BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Date::9/28/2008
Kampeni Tarime: Vyama vya Chadema, CCM vyazidi kujimarisha
*Zitto, Lissu, Ngeleja, Mashishanga wawasili
Frederick Katulanda, Tarime
Mwananchi
WAKATI zikiwa zimesalia siku 13 za kupiga kampeni kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, vyama vya upinzani vimeita viongozi wake wa juu ili kuongeza nguvu katika kampeni zake.
Uchaguzi huo unafanyika Oktoba 12 kuhitimisha kampeni zilizojaa matukio tofauti tangu zilipoanza Septemba 14. Kampeni hizo zitaisha Oktoba 11.
Uchaguzi huo mdogo unafanywa ili kuziba kiti kilichoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Chacha Zakayo Wangwe, ambaye alifariki kwa ajali ya gari mkoani Dodoma.
Katika kuhakikisha vinaongeza nguvu katika siku zilizosalia, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetuma jopo la viongozi wake wa juu, akiwemo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Mwanasheria wake Tindu Lissu pamoja na wabunge wake wote 10 ambao watakuwa mjini Tarime kusaidia kampeni.
Kwa upande wa CCM, licha ya kuwa na Katibu wake Mkuu, Yusuf Makamba na Makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, pia wamemwita mkuu wa zamani wa mkoa wa Mwanza na baadaye Morogoro, Stephen Mashishanga pamoja na mwanasiasa maarufu aliyepata kupitia chama cha upinzani cha CUF, Salum Msabaha na Waziri wa Nishati na Madini,William Ngereja kuongeza nguvu, wakijumuika na Stephen Wassira pamoja na Philimon Sarungi.
Wagombea wa vyama hivyo katika uchaguzi huo ni Charles Mwera Nyanguru wa Chadema na Christopher Ryoba Kangoye (CCM).
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Kampeni na Uchaguzi wa Chadema, Msafiri Mtemelwa alisema tayari Zitto Kabwe ameshawasili na kwamba wabunge wengine wa chama chao watawasili leo (Jumatatu) wakati Mwenyekiti wake Freeman Mbowe atawasili kesho kutwa.
Alisema kuja kwa viongozi hao ni sehemu na wajibu wao katika kuhakikisha wanasaidia chama na kwamba, wakiwa mjini Tarime watafanya mikutano yao katika kata za Nyamongo, Sirari, Tarime mjini pamoja na kata nyinginezo kadri chama hicho kitakavyoona inafaa.
Wanakuja katika kampeni, hili ni jambo la kawaida, wanakuja kwa ajili ya kurahisisha kampeni zetu, ndiyo maana wakiwa hapa tutawagawanya katika maeneo mbalimbali kusaidia kumnadi mgombea wetu, watafanya mikutano katika kata zile ambazo tunahitaji kufanya vizuri zaidi, lakini kwa upande wa Lissu yeye anakuja kuhakikisha haki na usawa kama mwanasheria inatumika, alieleza Mtemelwa.
Aliongeza kuwa pamoja na kushiriki katika mikutano ya kampeni hiyo pia Lissu atapambana na polisi ambao wameanza zoezi la kamatakamata vijana kwa kisingizio cha vurugu, ikiwa ni pamoja na kupiga kambi katika eneo la Mgodi wa Nyamongo ambako atapambana na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngereja.
Kwa upande wa CCM akizungumza na Mwananchi Katibu wa CCM wilayani Tarime, Luteni Iddi Stambuli, alipoulizwa kuhusiana na ujio wa viongozi wengine alisema hawezi kueleza kwa vile hilo ni suala la mikakati yao ambayo hawawezi kuitangaza magazetini.
Hayo ni masuala yetu ya ndani, kama tunaongeza au hatuongezi hayo sio ya magazeti, kama ni huyo Mashishanga yeye yupo hapa kama wanachama wengine, haya si masuala ya kuzungumzia katika magazeti, alieleza alipoulizwa kwa njia ya simu.
Hata hivyo, habari kutoka ndani ya CCM wilayani hapa zimeeleza kuwa, viongozi hao wamegawanywa katika kata ambapo Sarungi na Wassira wamegawanya katika maeneo yenye migogoro ya koo za wenyewe kwa wenyewe kutokana na kuaminika kuwa wanakubalika na wana ushawishi mkubwa, wengine wameachwa Tarime mjini huku Ngeleja akitarajiwa kupelekwa eneo la Mgodi wa Nyamongo.
Sisi viongozi wamegawanywa katika kata kulingana na umuhimu wa mtu na kata zenyewe na ugumu wake, lakini Makamba na Msekwa wao wamebaki kama viongozi na waratibu wa kampeni kila panapohitajika nguvu ya ziada wamekuwa wakienda kujazia,kilieleza chanzo chetu kimoja.
Tayari Zitto Kabwe ameshaingia mjini hapa wakati Lissu naye amethibitisha kufika kesho sambamba na wabunge wengine, lakini kwa upande wa CCM Ngeleja alipopigiwa simu kuthibitisha hilo aliomba kupigiwa baadaye kutokana na kuwa katika kikao.
Kampeni Tarime: Vyama vya Chadema, CCM vyazidi kujimarisha
*Zitto, Lissu, Ngeleja, Mashishanga wawasili
Frederick Katulanda, Tarime
Mwananchi
WAKATI zikiwa zimesalia siku 13 za kupiga kampeni kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, vyama vya upinzani vimeita viongozi wake wa juu ili kuongeza nguvu katika kampeni zake.
Uchaguzi huo unafanyika Oktoba 12 kuhitimisha kampeni zilizojaa matukio tofauti tangu zilipoanza Septemba 14. Kampeni hizo zitaisha Oktoba 11.
Uchaguzi huo mdogo unafanywa ili kuziba kiti kilichoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Chacha Zakayo Wangwe, ambaye alifariki kwa ajali ya gari mkoani Dodoma.
Katika kuhakikisha vinaongeza nguvu katika siku zilizosalia, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetuma jopo la viongozi wake wa juu, akiwemo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Mwanasheria wake Tindu Lissu pamoja na wabunge wake wote 10 ambao watakuwa mjini Tarime kusaidia kampeni.
Kwa upande wa CCM, licha ya kuwa na Katibu wake Mkuu, Yusuf Makamba na Makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, pia wamemwita mkuu wa zamani wa mkoa wa Mwanza na baadaye Morogoro, Stephen Mashishanga pamoja na mwanasiasa maarufu aliyepata kupitia chama cha upinzani cha CUF, Salum Msabaha na Waziri wa Nishati na Madini,William Ngereja kuongeza nguvu, wakijumuika na Stephen Wassira pamoja na Philimon Sarungi.
Wagombea wa vyama hivyo katika uchaguzi huo ni Charles Mwera Nyanguru wa Chadema na Christopher Ryoba Kangoye (CCM).
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Kampeni na Uchaguzi wa Chadema, Msafiri Mtemelwa alisema tayari Zitto Kabwe ameshawasili na kwamba wabunge wengine wa chama chao watawasili leo (Jumatatu) wakati Mwenyekiti wake Freeman Mbowe atawasili kesho kutwa.
Alisema kuja kwa viongozi hao ni sehemu na wajibu wao katika kuhakikisha wanasaidia chama na kwamba, wakiwa mjini Tarime watafanya mikutano yao katika kata za Nyamongo, Sirari, Tarime mjini pamoja na kata nyinginezo kadri chama hicho kitakavyoona inafaa.
Wanakuja katika kampeni, hili ni jambo la kawaida, wanakuja kwa ajili ya kurahisisha kampeni zetu, ndiyo maana wakiwa hapa tutawagawanya katika maeneo mbalimbali kusaidia kumnadi mgombea wetu, watafanya mikutano katika kata zile ambazo tunahitaji kufanya vizuri zaidi, lakini kwa upande wa Lissu yeye anakuja kuhakikisha haki na usawa kama mwanasheria inatumika, alieleza Mtemelwa.
Aliongeza kuwa pamoja na kushiriki katika mikutano ya kampeni hiyo pia Lissu atapambana na polisi ambao wameanza zoezi la kamatakamata vijana kwa kisingizio cha vurugu, ikiwa ni pamoja na kupiga kambi katika eneo la Mgodi wa Nyamongo ambako atapambana na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngereja.
Kwa upande wa CCM akizungumza na Mwananchi Katibu wa CCM wilayani Tarime, Luteni Iddi Stambuli, alipoulizwa kuhusiana na ujio wa viongozi wengine alisema hawezi kueleza kwa vile hilo ni suala la mikakati yao ambayo hawawezi kuitangaza magazetini.
Hayo ni masuala yetu ya ndani, kama tunaongeza au hatuongezi hayo sio ya magazeti, kama ni huyo Mashishanga yeye yupo hapa kama wanachama wengine, haya si masuala ya kuzungumzia katika magazeti, alieleza alipoulizwa kwa njia ya simu.
Hata hivyo, habari kutoka ndani ya CCM wilayani hapa zimeeleza kuwa, viongozi hao wamegawanywa katika kata ambapo Sarungi na Wassira wamegawanya katika maeneo yenye migogoro ya koo za wenyewe kwa wenyewe kutokana na kuaminika kuwa wanakubalika na wana ushawishi mkubwa, wengine wameachwa Tarime mjini huku Ngeleja akitarajiwa kupelekwa eneo la Mgodi wa Nyamongo.
Sisi viongozi wamegawanywa katika kata kulingana na umuhimu wa mtu na kata zenyewe na ugumu wake, lakini Makamba na Msekwa wao wamebaki kama viongozi na waratibu wa kampeni kila panapohitajika nguvu ya ziada wamekuwa wakienda kujazia,kilieleza chanzo chetu kimoja.
Tayari Zitto Kabwe ameshaingia mjini hapa wakati Lissu naye amethibitisha kufika kesho sambamba na wabunge wengine, lakini kwa upande wa CCM Ngeleja alipopigiwa simu kuthibitisha hilo aliomba kupigiwa baadaye kutokana na kuwa katika kikao.