notradamme
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 2,009
- 452
kwanza niwapongeze wana JF popote mlipo. Nimejaribu kufuatilia thread nyingi katika forum hii na nimegudua kuwa watanzania wengi wanasubili nini Dr. Slaa atasema ili watekeleze. Hii inaonesha ni namna gani watanzania walifanya maamuzi ambayo hayakupewa thamani.
Tumwombee kwa Mungu Dr. Slaa awe na hekima kuu ili aweze kuivusha nchi hii katika vuguvugu hili ambapo hata aliyetangazwa kuwa mshindi hana furaha na urais wake maana wananchi hawamuungi mkono!
Utaona thread zinasema ... Tunangojea Dr. Slaa atamke, tutekeleze. watz wana imani kubwa naye
Hivi vijana wa KITANZANIA,, mtaacha lini kujidanganya na kuishi kwa ndoto?????
nchi haiwezi kukombolewa na vijana wajinga ambao hawataki kuamini ukweli, wanaishi kwa kujipa matumaini hewa, hawajiamini na hawataki kuukubali ukweli na pindi wakiukubali wanataka kuupindisha kwa makusudi.
HUYO BABU YENU SLAA, anajuta ni kwa nini aligombea URAIS, anajua alishindwa na hata viongozi wa chama chake wamemuacha peke yake athibitishe uendawazimu wake(jaribu kumpelekea microphone kiongozi yeyote wa chadema uone atakavyokimbia).
mnasikitisha sana vijana wa kitanzania........
mtabaki kuwa watumwa wa CCM katika nchi yenu
mtabaki kulamba viatu vya wanasiasa uchwara wa chadema mpaka pale kitakapotoweka katika ramani ya nchi
mtabaki mkiuota ukombozi wa nchi huku mkidhani hiyo kazi inatakiwa kufanywa na watu fulani na sio ninyi
mtabaki kuwa wapiga soga vijiweni, wavivu wa kufikiri na msio na utashi wa kuamua.
mtabaki kufikiria kwa kutumia magazeti na wala sio kwa kuzifikirisha bongo zenu
utashi wenu utaongozwa na imani za kidini (dini za kikoloni) na sio uwezo wa akili zenu kuchanganua mambo
hamtaacha kulalamika,hamtaacha kujidanganya, hamtaacha kujipa matumaini hewa,hamtaacha kuamini watu wasioaminika,hamtaacha kukabidhi hatma yenu mikononi mwa wanasiasa, hamtaacha kusujudia na kuabudu wasiostahili na HAMTAKUWA NA UWEZO WA KUUKABILI UKWELI NA HIVYO KUTOKUWA TAYARI KUPAMBANA NAO kwani vijana wengi wa kitanzania hususan wasomi ni COWARDS.