Ngeleja: Msafara wangu haujazuiwa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,041
Ngeleja(55).jpg

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja


Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amesema msafara wake alipokuwa ziarani Geita kupita kwenye mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) Ijumaa, haukuzuiwa na walinzi wa mgodi huo kwa nia ya kupekuliwa.

Akizungumza na NIPASHE jana kutokana na kuchapisha habari kuhusu kuzuiwa kwa muda kwa msafara wake kwenye lango la GGM, Ngeleja alisema habari hizo zimemshitua sana kwani hakukuwa na kitu kama hicho.

Jana gazeti hili lilichapisha habari katika ukurasa wake wa kwanza ikisema kuwa Waziri Ngeleja alionja machungu baada ya msafara wake kuzuiwa kwa muda na walinzi wa GGM ili kupekuliwa.

Katika habari hizo ambazo ziliandikwa na mwandishi aliyekuwa kwenye msafara wa Ngeleja, zilisema kuwa msafara huo ulikaa langoni hapo kwa takribani dakika 10 hadi uongozi wa juu wa mgodi ulipoingilia kati na kuokoa jahazi.

Naye Ofisa Uhusiano wa GGM, Joseph Mangilima, ambaye habari ya jana ilisema alipoulizwa juu ya kadhia hiyo alikataa kuzungumzia kwa maelezo kuwa kampuni inayolinda mgodi huo ya G4S inajitegemea na
hawezi kuzungumza kwa niaba yao, alitoa ufafanuzi zaidi wa kadhia hiyo.

Akizungumza jana kwa njia ya simu na NIPASHE iliyotaka kujua kwa kina chanzo cha kadhia hiyo, Mangilima alisema kimsingi msafara haukuzuiwa ili upekuliwe.

“Walinzi walikuwa wanabadilishana zamu ndani ya kontena ndiyo maana wakachelewa kufungua geti mara moja. Hata dakika moja haikumalizika,” alisema Mangilima.

Alifafanua kuwa msafara wa Waziri Ngeleja ulikuwa umetokea ziwani lakini mgodini kulikuwa hakuna taarifa kwamba ulikuwa unaelekea huko (mgodini), ndiyo maana walinzi hawakuwa tayari kufungua geti mara moja.
Mangilima alisema wamesikitishwa na habari hiyo kwa kuwa haikueleza ukweli wa suala lenyewe.




CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Ngeleja(54).jpg

William Ngeleja.


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Mwanza, kimewaomba wakazi wa Jimbo la Sengerema kukisaidia kumng'oa Mbunge wa jimbo hilo, William Ngeleja.

Chadema imesema ingawa kinafahamu kuwa kazi ya kumng'oa Ngeleja jimboni humo ni ngumu, lakini kwa kuwa amekichokoza kwa kuwahujumu viongozi na wanachama wake, watalazimika kujibu mapigo.

Aidha, kimesema tayari kimeshajipanga na kitawashirikisha baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete, amteme katika nafasi yake ya uwaziri.

Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (Chadema), Ezekiel Wenje, aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika uwanja wa Mnadani.

Mkutano huo ulilenga kujijenga upya kwa chama hicho baada ya ofisi yake kufungwa kufuatia viongozi wake kukimbilia CCM na kupokewa na Ngeleja.

Katika mkutano huo, Wenje alisema awali alikuwa akimpenda Ngeleja, lakini baada ya kutishia chama chake kwa kuiba wanachama wake, basi sasa ametangaza vita na Chadema kitahakikisha kuwa anang'olewa kwenye nafasi ya uwaziri na hata ubunge mwaka 2015.

''Hakuna jinsi, nimeamua kuja kufanya mkutano hapa japokuwa najua Ngeleja anakubalika..nilipokuja katika uwanja huu mwaka jana, mliniambia huu ni uwanja wa Ngeleja, lakini bado kwa usajiri nimerudi kwa staili hii ya kuwaomba mtusaidie kumng'oa...hata sasa ninapohutubia hapa, Ngeleja yuko wilayani Magu kuendelea kuibomoa Chadema," alisema Wenje.

Pia Wenje alisema amekasirishwa sana na hatua ya Ngeleja kuendesha kikao cha ndani katika ukumbi wa jengo Chama Kikuu cha Ushrika cha Mkoa wa Mwanza jimboni kwake Nyamagana Januari 7, mwaka huu na kupokea wanachama 30 kutoka Chadema kutoka Wilaya za Magu na Kwimba na hivyo kutishia maslahi ya Chadema.

"Siko kwa ajili ya kusema mazuri wala kuipa ujiko serikali ya CCM au wabunge wake akiwemo Ngeleja, bali nipo kwa ajili ya kutetea na kulinda maslahi ya Chadema ili kuibomoa CCM," alisema.




CHANZO: NIPASHE
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom