Bra-joe
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,562
- 986
Bibi mmoja kibogoyo alikuwa amelazwa hospitali. Siku moja alimtuma mjukuu wake amletee kashata za karanga, kwa kuwa alikuwa hana meno alifyonza sukari halafu karanga akawa anaweka kwenye kisosi, alipolala nesi akanyata na kula zile karanga. Alipoamka akamuuliza nesi "nani kazitupa karanga zilizokuwa ktk kisosi"? Nesi akajibu "sijui" bibi akamuadithia kwamba karanga zilikuwa kashata na yeye kanyonya sukari kaachia karanga. Nesi nusu azimie.