neema alimtendea haki chidumule?

minda

JF-Expert Member
Oct 2, 2009
1,068
65
13 desemba,2010.
usiku wa kuamkia leo tumepata habari za kusikitisha kuhusu kifo cha dk remmy ongala.
kwa kuwa chidumule ni mtu aliyepata kufanya kazi na dk ongala, nimeona bora niwarudishie wakuu, hii post mliyopata 'kuipotezea' miezi 5 iliyopita.


wakuu, wimbo neema wa cosmas chidumule umenifanya niwaze sana kama kuna haki katika kutendewa vile kwa chidumule (mwanaume yeyote).


hebu tuone scenario yenyewe:

neema ni mwanamke aliyezaa na mwanaume mwingine ila kwa sasa ana uhusiano wa kimapenzi na chidumule (mwanaume yeyote).


neema:
kwa sasa tusijuane. tukikutana njiani tuchuniane kwa sababu mzazi mwenzangu yupo...yani unikome kabisa usijenichafulia...



chidumule:
sina neno neema kwa kuwa najua huyo ni mzazi mwenzio. penzi maua; penzi upepo. ipo siku nitakuja kwenu na nitakutambulisha kwa wazazi...





je, neema anamtendea haki chidumule(mwanaume yeyote)?

je, hata (neema na chidumule) wakija kuoana, neema atakuwa na uaminifu kweli kwa ndoa yake au atatekeleza ile dhana ya mzazi mwenzio hatongozeki?
 
usiku wa kuamkia leo tarehe 13 desemba, 2010; tumepata habari za kusikitisha kuhusu kifo cha dk remmy ongala.
kwa kuwa chidumule ni mtu aliyepata kufanya kazi na dk ongala, nimeona bora niwarudishie wakuu, hii post mliyopata 'kuipotezea' miezi 5 iliyopita.
 
Back
Top Bottom