News Alert: Wananchi wachomewa nyumba na serikali

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Habari ambazo zimeingia sasa hivi ni kuwa wananchi wa jamii ya Kimasai huko Kilosa wamejikuta wakichomewa nyumba zao kwa amri ya Mkuu wa Gereza la Mbigiri. Amri hiyo imetekelezwa bila kufuata sheria baada ya wananchi hao kudaiwa kuwa wamevamia eneo la gereza hilo. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Said Kalembo amemtaka Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro kumwajibisha Mkuu wa Gereza hilo kwa kuchukua sheria mikononi. Bw. Kalembo amesema kuwa "wananchi hao ni wananchi wenzetu na nchi hii ni yetu sote, na tusiwafanye wajihisi wako nchi nyingine". Mkuu wa Mkoa alidai sheria ni lazima zifuatwe na viongozi wa gereza hilo wangetumia muda kuwaelewesha wananchi juu ya eneo hilo badala ya kwenda na kuwachomea nyumba zao.

Hili ni suala jingine ambapo serikali inatumia nguvu zaidi katika masuala yanayohusu ardhi. Huko nyuma serikali kule Mkoani Mara iliwahi kuwachomea wananchi nyumba zao kiasi cha Tume ya Haki za Binadamu kuamua kufanya uchunguzi. Sakata la Buzwagi na lile la Bulyankulu bado yamo mawazoni mwa watu. Ni hatua gani zichukuliwe kwa wahusika hasa ukizingatia kuwa mapema mwaka jana viongozi wa magereza kule Ukonga waliamua kwenda kuwahamisha watu toka kwenye nyumba zao licha ya kesi kuwepo Mahakamani ambapo waandishi kadhaa walijikuta wanajeruhiwa..
 
Hawa wanafikiri nchi niya kwao ndio maana kila mtu ni bwana mkubwa.

Mungu awasadie watu hao ili waweze kukaa bila mvua kunyesha siku nne ili walau wajenge nyumba za maboksi ,serikali inaanza kuandaa wakimbizi wa ndani ni hatari sana .
 
Kama hilo eneo lilikua na Magereza walikua wapi hadi wamasai wajenga Huko?

Hamjui serikali ya Tz kupiti viongozi wake hujui ni Mungu watu?

Kama Vyeo kwa kujuana na kulindana, unafikiri huyo bwana atawajibishwa kwa mujibu wa sheria au atahamishwa kituo then imetoka? Nani anajua kuhusu aliykuwa Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai (Zombe)
 
Yaani kuna hii tabia ambayo inatokea mara kwa mara kuwa baadhi ya watu wanatendewa kana kwamba wao ni raia nusu. Wahadzabe wanakaribia kufa kwa njaa, na leo jamii ya wamasai ambao wameamua kuingia katika mambo ya kilimo na wako kwenye kijiji kilichopimwa rasmi lakini wachache wanaamua kuwachomea hizo nyumba na kila kitu.. hivi kwani hii ni Zimbabwe jamani?
 
chaguzi zilikwisha kitambo,sasa hawaangalii makunyanzi,unapokaribia uchaguzi kila kitu huwa swari ila wakishapata kula yao basi wakala na kuvimbiwa haya ndio matatizo yao.
 
ohhhhhhhhh
Poleni sana wamasai wa mbigiri huu ni unyama na unafaa ukomeshwa umeasahua kuwa cheo ni dhamana leo hii kuna waliokuwa wa kuu wa Gerezani tunagomabania nao daladala mjini na amesahau kuwa malipo ni hapa hapa duniani kwa unyama ameowafanyia wamasai.
 
duh,kumbe hata mkuu wa gereza ana amri kubwa kiasi hicho?kweli hii ni bongo,hao wamaasai kuwa huko wanakoishi hamna winter kama la wenzetu huku,mbona wangekufa kwa baridi,sijui kuhusu mvua,ila Mungu atawalinda,ccm tunaichagua wenyewe sasa tufanyeje.
 
Hata aliyeua akageuka entrepreneur bado liko mawazoni mwetu.
Huyo mkuu wa gereza kwa kuanzia ajiuzulu kwanza ili kupisha uchunguzi na taratibu za kumchukulia hatua kali za kisheria zifuatwe.

Lakini kwa taifa hili lenye kugeuza wauwaji kuwa wajasiriamali sijui kama litakua na dhamira ya dhati kumchukulia hatua kali

Kinachotakiwa ni sisi wananchi tuchukue hatua kali kama huyu mtu hatajiuzulu maanake hii ni fedheha
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom