Nehemia Mchechu- Bosi Mkuu Shirika la Nyumba Tanzania [NHC]

Unlike other political posts kama Uwaziri n.k hii post ni ya utendaji. Kama kweli ni mtendaji mzuri kama wengi wanavyodai hapa muda si mrefu tutaanza kuona matunda yake. That said...

NHC ni mojawapo ya Mashirika machache yaliyo past expire date ambayo bado yanatukumbusha siasa za Ujamaa. Sababu hatuko tena kwenye Ujamaa kwa vitendo, basi ni vema tukaachana nalo. Tukijiuliza hili shirika linamnufaisha nani kwa sasa hakuna mwenye jibu...Badala yake warekebishe mfumo mzima wa ujenzi Tanzania. Wafanye haya na mengine...

1. Harakisha Tin Number/ Social Security/National Insurance Number kwa kila raia.
2. Tuweke mfumo mzuri mikopo kwenye Mabenki,
3. Ondoa/Punguza Kodi kwenye malighafi na mashine za Ujenzi,
4. Weka misingi mizuri ya vibali na usimamizi wake kwenye ujenzi,
5. ....
6. ....

Sit back and watch, Wananchi wakijenga nyumba zao wenyewe tena kwa ufanisi.

Huwezi kufanya number mbili kama huna namba 1. Na hilo ndio linatuumiza sana.
 
Mkuu wewe endelea kukaa tu huko Pasadena ya NHC tuachie wenyewe. Endeleeni na financiers wenu huko huko California, pili pili iko Tanzania wewe inakuwashia nini? Wacha watu watoe maoni yao.

..na kukaa kwangu pasadena nafikiri nina mchango mkubwa katika maendeleo nyumbani kuliko wewe unayeishi Tandika na akili yako ya kuku.
 
Kwanza naomba nikupe hongera Nehemia binafsi nimewahi kukutana na wewe katika moja ya conference east africa. This guy ni mtu very bright to be honest. Ila hongera zangu naomba ziishie hapo kwani pana kazi kubwa mbele yako. Kwakuwa wewe ni mtu mchapa kazi hongera yangu kamilifu nitakupa ukilibadilisha shirika kuwa la kibiashara na lenye kuleta mabadiliko Tanzania.

Watu wengine kabla hatujawa critical kwa mtu tumpe nafasi ya utendaji wake. Tuache kuwa watu wa kulaumu badala yake tumpe nafasi ya utendaji wake. Wazee katika bodi mie nadhani sio tatizo (kama wabunge ndani ya bodi hawa ndio wanaua mashirika). Kuwa na wazee ndani ya bodi actually ni faida kwani wanakuwa na experience ya kutosha na huwa busara katika maamuzi mengi kwani sie vijana ni very ambitious. Hivyo sioni tatizo la wazee katika bodi ila wanasiasa ndio hatari.

Nilikuwapo!!!
 
Hongera sana ila ana kazi kubwa sana katika kuliweka sawa shirika hilo huko Tanzania.

Mkuu mimi nashangaa kwanini watu wanakimbilia kusema ulaja wakati ukweli wa mambo ni kuwa hilo ni shirika muhimu sana na lihitaji kazi sana. Inawezekana jamaa anaenda kufanya kazi ya kukusanya kodi na kupaka rangi nyumba badala ya kufanya kazi anazotakiwa kufanya.

Kuliwekwa shirika sawa ni kazi kubwa sana, ingekuwa vema kama tukianza kwa kumpa moyo na kujiandaa kumpa maoni na kumpa uungaji mkono kuliweka sawa shirika ambalo ni almost limeoza.
 
Poleni sana na Nehemia wenu, ninavyojua hakuna mtu anayeteuliwa kuwa Managing Director wa Nationa Housing bila kuwa na uhusiano na mafisadi.

Kwa muda mrefu wakurugenzi wote wa National Housing walikuwa wanateuliwa kwa kigezo cha kujikomba kwa lowasa, haruna mahesabu alikokotwa toka ardhi university, kila mtu akamsifu mtusi yule, leo wamemficha kule ewura asije gundulika kuwa si mtusi.

Kuna mtu anaitwa Chidiel Mmbaga yeye aliandaliwa hiyo nafasi kwa muda mrefu kwa sasa yeye ni director of real estates, ameoa mtoto wa mwinyi,mzee ruksa, sasa inaonekana kundi la lowasa limezidi kete hili la mwnyi.

For your information, managing director wa NHC corporation angepaswa kuwa mtu aliyesomea either estate management, au real estates, huyu nehemia wenu sana sana angekuwa director of finance. KWA KIFUPI UTEUZI WAKE NI MWENDOLEZO WA UFISADI TENA, POLENI HUU SI WAKAKATI WA KUANGALIA ETI CLASS MATE WANGU KATEULIWA, ANGALIA MCHAKACHO WA KUTEULIWA KWAKE KAMA NI MSAFI.

NI WAKATI WA KUWANYANGANYA HAKI ZA KUTEUA WATEULE WAO, NA NAFASI HIZI ZIJAZWE KWA MANUFAA YA WANANCHI
Tena huyu kijana ni aina ya akina Mafuru wa VodaCom, Mndolwa wa DAWASCO,........Wabeba mikoba wazuri wa wakubwa na mafisadi wakubwa watarajiwa.
 
Tena huyu kijana ni aina ya akina Mafuru wa VodaCom, Mndolwa wa DAWASCO,........Wabeba mikoba wazuri wa wakubwa na mafisadi wakubwa watarajiwa.
WHAAATT!!!!!
Inatisha manake vijana wachapakazi wabeba mikoba wapo wengi sana, kama na hao uliowataja wamo basi tumekwisha, manake wanakuja wengi tu wako njiani wengine wako mbali zaidi, kazi ipo!!! (there is job!!) huwa tunakuja kushtuka wakishakuwa mawaziri (masikini Tanzania yetu)
Anyway, nasikia ni mchapa kazi.

I wish all the best, punguza idadi ya watu unaowebebea mabegi,
onyesha jinsi vijana wanavyotakiwa kuijenga nchi kwa matendo na sio kwa maneno.
Onyesha jinsi utajiri na heshima inavyoweza kupatikana kwa kuchapa kazi sio kwa kutamani na kutega kazi na kuiba vihela,
Onyesha mfano kuwa ushirikina na majungu kazini hayajengi
Onyesha kuwa watanzania tunaweza kuwa na plans na tunaweza kuzisimamia (I trust you will see this to the end)
Mungu akulinde
 
WHAAATT!!!!!
Inatisha manake vijana wachapakazi wabeba mikoba wapo wengi sana, kama na hao uliowataja wamo basi tumekwisha, manake wanakuja wengi tu wako njiani wengine wako mbali zaidi, kazi ipo!!! (there is job!!) huwa tunakuja kushtuka wakishakuwa mawaziri (masikini Tanzania yetu)
Anyway, nasikia ni mchapa kazi.

I wish all the best, punguza idadi ya watu unaowebebea mabegi,
onyesha jinsi vijana wanavyotakiwa kuijenga nchi kwa matendo na sio kwa maneno.
Onyesha jinsi utajiri na heshima inavyoweza kupatikana kwa kuchapa kazi sio kwa kutamani na kutega kazi na kuiba vihela,
Onyesha mfano kuwa ushirikina na majungu kazini hayajengi
Onyesha kuwa watanzania tunaweza kuwa na plans na tunaweza kuzisimamia (I trust you will see this to the end)
Mungu akulinde
Ndugu yangu,
Nchi hufiki popote kama haujaonyesha kwa vitendo unawajali vipi wakubwa na mahitaji yao yasiyoisha na tamaa za ajabu walizonazo. Unaweza ukawa mchapakazi, ukawa na elimu ya kutosha, ukajituma sana lakini sifa hizo pekee zisikufikishe popote. Hivi kweli mle ndani ya NHC hakukuwa na aliyestahili kupewa nafasi hii?
 
Nampongeza sana Mchechu kwa uteuzi huo alioupata. Ni matarajio yangu kuwa atalifanya NHC liwe shirika la watu kwa masilahi ya umma wa watanzania.

Mortgage financing natumai itapata chachu ya kutekelezeka kwa vitendoo kupitia NHC chini ya uongoziiii.....

All the best.
 
Acheni chuki jengeni hoja kwanini Nehemiah hafai kwa nafasi hii. Mambo ya ubeba mikoba yanatoka wapi. Jamaa historia yake y autendaji uliotukuka nauaminifu inajitosheleza sana. Ndiyo maana hata kwenye private sector kafanikiwa bila kubebwa.

Mtu akifanikiwa private sector bila kubebwa ujue ni mchapakazi kwelikweli,serikalini watu vyeo wanabebana tu. Unatakiwa uwe mzuri kwa wanasiasa ili ufanikiwe,lakini si private sector.
 
Hongera kijana, please do us proud.

Kwanza ningependa kujua vision ya hili shirika ni nini hasa? Maana kuna wakati walianza kuuza nyumba, mara wakaacha sasa sielewi, what is the plan? Na hii plan ni CEO atakayeipanga au itatoka Wizarani somewhere?

Pili nothing personal, simjui huyu jamaa kabisa.
Ila kama pessimist lazima nijiulize kwanini mtu aache kazi ya CEO CBA, atose offer za Kenya Commercial then aende NHC?!! Sidhani kama serikali inaweza kumatch hizo kampuni kwenye mshahara/benefits. What is his motivation here?
 
Acheni chuki jengeni hoja kwanini Nehemiah hafai kwa nafasi hii. Mambo ya ubeba mikoba yanatoka wapi. Jamaa historia yake y autendaji uliotukuka nauaminifu inajitosheleza sana. Ndiyo maana hata kwenye private sector kafanikiwa bila kubebwa.

Mtu akifanikiwa private sector bila kubebwa ujue ni mchapakazi kwelikweli,serikalini watu vyeo wanabebana tu. Unatakiwa uwe mzuri kwa wanasiasa ili ufanikiwe,lakini si private sector.
Angefanikiwa hivyo unavyomwelezea asingeondoka huko. Unadhani Dr Kimei anaweza kuiacha CRDB baada kuifikisha hapo ilipo? Kuteuliwa kuongoza Taasisi yoyote ya UMMA kwa sasa ni lazima uwe "mtiifu" kwelikweli kwa wanaokuteua.
 
Mmeshaanza, watu wataanza kuvuta undugu, urafiki, ujirani, ukwe, ushemeji kwa kina Luhanga, watu bwana.

Hongera Nehemia

Mkuu Ama. I. I hate nepotism. Everything by merit. Na huwa sijipendekezi, sina undugu wala uhusiano wowote na Nehemiah zaidi ya ule uhusiano wa utaifa (watanzania, wazalendo). Nipo hapa kusema yale niyafahamuyo kuhusu utendaji wake. Utajuaje kama pengine nilishafanya naye kazi. Mambo mengine ni private. Bottom line, he is a performer. Na nitatamani watoto wangu na ndugu zangu wawe performer waonekane na si kubebwa.

Tumwombee Mungu aweze kupambana na ile hali tete ya lile shirika lililojaa wafanyakazi wanaofanya kazi kwa mazoea na ukiritimba wa hali ya juu.
 
Anaweza akawa performer. Lakini kwenye mazingira ya sasa ya taasisi za umma lazima uwasikilize waliokuweka pale wanataka nini kwanza. Kwa sifa hizi mnazommiminia pale hapamfai, kama ni mtu wa msimamo na maadili (na sio madili!) pale hatakaa.
 
Hili shirika la NHC lilianzishwa mwaka gani?
Aliyeiandika habari anasema lilianzishwa mara tu baada ya Tanganyika kupata uhuru.....

Mchechu hongera na tunakutakia mafanikio. Tunaamini utakuwa tayari kukabiliana na vikwazo utakwavyokutana navyo katika utendaji wako!
 
Huyu bwana nakumbuka mwishoni mwa miaka ya 90 wakati nafundisha pale mlimani aliwahi kuniomba nimuongezee marks kwenye coursework yake, ambayo kwa kweli ilikuwa chafu. Lakini nilimtolea nje kiustaarabu. Otherwise, he looks ambitious.
 
Back
Top Bottom