nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]
[/FONT]
Saturday, 26 November 2011 08:50 |
Hussein Issa SIKU moja baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kumvua madaraka aliyekuwa katibu wa chama hicho mkoani Dar es Salaam, Kilumbe Ng'enda,mtendaji huyo ameibuka na kusema "sikuzaliwa ili kuwa Katibu wa CCM" .Ng'enda alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili kuhusu uamuzi wa kumwondoa kwenye nafasi hiyo ya utendaji ndani ya chama. Ngenda alisema kuvuliwa kwake madaraka si kosa wala balaa na kwamba ni utaratibu wa kawaida katika shughuli za utendaji. Hiyo ndio tabia ya vyeo, si kosa mimi kuondolewa lakini najipanga kupokea cheo kingine ndani ya chama changu, alisema Ngenda. Juzi Halmashauri Kuu ya CCM iliyokutana mjini Dodoma,ilitangaza kumvua madaraka Ng'enda kwa kile kilichoelezwa kuwa hakufuata maamuzi ya vikao halali vya chama kwenye masuala ya uchaguzi wa viti maalumu. Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma baada ya vikao kuwa hatua hiyo inatokana na mtendaji huyo kwenda kinyume cha maamuzi ya vikao halali vya chama hicho. Alisema hata hivyo Ngenda atapangiwa kazi nyingine ndani ya chama hichoHabari zaidi zilisema mkakati wa kujivua gamba ulioasisiwa na chama hicho Aprili mwaka huu, sasa unarejeshwa katika Kamati ya Maadili ambako watuhumiwa wa makosa mbalimbali watafikishwa na kuelezwa tuhuma zinazowakabili. Mpango wa kujivua gamba ulilenga kuwashinikiza watuhumiwa wa ufisadi kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama hicho kinachotawala. |