi hapo zaidi ya miaka 20.

Hao wamasai walitumwa na nani?

Kuna Watanzania wanaipeleka pabaya hii nchi. Mnawatafuta wawekezaji kwa udi na uvumba na wanapofika kuna wachache wasiopenda maendeleo wanafanya njama za kuwahujumu. Huyo ana hati miliki ya hiyo ardhi ki halali kabisa na yeyote anae tresspass katika eneo lake anaweza hata kuuwawa.

Huyo Mzungu hana kosa, asionewe bure. Wenye kosa ni hao wamasai wanaorubuniwa na kuvamia sehemu za watu, tumeshasikia wamasai wakivamia Bagamoyo na Morogoro na kufanya uharibufu na ukaidi hata kwa Watanzania wenzao, Hii si mara ya kwanza kwa Wamasai kuwa wakaidi na wabishi. Lakini wameuvaa mkenge, wanawaonea wakwere na waluguru tu.
 
kule meru wananchi wamegawana kiwanja cha muwekezaji na kutenga maeneo ya shule,hospitali na kituo cha polisi
 
Back
Top Bottom