Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kutoka mwanakijiji.com
Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Lawrence Masha leo ametembelea gereza la Keko ambapo mawaziri wawili wa zamani wanashikiliwa rumande wakikabiliwa na jumla ya mashtaka 13 dhidi yao kutokana na matumizi mabaya ya madaraka yaliyoisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi. Mawaziri hao wa zamani Bw. Basil Mramba (Rombo - CCM) na Daniel Yona walishindwa kupata dhamana jana baada ya kila mmoja wao kutakiwa kuweka dhamani ya karibu shilingi bilioni 3.
Bw. Masha aliyeenda gereza hilo kwa gari lake la binafsi na ambaye hakuwa ameonekana kuvaa "kiofisi" alishindwa kueleza ni kwanini kama amekwenda kule kikazi aende kwa kutumia gari la binafsi na bila ya kutoa taarifa ya awali kwa umma. Bw. Masha alishindwa kuelezea hilo hasa ikizingatiwa kuwa katika eneo la Dar kuna magereza mengine makubwa mawili ya Ukonga na Segerea ambayo angeweza kuyatembelea lakini aliamua kwenda kwenye gereza la Keko ambapo "jamaa" zake wanashikiliwa.
"Sisi hatujui alizungumza nao nini, kwani alipata nafasi ya kuzungumza nao" kimeelezea chanzo chetu si mbali sana na kuta za gereza hilo maarufu ambalo pia siku ya jana lilipata ugeni wa Dr. Ferdinand Masau ambaye alishindwa dhamana katika kesi iliyofunguliwa dhidi yake na NSSF. Dr. Masau ametimiza masharti leo na sasa yuko nje kwa dhamana.
"Jinsi alivyokuja kwa kweli aidha alikuwa na ujumbe fulani ambao ni yeye tu angeweza kuutoa au alikuja kuchukua ujumbe kutoka kwa washtakiwa" amesema afisa mmoja ambaye ana uhakika wa anachosema.
Wakati huo huo Mawakili wa kina Mramba na Yona wamefika tena kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi ambapo wameomba kupata mwenendo wa kesi hiyo ili waweze kupitia misingi ya dhamana iliyodaiwa na mahakama hiyo dhidi ya wateja wao. Haki anayesikiliza kesi hiyo Bw. Hezron Mwankenja amewaagiza makarani wa mahakama hiyo kuwapatia mara moja mawikili hao nakala hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya mahakamana Mawakili wa kina Mramba wanataka kukata rufaa kupinga kiasi kikubwa cha dhamana hiyo ili hatimaye wateja wao waweze kuachiliwa wakingojea kesi yao kutajwa tena Disemba 2. Vyanzo vyetu vimesema kuwa Mramba ni lazima awe nje kabla ya Ijumaa hii ili aweze kuhudhuria harusi ya binti yake anayeolewa na kijana wa Elvis Musiba siku chache zijazo.
Kama KLHN ilivyoripoti wiki iliyopita, kufikishwa mahakamani kwa mawaziri hao kulicheleweshwa wiki iliyopita kutokana na "send off" ya binti huyo wa Mramba ambayo ilifanyika katika hoteli ya Movenpick na kuhudhuriwa na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo Rais mstaafu Benjamin Mkapa.
Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Lawrence Masha leo ametembelea gereza la Keko ambapo mawaziri wawili wa zamani wanashikiliwa rumande wakikabiliwa na jumla ya mashtaka 13 dhidi yao kutokana na matumizi mabaya ya madaraka yaliyoisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi. Mawaziri hao wa zamani Bw. Basil Mramba (Rombo - CCM) na Daniel Yona walishindwa kupata dhamana jana baada ya kila mmoja wao kutakiwa kuweka dhamani ya karibu shilingi bilioni 3.
Bw. Masha aliyeenda gereza hilo kwa gari lake la binafsi na ambaye hakuwa ameonekana kuvaa "kiofisi" alishindwa kueleza ni kwanini kama amekwenda kule kikazi aende kwa kutumia gari la binafsi na bila ya kutoa taarifa ya awali kwa umma. Bw. Masha alishindwa kuelezea hilo hasa ikizingatiwa kuwa katika eneo la Dar kuna magereza mengine makubwa mawili ya Ukonga na Segerea ambayo angeweza kuyatembelea lakini aliamua kwenda kwenye gereza la Keko ambapo "jamaa" zake wanashikiliwa.
"Sisi hatujui alizungumza nao nini, kwani alipata nafasi ya kuzungumza nao" kimeelezea chanzo chetu si mbali sana na kuta za gereza hilo maarufu ambalo pia siku ya jana lilipata ugeni wa Dr. Ferdinand Masau ambaye alishindwa dhamana katika kesi iliyofunguliwa dhidi yake na NSSF. Dr. Masau ametimiza masharti leo na sasa yuko nje kwa dhamana.
"Jinsi alivyokuja kwa kweli aidha alikuwa na ujumbe fulani ambao ni yeye tu angeweza kuutoa au alikuja kuchukua ujumbe kutoka kwa washtakiwa" amesema afisa mmoja ambaye ana uhakika wa anachosema.
Wakati huo huo Mawakili wa kina Mramba na Yona wamefika tena kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi ambapo wameomba kupata mwenendo wa kesi hiyo ili waweze kupitia misingi ya dhamana iliyodaiwa na mahakama hiyo dhidi ya wateja wao. Haki anayesikiliza kesi hiyo Bw. Hezron Mwankenja amewaagiza makarani wa mahakama hiyo kuwapatia mara moja mawikili hao nakala hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya mahakamana Mawakili wa kina Mramba wanataka kukata rufaa kupinga kiasi kikubwa cha dhamana hiyo ili hatimaye wateja wao waweze kuachiliwa wakingojea kesi yao kutajwa tena Disemba 2. Vyanzo vyetu vimesema kuwa Mramba ni lazima awe nje kabla ya Ijumaa hii ili aweze kuhudhuria harusi ya binti yake anayeolewa na kijana wa Elvis Musiba siku chache zijazo.
Kama KLHN ilivyoripoti wiki iliyopita, kufikishwa mahakamani kwa mawaziri hao kulicheleweshwa wiki iliyopita kutokana na "send off" ya binti huyo wa Mramba ambayo ilifanyika katika hoteli ya Movenpick na kuhudhuriwa na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo Rais mstaafu Benjamin Mkapa.