Neno La Leo: Pinda’s Paradox!

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu Zangu,


PARADOX ni ile hali ya maelezo kupingana yenyewe. Kutokuwepo na lojiki ya jambo zima. Haujapita mwezi tangu pale Waziri Mkuu Mizengo Pinda alijitokeza hadharani na kuunga mkono hudumna ya tiba ya Babu wa Loliondo ikiwemo madai ya Babu mwenyewe, kuwa dawa yake inatibu UKIMWI mbali ya maradhi mengine mengi.

Ni heri Pinda angekaa kimya, maana, Juni mwaka huu Umoja wa Mataifa unaadhimisha miaka 30 ya mapambano dhidi ya UKIMWI. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon alikuwa Kenya majuzi kuzindua mwanzo wa maadhimisho hayo ambayo kidunia yatafanyika Kenya.


Na leo Waziri Mkuu Pinda anatarajiwa kuzindua Mkakati wa Taifa wa Kinga ya UKIMWI (2009-2012), pamoja na Mpango Kazi kuhusu Jinsia na UKIMWI (2010-2012).


Tunaambiwa, kuwa uzinduzi huo unafanyika ikiwa ni moja ya sehemu ya ushiriki wa ugeni wa Naibu Katibu Mkuu, Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kushughulikia UKIMWI (UNAIDS) Bw. Michel Sidibe.


Tunaambiwa pia, kuwa wakuu hao wa Umoja wa Mataifa wako nchini kwa ziara ya siku mbili kuongeza hamasa kwa nchi za Afrika kutilia mkazo zaidi kinga ya UKIMWI ili kupunguza maambukizo mapya hadi kufikia sufuri hasa wa kizazi kipya, ifikapo miaka mitano ijayo, pamoja na kuhakikisha kuwa vifo vitokanavyo na UKIMWI navyo vinapungua.


Ukweli ni huu, kuwa kwa Serikali yetu kushadidia tiba ya Babu wa Loliondo kabla hata haijathibitishwa kitaalamu kuwa inatibu UKIMWI inachangia katika kuongeza maambukizi mapya ya UKIMWI, maana, kuna Watanzania leo walioaminishwa kuwa tiba ya UKIMWI imeshapatikana. Wanaendeleza ngono zembe, si kuna ‘ Kikombe Cha Babu!’.


Mbaya zaidi, Serikali kupitia Wizara ya Afya haijaweka msisitizo kwa wanaotumia ARV's kuendelea kutumia dawa zao hata baada ya kikombe cha Babu. Hili ni pigo kubwa katika mapambano yetu dhidi ya UKIMWI.



Kwetu Watanzania hiki kinabaki kuwa kizungumkuti, a paradox! Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid
Iringa,
Jumatatu, April 4, 2011
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
 
Si ndiyo hawa ulikuwa unawashabikia wachaguliwe? ili iwe nini sasa? CCM itaondoka na mizoga yake yote
 
Sasa huu ni upuuzi nadhani.badala ya kuongelea hoja iliyopo mtu anaongelea uchaguzi.what is this
 
Maggid,hiyo imeshakua ni kawaida kwa wanasiasa wetu hasa hawa wa Chama tawala,matamko yao hayaendani na matendo kwa kuwa wanaangalia zaidi msukumo wa kisiasa badala ya hali halisi.Wanataka waridhishe watu bila kufikiri madhara ya upande hasi.Mbaya zaidi kwa huyu PM wetu amezoeleka kwa kuongea bila hata kujali sheria inasemaje,mfano mauaji ya albino na bomoa bomoa ya Magufuli.
 
... na huyo ndiye Mtoto wa Mkulima niliyepata kumuamini sana sana miongoni mwao wanasia wetu nchini!!!!!!!!!!
 
Mimi sijaiona hiyo paradox hapa. Ingekuwa paradox kama Pinda angekuwa amehubiri kitu kimoja na huku akifanya kingine. Yeye kama msimamizi wa shughuli za serikali alikuwa na wajibu wa kufanya wale wanaoamini kwamba kuna tiba mbadala basi waipate bila usumbufu au adha yoyote. Tiba za namna hii zimekuwepo kila mahali na wala hazikinzani na juhudi za serikali na hata mashirika ya kimataifa katika kupambana na ukimiwi. Afterall, kikombe cha babu kinatibu magonjwa(kwa wale wanaoamini) mengi kuliko huo ukimwi. Mimi nafikiri babu na hao UNAIDS au mwingine yeyeote wana lengo moja la kutafuta suluhu ya janga hili zito na kuwasaidia wananchi kupata nafuu. Hata babu mwenyewe amekwa akisisitiza kwamba ukitibiwa na ukapona, ukiambukizwa tean huwezi pona. Hao wa ngono zembe wamekuwepo hata kabla ARVs hazijaaanza kusambazwa.
 
... na huyo ndiye Mtoto wa Mkulima niliyepata kumuamini sana sana miongoni mwao wanasia wetu nchini!!!!!!!!!!

Ulikurupuka kumuuamini kabla ya kumfanyia tathmini na kumjua zaidi; sasa nadhani unamfahamu vya kutosha kutokana na matamshi yake tata ikiwamo ya kuwaogopa hao waliomuweka madarakani yaani MAFISADI!!
 
Kweli hili ni neno la leo, watu wamehamishia akili zao kwa babu na wamesahau mambo ya msingi bila kujali ufanisi wa tiba ya babu! Media zote ziko kw a babu, ufisadi na hali ngumu ya maisha isababishwayo na utawala mbovu viko kando kwanza,ama kweli kazi na dawa!
 
Sasa huu ni upuuzi nadhani.badala ya kuongelea hoja iliyopo mtu anaongelea uchaguzi.what is this

Mkuu kwa jicho lako umeona kuwa ishu ya uchaguzi ndo iliyoandikwa.. Heshimu maoni ya wenzako usiyaite upuuzi, ni bora ungetafakari kidogo ili ufaham utoke vp.
 
Sasa huu ni upuuzi nadhani.badala ya kuongelea hoja iliyopo mtu anaongelea uchaguzi.what is this

Angalia hili jinga, sasa na wewe umechangia hoja gani kwenye thread hii? Maggid ni mpiga debe wa CCM, kwahiyo aliemuuliza yuko sahihi kwa 100% haiwezekani tuchague kama majuha halafu tuanze kulalama kama wehu.
 
Sasa huu ni upuuzi nadhani.badala ya kuongelea hoja iliyopo mtu anaongelea uchaguzi.what is this
Kuna ubaya gani kuuhusisha uchaguzi na viongozi?Uchaguzi sindio unaozaa UONGOZI au mkuu umetafasiri kiaje?Hivi mkuu unaona Pinda anasimama kweli kama waziri mkuu au wameziba nafasi tu walau siku ziende?believe or not Tanzania tuna ombwe la uongozi.
 
Kwangu mimi Pinda ni aina ya wale viongozi wanaobadilika badilika hivyo tuwe naye macho kwa maana kwa misimamo ya aina hii mmh! sidhani kama tutafika, tutafikeje kama mtendaji mkuu wa serikali anajiparadox? , Asante sana kaka Mjengwa(mdogo wako Nova Kambota)
 
MAGGID AND 'THE PINDA PARADOX ON LOLIONDO AIDS CURE' CLAIMS SIMPLY CAN
NOT BE OVERSTATED ANY BETTER


Ndugu 'The Paradox' is just but so wide and glaring here on the Pinda claims of 'Kikombe Cha Babu' on AIDS and his latter defiance to NOT to speak when he had a duty to do so with the visiting UN high-profile entourage with regard to the scouge.

Ndio, Mhe Pinda kahubiri kwa Watanzania juu ya usalama, uhakika na tumaini jipya kwa 'Kikombe Cha Babu wa Loliondo' kutibu magonjwa yote ikiwemo UKIMWI.

Hadi hapa kunapotokea ujumbe mzito wa UN nchini (Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiandamana na Mkurugenzi wa UN kitengo cha Mashirika ya kushughulikia UKIMWI dunia) na kumualika yeye mwenyewe Mtoto wa Mkulima kwenda kuzindua hili na lile kitaifa kwa niaba ya umoja huo, wala Mhe Pinda hakuchukua nafasi ya kuwafahamisha UN kwamba hivi karibuni tu Tanzania tumejikomboa kwa kugundua dawa.

Kwa kuwa huo ndioujumbe halisi ulioenea kila mahali nchini kwamba kuna dawa ya UKIMWI Arusha na hata serikali imethibitisha hilo; na vijana kusadikika kuanza kuchukua hatua zaidi kwa ngono zembe wakijua tiba ni nauli ya kwenda na kurudi Arusha pamoja na nauli ya baiskeli kufikishwa kwa Babu Loliondo basi unaambiwa sasa hivi kuna moto mkubwa wa ngono isiosalama nchini huku wakidai hadi mawaziri kibao wa CCM wameonekana kupata tiba kwa Tsh 500 tu kwa kikombe huko badala ya kwenda kubadilisha damu kwa bei kubwa Ulaya.

Nasema kwamba pamoja na kwamba CCM walionelea vema kututafutia kitu cha kutuweka bize kama taifa (baada ya kugundua kwamba siku hizi TBC1 na Ze Komedi hazipandi) ili tusilijadili jambo la msingi la Muswada kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya kwa namna tuipendavyo, nadiriki kusema kwa kumunga sana mkono Maggid Mjengwa kwamba endapo serikali haina uthibitisho wa ki-sayansi juu ya tiba ya 'Kikombe Cha Babu' kwa UKIMWI basi kutumika kule kusivyo juu ya huyu babu kwa maslahi ya muda mfupi kisiasa huenda itatugharimu ajabu ki-nguvu kazi na hela ya kuagizia ARVs kwa kundi kubwa zaidi nchin.

Hakika Mhe Pinda alipashwa kueleza ule ujumbe wa UN, kabla ya yeye kuwakubalia na kushiriki uzinduzi wao juu ya miradi zaidi kudhibiti UKIMWI nchini, kwamba wenzenu huku Tanzania kama ni dawa ya UKIMWI Mungu keshatujalia hivyo janga hili wala si tishio tena na hakuna hata haja kutusaidia zaidi maana Babu wa Ukweli yupo kule kwenye misitu yetu ya kuleee Loliondo akichuma zake jani fulani hivi na kugawa dozi ya uhakika ya 'Chikombe Cha Babu' kutwa mara tatu kwa siku mbili tu na mtu kupona kabisa.

Kwangu mie nionapo ujumbe mzaito kama huu peke yake basi tayari inatuambia kwa Tanzania hatuko shwari kitakwimu wa UKIMWI huko kwa wenzetu UN.

Mimi sijaiona hiyo paradox hapa. Ingekuwa paradox kama Pinda angekuwa amehubiri kitu kimoja na huku akifanya kingine.

Yeye kama msimamizi wa shughuli za serikali alikuwa na wajibu wa kufanya wale wanaoamini kwamba kuna tiba mbadala basi waipate bila usumbufu au adha yoyote.

Tiba za namna hii zimekuwepo kila mahali na wala hazikinzani na juhudi za serikali na hata mashirika ya kimataifa katika kupambana na ukimiwi. Afterall, kikombe cha babu kinatibu magonjwa(kwa wale wanaoamini) mengi kuliko huo ukimwi.

Mimi nafikiri babu na hao UNAIDS au mwingine yeyeote wana lengo moja la kutafuta suluhu ya janga hili zito na kuwasaidia wananchi kupata nafuu. Hata babu mwenyewe amekwa akisisitiza kwamba ukitibiwa na ukapona, ukiambukizwa tean huwezi pona.

Hao wa ngono zembe wamekuwepo hata kabla ARVs hazijaaanza kusambazwa.
 
Upupu mtupu. Sasa hivi ndo unajifanya kutafuta sapoti hapa jamvini. Kaendelee na kampeni za ccm. Njaa hizi, we acha tu! Kile cheo ulichokitegemea kimeota mbawa nini? Mwenzio michuzi kaula, na wewe subiri tena miaka mi5 ijayo ujaribu bahati yako. unaweza ukaenda RFA au DW, who knows?
 
Upupu mtupu. Sasa hivi ndo unajifanya kutafuta sapoti hapa jamvini. Kaendelee na kampeni za ccm. Njaa hizi, we acha tu! Kile cheo ulichokitegemea kimeota mbawa nini? Mwenzio michuzi kaula, na wewe subiri tena miaka mi5 ijayo ujaribu bahati yako. unaweza ukaenda RFA au DW, who knows?

Ndugu Mkeshaji,

Huo ni mtazamo wako. Na mimi sitauita upupu hata kama sikubaliani nao. Si hulka ya waungwana.
 
Hebu tupe kidogo hiyo ya Michuzi.

Na wewe Maggid kweli huwge unaeleweka si tu uandishi maslahi binafsi ambayo hivi sasa inamuumiza mzee wetu Prince Bagenda tangu tumtaje hapa JF wiki jana katika kula njama dhidi ya sisi Watanzania wenzake na hatimaye kilichomkuta UDSM pale ukumbi wa Nkuruma siku ya Jumamosi.

Will you do something about being a reliable defender of ordinary Tanzanians with your pen sir?

Upupu mtupu. Sasa hivi ndo unajifanya kutafuta sapoti hapa jamvini.

Kaendelee na kampeni za ccm. Njaa hizi, we acha tu! Kile cheo ulichokitegemea kimeota mbawa nini? Mwenzio michuzi kaula, na wewe subiri tena miaka mi5 ijayo ujaribu bahati yako.

Unaweza ukaenda RFA au DW, who knows?
 
Hebu tupe kidogo hiyo ya Michuzi.

Na wewe Maggid kweli huwge unaeleweka si tu uandishi maslahi binafsi ambayo hivi sasa inamuumiza mzee wetu Prince Bagenda tangu tumtaje hapa JF wiki jana katika kula njama dhidi ya sisi Watanzania wenzake na hatimaye kilichomkuta UDSM pale ukumbi wa Nkuruma siku ya Jumamosi.

Will you do something about being a reliable defender of ordinary Tanzanians with your pen sir?

Ndugu Uwezo Tunao,

Asante sana,
Mimi ni Maggid, na siku zote nimekuwa hivyo. Namsifu sana John Mnyika. Mwanasiasa anayekwenda na wakati. Yeye hakusubiri tangazo langu la kuwataka wanasiasa na vyama kutangaza habari zao za uchaguzi bila malipo kwenye Mjengwablog. Mnyika ndiye MwanaCHADEMA pekee ambaye aliweza kutuma habari na picha za matukio yake nyingi kwenye Mjengwablog, na hakuna hata senti tano niliyomwomba kwa ajili ya vocha. Kamwulize John Mnyika. Tatizo letu Watanzania ni wepesi sana wa kulalamika na kutuhumu bila kuuliza kwanza au kuumiza vichwa. Ndivyo tulivyo.
 
Maggid mjukuu wangu, unaniskitisha kitu kimoja, kwa nini unang'ania sana hoja yako na kusisisitiza kupita kiasi.

Ilitosha kutoa maoni yako kuusu tiba ya loliondo na tukakuelewa, lakini kwa sababu zisizoeleweka kila kukicha ni babu babu babuuuuuuuu, mpaka inakera.
I swear maggid nimeacha kutembelea blog kwa ajili ya hili its too much, kama hukubaliani nalo tumeshakuelewa.

Naomba uache double standard, kuna mambo mengi yanayosumbua taifa hili ufisadi, kukosa uwajibikaji, kutokuwa na uzalendo n.k. nadhani ungeweza kutumia muda wako kuyaongelea haya ungetusaidia, sijui kwa nini unakuwa king'anganizi hivi, inakera eti.

Sikupangii cha kufanya, ila nakushauri tu kuwa " mhitimu ahitimu shahada kwa ujuzi wa topic moja"
 
Maggid mjukuu wangu, unaniskitisha kitu kimoja, kwa nini unang'ania sana hoja yako na kusisisitiza kupita kiasi.

Ilitosha kutoa maoni yako kuusu tiba ya loliondo na tukakuelewa, lakini kwa sababu zisizoeleweka kila kukicha ni babu babu babuuuuuuuu, mpaka inakera.
I swear maggid nimeacha kutembelea blog kwa ajili ya hili its too much, kama hukubaliani nalo tumeshakuelewa.

Naomba uache double standard, kuna mambo mengi yanayosumbua taifa hili ufisadi, kukosa uwajibikaji, kutokuwa na uzalendo n.k. nadhani ungeweza kutumia muda wako kuyaongelea haya ungetusaidia, sijui kwa nini unakuwa king'anganizi hivi, inakera eti.

Sikupangii cha kufanya, ila nakushauri tu kuwa " mhitimu ahitimu shahada kwa ujuzi wa topic moja"

Ndugu Yangu Babu Wa Loliondo,

Ahsante, lakini tambua, kuwa na ' Babu Wa Loliondo' kuna ufisadi, kukosa uwajibikaji na kukosa uzalendo!
 
Back
Top Bottom