Consigliere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 12,037
- 24,595
Majambazi watatu wamefanikiwa kutoroka mahakamani leo asubuhi mjini Tabora.
Majambazi hao watatu waliopelekwa mahakamani wakiwa vifua wazi, walitoroka baada ya askari waliokuwa wakiwalinda kuzembea a hivyo kuacha upenyo. Baada ya kutoroka askari walianza kuwafukuza majambazi hao huku wakirusha risasi hovyo na kuzua taharuki kubwa kwa watu waliokuwa wakiendelea shughuli zao, lakini kwa msaada wa raia polisi walifanikiwa kuwakamata majambazi wawili na mmoja kufanikiwa kutoroka kabisa na juhudi za kumsaka zinaendelea.
MTU MMOJA AJERUHIWA MDOMONI.
Katika sakata hilo lilopelekea askari kurusha risasi, kijana mmoja aliekuwa kwenye kibanda chake cha Mpesa, amejeruhiwa vibaya na risasi ya askari hao iliyompiga mdomoni
Majambazi hao watatu waliopelekwa mahakamani wakiwa vifua wazi, walitoroka baada ya askari waliokuwa wakiwalinda kuzembea a hivyo kuacha upenyo. Baada ya kutoroka askari walianza kuwafukuza majambazi hao huku wakirusha risasi hovyo na kuzua taharuki kubwa kwa watu waliokuwa wakiendelea shughuli zao, lakini kwa msaada wa raia polisi walifanikiwa kuwakamata majambazi wawili na mmoja kufanikiwa kutoroka kabisa na juhudi za kumsaka zinaendelea.
MTU MMOJA AJERUHIWA MDOMONI.
Katika sakata hilo lilopelekea askari kurusha risasi, kijana mmoja aliekuwa kwenye kibanda chake cha Mpesa, amejeruhiwa vibaya na risasi ya askari hao iliyompiga mdomoni