mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,966
Taarifa nilizozipata kutoka Bukoba ni kwamba,watu wanane wamekamatwa wakiwa nje ya kanisa katoliki mjini Bukoba wakiwa na vifaa ambavyo uchunguzi wa awali ulionesha kuwa ni vya mlipuko.Katika kanisa hilo ndipo misa ya shukrani iliyohudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda,ilifanyika katika kanisa la Cathedral ambapo ndipo mwili wa Cardinal Rugambwa ulizikwa rasmi jumamosi.Watu hao wameshikiliwa kituo cha polisi kwa uchunguzi na mahojiano zaidi.