Neno Kabla ya IT & COMMUNICATION SUMMIT 2010

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Wakati ambapo Watanzania wakijiandaa na Ufunguzi wa IT & Communication Summit , Nchini Kenya wiki hii Kumefunguliwa kituo cha TEKNOHAMA ambapo wadau mbalimbali wa Fani hiyo wanaweza kwenda kutumia vifaa vya vituo hivyo kwa ajili ya kazi zao mbalimbali haswa kwa wanafunzi ambao wanahitaji kufunza zaidi na wale wanaopenda kujiajiri wenyewe mradi huu uko chini ya Ushahidi.com Hii ni hatua nzuri sana kwa Kenya na afrika mashariki kwa ujumla .

Pia Kampuni kadhaa za mawasiliano ya mtandao yameahidi kusaidia katika kuhakikisha kituo hicho kinapata huduma ya mawasiliano bure kwa siku zao zote za kazi .

Uganda napo serikali ya nchi hiyo itaanza kuwapa ardhi bure wadau wa TEKNOHAMA lakini hii itafanyika kwa wale wenye miradi inayoeleweka ya kibiashara ambayo inaweza kusaidia jamii za sehemu ambapo mdau husika yupo haswa vijijini na sehemu zingine ambapo teknologia hii iko nyuma kidogo hii itakuwa changamoto sana kwa wadau mbalimbali wan chi hiyo kuja na mawazo miradi na mambo mengine kwa faida ya jamii zao .

Mambo hayo yakiwa yanaendelea kwenye nchi za wenzetu tena jirani zetu kuna mambo ambayo sisi kama watanzania yatupasa kujiuliza mipango yetu ya TEKNOHAMA mpaka sasa hivi inaendeleaje je yale ambayo yalipendekezwa miaka 5 iliyopita yamefikia malengo au kutekelezwa hata kidogo tu tunaweza kuona nyota njema ikingaa mbele zetu ?

Kwa kuanzia tunaweza kuangalia upya kama TCRA Taasisi inayohusika na mawasiliano nchini kwa ujumla kama imeweza kufikia malengo yake iliyojiwekea na kama bado inafaida kwetu kama taifa au kuwe na taasisi nyingine mama iliyohuru katika utendaji wake wa kazi mbalimbali zinazohusu mawasiliano , kwa kweli Hii Taasisi ni ya kuangalia kwa macho makali , lazima ifanyiwe mabadiliko ili iwe ya kisasa iweze kuendana na wakati wa sasa kwenye Sekta ya Mawasiliano Kuna hitajika platform Mpya ya kuendesha mfumo mzima wa mawasiliano Nchini

Imeonekana Umeme kuwa Tatizo sugu sana katika utendaji wa Masuala mengi ya TEKNOHAMA , hapa ninapoandika hii barua fupi niko Katikati ya Jiji zaidi ya Nusu ya Jiji lote la DSM halina umeme kwa masaa 4 sasa na hali hii imekwepo toka mwaka jana hii ina maana shuguli nyingi za teknohama haziwezi kuendelea kama ilivyo labda kwa wale wenye uwezo wa kuwa na vifaa vya kuzalishia umeme lakini hii inaweza pia ngumu kwa wale wasiokuwa na uwezo .

Kitu cha mwisho ni kwa wadau mbalimbali kufikria sasa kuwa na Contents zinazohusu mambo yetu kwenye wavuti zao suala hili limeonekana kuwa gumu kwa wengi wetu lakini naamini siku zijazo kunaweza kuwa na mabadiliko makubwa tukiamua kuwa na contents zetu .

Na ushirikiano kati ya watu wa TEKNOHAMA Umekuwa hafifu sana wengi hawaaminiani - Hili siwezi kuliongelea kwa mapana lakini nawaomba wana TEKNOHAMA tuzidishe ushirikiano wa kazi za kila siku ili tusogeze taifa hili Mbele ,Lakini kutokuwepo Taasisi ya kutambua wataalamu mbalimbali kwenye TEKNOHAMA imechangia sana suala hili .
 
Hakika nakubaliana na Shy, Jumanne nilisikia BBC Swahili wakitangaza kuhusu ihub,na tunajua Ushahidi imepata umaarufu kote duniani - si kitu cha ajabu ni idea iliyozaa software yenye practical use katika global scale.

Taznania tunakosa focus na priority ya nini muhimu cha kufanya kwa taifa kuweza kushindana na majirani zetu na hata nje ya mipaka ya Afrika.

Nimekuwa nikifanya utafiti kwa muda sasa katika kuandaa mipango ya mradi wa kuhamasisha IT Tanzania bara na Zanzibar, nilichogundua ni kwamba Kenya wametuacha kwa umbali mrefu sana, wakifuatiwa na Rwanda hata Uganda - kwenye hiyo league sisi tuna-face relegation.

Kenya wamepiga hatua kubwa na wanaendelea kupiga hatua zaidi ikiwa ni pamoja kuandaa mipango ya serikali na sekta binafsi na isiyo binafsi. Mfano wameandaa Malili Technopolis Concept Paper eneo maalum nje ya Nairobi kuwa business park ya IT projects - exclusively.

Sisi ardhi tunayo, mfano Kigamboni - ingetumika kwa kiasi fulani kuandaa mipango ya baadaye iwe IT business park.

Sera zetu za IT zipo kwenye makabrasha, lakini utekelezaji kama upo basi hauko wazi - na serikali is not leading us - then individuals tunaweza kujisukuma wenyewe.

Hatupo creative! Natoa changamoto kwa walio tayari (kama induviduals tutakaofanya umoja) tukusanye mawazo tufanye kitu cha kuanzia, mpaka mwisho wa mwaka tuwe na ukurasa wa kwanza.
 
Kwangu mimi Taasisi kuu inayohusika na usimamizi wa masuala ya Mawasiliano Tanzania imeshindwa kazi hii ni wajibu wa vigogo wa taasisi hii kujiuzuru mara moja kuachia madaraka hayo watu wengine ambao wataweza kuja na mambo mapya au hata kuendeleza mapendekezo ambayo yaliwahi kutolewa kwa vitendo na ionekane inafanya kazi .

Mfano rahisi ni hili suala la Kuwa na sheria za Mitandao , wanasheria wa Taasisi hii wamezunguka karibu dunia nzima kuona nchi nyingine wanafanya nini , wamewakilisha walichoandika katika semina mbalimbali lakini wanapotoka nje ya ukumbi vitu vile huishia pale pale juzi juzi hapa mmoja wa wanasheria hao wakaomba labda kwenye semina na mikutano mengine ya teknohama tuwe tunaalika wanasiasa ili waweze kutusaidia kupigia kelele suala hili bungeni .

Pesa za ummah zinatumika kusafirisha watu hawa kwenda kwenye nchi hizo kwa ajali ya kupata uzoefu na maarifa kwa mategemeo kwamba wanaweza kuja kufanya mapinduzi kwao lakini wapi na muda unazidi kwenda kizazi kijacho kitatulaumu sisi kwa kulea uongozi huu

Pamoja na hayo kumekuwa na vitu mbalimbali vinapitishwa Na taasisi hii bila kupata maoni ya walio wengi na bila kuwa na sheria za kudhibiti masuala hayo mfano ni Huu usajili wa Namba za simu sijui mjadala ulifanyikia wapi na taarifa ilitolewa wapi nilisikia morogoro sijui lakini vitu vimepitishwa wananchi wanashangaa tu Tunaburuzwa Taasisi imeshindwa kazi wasimamizi waachie ngazi mara moja wakubali kushindwa majukumu wenyewe hatutaki kusimama kwenye geti lao na mabango ya kuwalazimisha kuachia ngazi .

Hayo niliyotaja hapo juu ni machache sana kuna mengine yatakuja baada ya usajili wa simu kukamilika .
 
Back
Top Bottom