Maendeleo mapya: Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Uzalendo

Hivi kwanini tusi washawishi Watanzania tuungane Tanzania Nzima Kudai Katiba mpya?
Tuungane kuidai Katiba mpya

Silver25;

Hiyo kazi ya kushawishi Watanzania kuungana Tanzania nzima kwa sasa inafanywa na UKAWA(Umoja wa Katiba ya Wananchi). Kinachotakiwa kwa sasa ni kuwaunga mkono UKAWA ambao wameamua kutoka nje ya BMK ili kwenda kuwahamasisha Watanzania kuungana na kupinga udhalimu na ubeberu wa CCM wa kulazimisha Katiba ilingane na matakwa yao yaani SERIKALI 2!

Bado kuna changa moto nyingi sana kuja kuipata Katiba mpya hatimaye Tanzania kwenda kuwa na Uchaguzi Huru na Haki ambao utawapa Watanzania utawala wanaoutaka wao na si kama sasa kuwa kila Uchaguzi ni CCM! Watanzania lazima tujue kuwa KUPIGA KURA ni haki ya Kikatiba ya kila Mtanzania aliye na umri wa MIAKA 18 na kuendelea. Tunataka KATIBA ambayo itatupatia TUME HURU(NEC) YA UCHAGUZI itakayosimamia Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa haki bila upendeleo wala shinikizo lolote toka CCM na Serikali yake kama ilivo sasa.

Tunajua kutokana na Madaraka makubwa aliyo nayo Rais wa CCM amekuwa ndiye anayemteua Mwenyekiti wa TUME YA UCHAGUZI na Wasaidizi wake. Tunajua kuwa Wakurugenzi wa MAJIJI na HALMASHAURI ndiye wanaosimamia Chaguzi zote Kubwa na Ndogo na wote hawa ni Wateule wa Rais wa CCM! Katika mazingira kama haya,hivi Watanzania tunategemea kuja kuiondosha CCM madarakani kweli?? Jibu ni NEVER! Mwenyekiti wa TUME na Wakurugenzi wa Miji na Majiji hawawezi kuruhusu CCM ishindwe hata mara moja! Watachezea matokeo tu ili kuinusuru CCM.

Tunajua DAFTARI LA WAPIGA KURA halijaboreshwa tangu mwaka 2010 kwa maksudi mazima. CCM wanajua kizazi cha Vijana waliokuwa na umri wa miaka kuanzia 13 mpaka 17 mwaka 2010 kwa sasa wana HAKI YA KUPIGA KURA lakini CCM na NEC(Tume ya Uchaguzi) wamenyamaza kimya. Wanajua idadi ya Vijana hawa inaweza kuwa sawa na idadi ya KURA alizopata Rais wa CCM Bwana Kiwete mwaka 2010 ambazo zilikuwa ni kama 5m+. CCM wanajua vijana wanataka mabadiliko wameshachoka na vizee na vibabu vya CCM wanataka vijana wenzao walioko Vyama vingine vya Siasa nje ya CCM kushika Madaraka.

Juzi tumesikia kwenye media mapema mwaka huu kuwa NEC wamepewa Dola milioni 200+ kwa ajili ya KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA lakini mpaka sasa si NEC wala SERIKALI ya CCM wanashughulikia uboreshaji huo. Wamenyamaza kimya kwa makusdi. Wanataka mpaka Uchaguzi wa Serikali za MITAA na Uchaguzi Mkuu ukikaribia ndiyo waanze porojo na longolongo za kuanza kuboresha daftari, lakini ukweli ni kwamba CCM hawana mpango huo kwa sababu wanatka kubakiza idadi ileile waliyoipata mwaka 2010 iendelee kuwepo ili waje kujidai wameshinda kwa kishindo!

Mimi nawaomba UKAWA wanapopita kuelimisha Watanzania kuhusu Katiba Mpya lazima wazungumzie mambo matatu muhimu sana. Kwanza ni UMUHIMU WA KUWA NA TUME HURU YA UCHAGUZI kwenye Katiba tunayoipigania. Pili ni UMUHIMU wa KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA na tatu na mwisho ni UMUHIMU WA KILA MWANANCHI KWENDA KUPIGA KURA SIKU YA UCHAGUZI. Hii itawaamusha Wananchi na itasaidia mbele ya Safari tunapoelekea kwenye Chaguzi hizi muhimu.

Nimalize kwa kuwakumbusha Watanzania kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kwamba tulijiandikisha Watu zaidi ya milioni 20 kulingana na hesabu za Tume ya Uchaguzi-NEC kama si za kuchakachua. Lakini siku ya Uchaguzi ni watu Milioni 8 tu walijitokeza kupiga kura hii ikiwa ni asilimia 40(40%) ya Watanzania wote waliojiandikisha kupiga kura. Rais wa CCM Bwana Kiwete alipata kura 5m+ zilizompa Urahisi(siyo Urais) na hii ni sawa na asilimia 25(25%)ya Watanzania wote waliojiandikisha kupiga kura!!Hii maana yake nini. Kwamba Rais wa CCM yuko Madarakani kwa Kura 25% ya Watanzania waliojiandikisha kupiga kura kwa maana hiyo 75% hawakuitaka CCM iingie madarakani.Hii ni kasoro kubwa lazima iangaliwe na kurekibishwa tunapoelekea kwenye Katiba Mpya na Chaguzi kuu zijazo.

Kuna haja pia ya kuangalia uwezekano wa kutunga sheria kwa Wapiga kura ambayo itambana KILA MPIGA KURA ALIYEJIANDIKISHA kwenda kupiga kura. Kwamba swala la KUJIANDIKISHA NA KUPIGA KURA IWE NI LAZIMA siyo hiari na siku ya kupiga kura atakayekosa kupiga kura kuwe na adhabu iliyo wazi yenye kuainisha adhabu ya kuwaadhibu waliokwepa kupiga kura. Serikali na Tume zinatumia mabilioni kuandikisha wapiga kura halafu mtu anajiandikisha na anaingia mitini. Hii haikubaliki. Tunajua pengine kuna Watanzania wamesha kata tamaa kuwa hata ukienda kupiga kura ukachagua chama tofauti na CCM haitaleta mabadiliko kwa vile CCM lazima watachakachua na kuchukua ushindi. Hii ni kutokana na kama nilivoeleza hapo juu kuwa madhali Rais wa CCM ndiye anayeteua Wakuu wa NEC na Wasimamizi wa Chaguzi zote hilo lazima litokee. Lakini kama hili litadhibitiwa kwenye Katiba Mpya kwa kumwondolea Rais madaraka ya kuteua utitiri wa Viongozi hawa ambao wengi ni Makada wa CCM tatizo la Uchakachuaji litakuwa ni historia!

''UKAWA JUU, JUU, JUU ZAIDI,MSHIKAMANO DAIMA KUTENGANA AU KURUDI NYUMA MWIKO!''
 
Mimi naomba Serikali iaiingilie mikutano ya UKAWA na kama jaji Warioba na Mhe Butiku wasiwe wanafiki wawe mstari wa mbele kudai katiba ya wananchi
 
Amani kwenu wazalendo wenzangu:

Baada ya salaam ningependa kusema kuwa uchaguzi uliopita una mapungufu makubwa sana. Mapungufu mengi ni ya masuala ya kikatiba ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu kuanzia uchaguzi wa 1995. Mapungufu hayo hayakujionyesha sana katika vipindi vya uchaguzi vilivyopita kwa sababu wagombea wa chama tawala walikuwa hawana upinzani mkubwa. Hivyo kasoro zote za kikatiba zilifunikwa na umaarufu wa kihistoria wa CCM. Kwa kipindi cha uchaguzi cha 2015, Tanzania itakaribisha wapiga kura wapya wapatao 1.5 miloni au waliozaliwa mwaka 1995 na baadaye.

Hatutajitendea haki wenyewe na kizazi kipya iwapo tutaendelea kutumia katiba iliyo sasa kama mwongozo wa kuendeleza nchi. Hivyo kwa maombi yangu binafsi, wazalendo wa Tanzania tuanze kusukuma mabadiliko ya kikatiba. Ninapoita wazalendo, nina maana wananchi bila kujali itikadi zao vyama vya kisiasa, dini au ukabila.

Bila ya kutaja matatizo ya katiba yetu, ningependa kueleza toka tumepata uhuru katiba ya Tanzania imekuwa ni kitu kisichoeleweka wazi kwa wananchi. Tuliosoma shule wakati somo la siasa linafundishwa mashuleni, tulikuwa tunafundishwa katiba ya CCM na miongozi ya chama hicho. Hivyo basi kuna uwezekano mkubwa hata wanasiasa wetu wengi hawajui umuhimu wa kitabu hicho.

Hivyo ningependa kufungua ukumbi kwa kuwakaribisha wenye mawazo na nia ya kubadilisha katiba kutoa mawazo yao.

Na vilevile kama kutakuwa na watu wanaotaka kuanzisha jumuia ya kufanya mabadiliko ya kikatiba, naomba mjitokeze.
Kutaka mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya Uchaguz ni fikra za kichama zaidi kwa sababu kuna mambo mengi ambayo sisi wananchi tunataka yabadilike na kusema kweli hili la Muungano na serikali 3 ni sehemu ndogo sana ya matakwa yetu ukifuatilia rasimu ya katiba.

Kuiondoa CCM madarakani kupitia Katiba hii ni hofu mbaya sana ambayo inajenga uadui na ndipo tuliposimama kwa sababu CCM hawatakubali kubadilisha vipengele vya Katiba hii kwa minajiri hiyo, Na Katiba mpya ni kwa manufaa ya wananchi ambao wengi sii wanachama wa CCM, Chadema, wala NCCR na wanachokitaka ni katiba bora yenye uongozi bora. Uzalendo, uwajibikaji, uwazi na sifa zote zenye kuwapa haki kama raia huru wa nchi hii. katiba mpya yenye lengo la kuiondoa CCM pasipo Uwazi na uwajibikaji ni sawa na kubadilisha Ufalme ambao viongozi wengi wanautaka. Kila kiongozi anataka kuingia Ikulu kama kwamba ndiyo sababu ya kuitaka katiba mpya!

Nimewasikia wana siasa wengi wakitaka mabadiliko haya kwanza kwa sababu ya uchaguzi wa mwaka 2015 wakati ni wao ndio wametukwamisha hapa kutokana na siasa zao. Na vipi wananchi wategemee utawala mpya wenye kuwagharimu fedha nyingi, kodi kubwa, misamaha ya kodi kwa mashirika ya nje yenye kuhodhi asilimia 100. Vipi kuhusu sheria ya kuheshimu vyombo na taasisi za ushirika wa jumuiya za wakulima na wafanyakazi? haki za kumwondoa kiongozi katika madaraka anaposhindwa kutekeleza wajibu, haki ya wananchi kumshitaki kiongozi yeyote anaye fisadi kwa kutumia madaraka alokabidhiwa. Miiko na maadili ya Uongozi, Na sheria kuwa msingi wa kutoa haki kwa wananchi wote badala ya Uheshimiwa kuwa kinga dhidi ya sheria. Leo tunalia na Polisi chini ya CCM kesho tulie tena Polisi kuwa chini ya Chadema ikiwa sheria ni zile zile?
 
Kutaka mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya Uchaguz ni fikra za kichama zaidi kwa sababu kuna mambo mengi ambayo sisi wananchi tunataka yabadilike na kusema kweli hili la Muungano na serikali 3 ni sehemu ndogo sana ya matakwa yetu ukifuatilia rasimu ya katiba.

Kuiondoa CCM madarakani kupitia Katiba hii ni hofu mbaya sana ambayo inajenga uadui na ndipo tuliposimama kwa sababu CCM hawatakubali kubadilisha vipengele vya Katiba hii kwa minajiri hiyo, Na Katiba mpya ni kwa manufaa ya wananchi ambao wengi sii wanachama wa CCM, Chadema, wala NCCR na wanachokitaka ni katiba bora yenye uongozi bora. Uzalendo, uwajibikaji, uwazi na sifa zote zenye kuwapa haki kama raia huru wa nchi hii. katiba mpya yenye lengo la kuiondoa CCM pasipo Uwazi na uwajibikaji ni sawa na kubadilisha Ufalme ambao viongozi wengi wanautaka. Kila kiongozi anataka kuingia Ikulu kama kwamba ndiyo sababu ya kuitaka katiba mpya!

Nimewasikia wana siasa wengi wakitaka mabadiliko haya kwanza kwa sababu ya uchaguzi wa mwaka 2015 wakati ni wao ndio wametukwamisha hapa kutokana na siasa zao. Na vipi wananchi wategemee utawala mpya wenye kuwagharimu fedha nyingi, kodi kubwa, misamaha ya kodi kwa mashirika ya nje yenye kuhodhi asilimia 100. Vipi kuhusu sheria ya kuheshimu vyombo na taasisi za ushirika wa jumuiya za wakulima na wafanyakazi? haki za kumwondoa kiongozi katika madaraka anaposhindwa kutekeleza wajibu, haki ya wananchi kumshitaki kiongozi yeyote anaye fisadi kwa kutumia madaraka alokabidhiwa. Miiko na maadili ya Uongozi, Na sheria kuwa msingi wa kutoa haki kwa wananchi wote badala ya Uheshimiwa kuwa kinga dhidi ya sheria. Leo tunalia na Polisi chini ya CCM kesho tulie tena Polisi kuwa chini ya Chadema ikiwa sheria ni zile zile?

Kaka Mkandara salaama !!!!!!!!

Nilianzisha thread hii mara baada ya uchaguzi wa 2010 wakati kukiwa na machafuko ya kupinga matokeo. Na sababu kubwa ni kuwa vyama vya upinzani vilifanya makosa katika kipindi cha 1992-1995. Vilikubali kushiriki katika uchaguzi kwa kutumia katiba yenye mtazamo wa muundo wa chama kimoja. Walifikiri ni umaarufu wao utakaowapeleka madarakani. Matokeo yake walaihalalisha matumizi ya katiba hiyo. Kama Mrema na Lipumba walikubali 1995, kwanini waikatae 2000, 2005, na 2010?

Kutoka na mafanikio ya Mkapa kwenye baadhi ya sekta za uchumi, watanzania wengi walilifumbia macho suala la mabadiliko ya katiba. Nakumbuka tukiwa kwenye ukumbi wa BStimes, watu wengi walijiingiza kwenye mjadala wa nani atakayemrithi Mkapa toka ndani ya CCM. Hivyo mjadala mzima wa mabadiliko ya katiba ulikuwa haupo ndani ya akili za watanzania wengi.

Kwa upande wangu mabadiliko ya katiba ni ya kimsingi zaidi kuliko mabadiliko ya kiuchumi na matatizo ya uchaguzi ya 2010 yalitoa nafasi kwa watanzania kutafuta katiba mpya. Hivyo nilipoanzisha thread sikuwa na mawazo ya serikali tatu au mbili. Nilikuwa na mawazo ya kuwa na katiba inayowapa na kulinda haki zao za kimsingi.

Lakini kutokana na mjadala na unavyoendeshwa nimepata hitimisho kuwa Tanzania ni nchi ya wajinga au kama sio nchi ya wajinga basi uhuru ulipatikana mapema. Watanzania hawana unique experience kama wanavyojidanganya. Kama ni muungano, kuna nchi zimeungana au za mashirikisho. Kama kuwa nchi ya watu wa makabila tofauti, kuna nchi zenye watu wa makabila tofauti.

Hivyo uandishi wa katiba mpya yenye kukidhi mahitaji ya watanzania katika karne ya 21 sio rocket science. Ni common sense na sioni sababu kwanini nchi inatumia gharama kubwa kufanya zoezi ya vitu vilivyo wazi.

Msingi wa katiba ni kumpa raia haki zake za kiraia. Na muundo wa serikali unaingizwa ndani ya katiba hili ulinde haki ya za raia. Kwa watanzania katiba ni muundo wa serikali wa kupata watawala. Huwezi kupata chochote cha maana kwenye watu wenye fikra kama hizi. Huwezi kupata chochote cha maana kwa watu wenye fikra za kutawaliwa na kutawala.

Nyie endeleni. Nimeshachukua gamba la mnyamwezi na hata uraia pacha sitaki kusikia. Na nawapeni ruhusa kwenda Morogoro na kuwauzia wawekezaji makaburi ya mababu zangu.
 
Nilivyo kuelewa kama vile una tetea mawazo ya waliopo madarakani kwa upande mmoja maana ikiwa msingi wa katiba kulinda haki na uhuru vipi mambo haya yajadiliwe kwa upande walio teuliwa na utawala tu?
 
Katiba mpya inavyoelekea haitakuwa na tija maana imegubikwa na malumbano yenye hisia na maslahi ya kivyama
 
Kaka unazungumzia katiba au unaongelea upigaji wa kura? Na usiseme Rais wa ccm sema Rais wa Tanzania kaka,
 
Ni kweli ila swala lamsingi kwa sasa ni watanzania kujua maana hata kinacho endelea kwa bmt ni kama kiini macho aliye kuwa amepewa dhana ya kukusanya maoni ya rasmuya kstiba ni jaji wsriomba siyo sita anachukua maoni ya wanaichi kwa sasa
 
Warioba alipewa majukumu ya kuunda katiba na anefanikisha ;hao mamburura wanaosema ni mawazo yake wamefanya nn au wamezoea kumeza tu na kujaza matumbo kisa tu kawabania .mm mtazami wangu hii kura ya maoni ya katiba ni ya wiz kwanza katiba tunaipigia chapa moja .basi ziwekwe mbili ya kwao na ya warioba ili mwananchi achague kilicho chema kwake. Sio kutuletea mawazo yao na kusema hi ndiyo sahihi.
Pili katiba yao ni Ileile ya zaman hamna kilichobadiliswha
Swaen kabisa hao
 
Mkumbuke hata hiyo mnayoiita katiba ya warioba mnapotosha.. Katiba ni ya wananchi na kwa Hali ya Kawaida zipo hatua zinazofuatwa wakati wa utengenezaj wa katiba sio Tanzania tuuu Bali dunian kote
 
Amani kwenu wazalendo wenzangu:

Baada ya salaam ningependa kusema kuwa uchaguzi uliopita una mapungufu makubwa sana. Mapungufu mengi ni ya masuala ya kikatiba ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu kuanzia uchaguzi wa 1995. Mapungufu hayo hayakujionyesha sana katika vipindi vya uchaguzi vilivyopita kwa sababu wagombea wa chama tawala walikuwa hawana upinzani mkubwa. Hivyo kasoro zote za kikatiba zilifunikwa na umaarufu wa kihistoria wa CCM. Kwa kipindi cha uchaguzi cha 2015, Tanzania itakaribisha wapiga kura wapya wapatao 1.5 miloni au waliozaliwa mwaka 1995 na baadaye.

Hatutajitendea haki wenyewe na kizazi kipya iwapo tutaendelea kutumia katiba iliyo sasa kama mwongozo wa kuendeleza nchi. Hivyo kwa maombi yangu binafsi, wazalendo wa Tanzania tuanze kusukuma mabadiliko ya kikatiba. Ninapoita wazalendo, nina maana wananchi bila kujali itikadi zao vyama vya kisiasa, dini au ukabila.

Bila ya kutaja matatizo ya katiba yetu, ningependa kueleza toka tumepata uhuru katiba ya Tanzania imekuwa ni kitu kisichoeleweka wazi kwa wananchi. Tuliosoma shule wakati somo la siasa linafundishwa mashuleni, tulikuwa tunafundishwa katiba ya CCM na miongozi ya chama hicho. Hivyo basi kuna uwezekano mkubwa hata wanasiasa wetu wengi hawajui umuhimu wa kitabu hicho.

Hivyo ningependa kufungua ukumbi kwa kuwakaribisha wenye mawazo na nia ya kubadilisha katiba kutoa mawazo yao.

Na vilevile kama kutakuwa na watu wanaotaka kuanzisha jumuia ya kufanya mabadiliko ya kikatiba, naomba mjitokeze.


Hee wewe hakuna katiba ya chama,tumedumu kwa mika 53 tukiwa poa ma tunataka tuendeleze mafanikio haya na new katiba hapana chezea wtz,nachosema watz wa sasa tuko understanding umenisoma acha kudanganya wewe toa hoja nyingine!!!
 
Back
Top Bottom