NECTA na mustakabali wa elimu-Tanzania

Brooklyn

JF-Expert Member
Mar 17, 2009
1,459
284
Ni wiki moja hivi imepita toka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) litangaze matokeo ya kidato cha sita. Tukio hilo uambatana na wahitimu hao kukimbizana huku na kule katika harakati za kuhakikisha wana meet deadline za ujazaji na urejeshwaji wa fomu za maombi ya mikopo toka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na maombi ya kujiunga na vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu ndani na nje ya nchi.

Mmoja kati ya wahitimu hao ni binamu yangu mwenye umri wa miaka 42 anayeishi na kufanya kazi mkoani Shinyanga. Baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 akaamua aongeze ujuzi na akajiunga na masomo ya kidato cha tano na sita. Baada ya mama Joyce Ndalichako (CEO-NECTA) kutangaza kutoka kwa matokeo hayo, huyu ndugu akakimbia kwenda kuangalia matokeo yake kwenye internet na kukuta ana Division Two point 10 (Hist C, Kisw D & Lang C). Jamaa akafurahi kupita kiasi na kunijulisha kuhusu matokeo hayo na kuniomba nimchukulie fomu za mikopo na fomu za kujiunga na vyuo walau vinne, huku akiahidi kuwa anajitahidi akopekope pesa kwa ndugu na marafiki ili apate nauli za kuja DSM kufuatilia Results slip na kulipia application fees za vyuo na bodi ya mikopo.

Mungu akamsaidia akapata kama Tzs. 250,000, na kuwasili DSM siku ya Jumatano ya tarehe 6/5/2009. Alhamisi akaitumia kwenda benki kulipia hizo fees kwa ajili ya kusubmit filled forms ili ameet hizo deadline. Ijumaa akaenda kufuatilia result slip yake na cha kushangaza akakuta matokeo tofauti kabisa ktk slip hiyo. Matokeo yaliyoandikwa ktk slip ni Division four ya mwisho kabisa. Jamaa presha imepanda, deni ndo hilo tena inabidi lilipwe kutoka kwenye kijimshahara kidogo cha ualimu wa shule ya msingi.

Sasa najiuliza hivi inakuwaje NECTA wafanye makosa kama haya ambayo yanaweza kuepukwa kabisa?? Kwenye makosa kama haya ni watanzania wangapi wanapewa matokeo ambayo si yao?? Kuhusu huu usumbufu na hasara wanayopata wahitimu na wazazi wao nani anawajibika?? Ni aina gani ya professionals tunaowatengeneza katika mazingira kama haya?? Kama baraza linashindwa na kumatch matokeo ya watahiniwa wake ambao hawazidi hata 60,000 je watawezaje kucontrol vyeti feki vilivyozagaa nchi nzima???

Wakuu nauliza haya ndio maisha bora kwa kila mdanganyika???
 
Hilo baraza la mitihani inabidi livunjwe,Dr Ndalichako hana jipya yeye anachojua kufukuza wafanyakazi na ameajiri watu Bogus kama Daniel Mafie(Director of Finance and Administration)na Kihanga (Human Resource Officer(sio raia wa tanzania ni mtusi) na wengine wengi ambao wameguza baraza la mitihani kama soko la kariakoo
 
Hilo baraza la mitihani inabidi livunjwe,Dr Ndalichako hana jipya yeye anachojua kufukuza wafanyakazi na ameajiri watu Bogus kama Daniel Mafie(Director of Finance and Administration)na Kihanga (Human Resource Officer(sio raia wa tanzania ni mtusi) na wengine wengi ambao wameguza baraza la mitihani kama soko la kariakoo
Nini ubogus wa DF? maana umeweka taarifa nusu hyo mwingine angalau umesema sio raia
 
Ni wiki moja hivi imepita toka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) litangaze matokeo ya kidato cha sita. Tukio hilo uambatana na wahitimu hao kukimbizana huku na kule katika harakati za kuhakikisha wana meet deadline za ujazaji na urejeshwaji wa fomu za maombi ya mikopo toka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na maombi ya kujiunga na vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu ndani na nje ya nchi.

Mmoja kati ya wahitimu hao ni binamu yangu mwenye umri wa miaka 42 anayeishi na kufanya kazi mkoani Shinyanga. Baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 akaamua aongeze ujuzi na akajiunga na masomo ya kidato cha tano na sita. Baada ya mama Joyce Ndalichako (CEO-NECTA) kutangaza kutoka kwa matokeo hayo, huyu ndugu akakimbia kwenda kuangalia matokeo yake kwenye internet na kukuta ana Division Two point 10 (Hist C, Kisw D & Lang C). Jamaa akafurahi kupita kiasi na kunijulisha kuhusu matokeo hayo na kuniomba nimchukulie fomu za mikopo na fomu za kujiunga na vyuo walau vinne, huku akiahidi kuwa anajitahidi akopekope pesa kwa ndugu na marafiki ili apate nauli za kuja DSM kufuatilia Results slip na kulipia application fees za vyuo na bodi ya mikopo.

Mungu akamsaidia akapata kama Tzs. 250,000, na kuwasili DSM siku ya Jumatano ya tarehe 6/5/2009. Alhamisi akaitumia kwenda benki kulipia hizo fees kwa ajili ya kusubmit filled forms ili ameet hizo deadline. Ijumaa akaenda kufuatilia result slip yake na cha kushangaza akakuta matokeo tofauti kabisa ktk slip hiyo. Matokeo yaliyoandikwa ktk slip ni Division four ya mwisho kabisa. Jamaa presha imepanda, deni ndo hilo tena inabidi lilipwe kutoka kwenye kijimshahara kidogo cha ualimu wa shule ya msingi.

Sasa najiuliza hivi inakuwaje NECTA wafanye makosa kama haya ambayo yanaweza kuepukwa kabisa?? Kwenye makosa kama haya ni watanzania wangapi wanapewa matokeo ambayo si yao?? Kuhusu huu usumbufu na hasara wanayopata wahitimu na wazazi wao nani anawajibika?? Ni aina gani ya professionals tunaowatengeneza katika mazingira kama haya?? Kama baraza linashindwa na kumatch matokeo ya watahiniwa wake ambao hawazidi hata 60,000 je watawezaje kucontrol vyeti feki vilivyozagaa nchi nzima???

Wakuu nauliza haya ndio maisha bora kwa kila mdanganyika???
kwa tatizo kama hili na sisi tuwe waangalifu kabla ya kutoa huku, namba yake ukiiangalia na Matoke yake kwenye internet ni sawa na ya kwenye slip? maana katika kiwehuwehu cha kuangalia matokeo kwenye internet unaweza angalia ya mtu mwingine na inapofika kwenye reality namba yako ni nyingine, maana kama nikweli kuna makosa kama hayo mwambie nuduguyo aprint ya kwenye internet na alinganishe na hayo wa kwenye slip
 
Back
Top Bottom