Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Ni wiki moja hivi imepita toka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) litangaze matokeo ya kidato cha sita. Tukio hilo uambatana na wahitimu hao kukimbizana huku na kule katika harakati za kuhakikisha wana meet deadline za ujazaji na urejeshwaji wa fomu za maombi ya mikopo toka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na maombi ya kujiunga na vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu ndani na nje ya nchi.
Mmoja kati ya wahitimu hao ni binamu yangu mwenye umri wa miaka 42 anayeishi na kufanya kazi mkoani Shinyanga. Baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 akaamua aongeze ujuzi na akajiunga na masomo ya kidato cha tano na sita. Baada ya mama Joyce Ndalichako (CEO-NECTA) kutangaza kutoka kwa matokeo hayo, huyu ndugu akakimbia kwenda kuangalia matokeo yake kwenye internet na kukuta ana Division Two point 10 (Hist C, Kisw D & Lang C). Jamaa akafurahi kupita kiasi na kunijulisha kuhusu matokeo hayo na kuniomba nimchukulie fomu za mikopo na fomu za kujiunga na vyuo walau vinne, huku akiahidi kuwa anajitahidi akopekope pesa kwa ndugu na marafiki ili apate nauli za kuja DSM kufuatilia Results slip na kulipia application fees za vyuo na bodi ya mikopo.
Mungu akamsaidia akapata kama Tzs. 250,000, na kuwasili DSM siku ya Jumatano ya tarehe 6/5/2009. Alhamisi akaitumia kwenda benki kulipia hizo fees kwa ajili ya kusubmit filled forms ili ameet hizo deadline. Ijumaa akaenda kufuatilia result slip yake na cha kushangaza akakuta matokeo tofauti kabisa ktk slip hiyo. Matokeo yaliyoandikwa ktk slip ni Division four ya mwisho kabisa. Jamaa presha imepanda, deni ndo hilo tena inabidi lilipwe kutoka kwenye kijimshahara kidogo cha ualimu wa shule ya msingi.
Sasa najiuliza hivi inakuwaje NECTA wafanye makosa kama haya ambayo yanaweza kuepukwa kabisa?? Kwenye makosa kama haya ni watanzania wangapi wanapewa matokeo ambayo si yao?? Kuhusu huu usumbufu na hasara wanayopata wahitimu na wazazi wao nani anawajibika?? Ni aina gani ya professionals tunaowatengeneza katika mazingira kama haya?? Kama baraza linashindwa na kumatch matokeo ya watahiniwa wake ambao hawazidi hata 60,000 je watawezaje kucontrol vyeti feki vilivyozagaa nchi nzima???
Wakuu nauliza haya ndio maisha bora kwa kila mdanganyika???
Mmoja kati ya wahitimu hao ni binamu yangu mwenye umri wa miaka 42 anayeishi na kufanya kazi mkoani Shinyanga. Baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 akaamua aongeze ujuzi na akajiunga na masomo ya kidato cha tano na sita. Baada ya mama Joyce Ndalichako (CEO-NECTA) kutangaza kutoka kwa matokeo hayo, huyu ndugu akakimbia kwenda kuangalia matokeo yake kwenye internet na kukuta ana Division Two point 10 (Hist C, Kisw D & Lang C). Jamaa akafurahi kupita kiasi na kunijulisha kuhusu matokeo hayo na kuniomba nimchukulie fomu za mikopo na fomu za kujiunga na vyuo walau vinne, huku akiahidi kuwa anajitahidi akopekope pesa kwa ndugu na marafiki ili apate nauli za kuja DSM kufuatilia Results slip na kulipia application fees za vyuo na bodi ya mikopo.
Mungu akamsaidia akapata kama Tzs. 250,000, na kuwasili DSM siku ya Jumatano ya tarehe 6/5/2009. Alhamisi akaitumia kwenda benki kulipia hizo fees kwa ajili ya kusubmit filled forms ili ameet hizo deadline. Ijumaa akaenda kufuatilia result slip yake na cha kushangaza akakuta matokeo tofauti kabisa ktk slip hiyo. Matokeo yaliyoandikwa ktk slip ni Division four ya mwisho kabisa. Jamaa presha imepanda, deni ndo hilo tena inabidi lilipwe kutoka kwenye kijimshahara kidogo cha ualimu wa shule ya msingi.
Sasa najiuliza hivi inakuwaje NECTA wafanye makosa kama haya ambayo yanaweza kuepukwa kabisa?? Kwenye makosa kama haya ni watanzania wangapi wanapewa matokeo ambayo si yao?? Kuhusu huu usumbufu na hasara wanayopata wahitimu na wazazi wao nani anawajibika?? Ni aina gani ya professionals tunaowatengeneza katika mazingira kama haya?? Kama baraza linashindwa na kumatch matokeo ya watahiniwa wake ambao hawazidi hata 60,000 je watawezaje kucontrol vyeti feki vilivyozagaa nchi nzima???
Wakuu nauliza haya ndio maisha bora kwa kila mdanganyika???