NECTA na matokeo batili ya mtihani somo la Islamic Knowledge!

Status
Not open for further replies.

MchukiaUonevu

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
207
79
Ndugu wadau,
Ripoti ya tume iliyochunguza tuhuma dhidi ya upotoshaji wa matokeo ya mtihani wa somo la Islamic knowledge kidato cha sita mwaka 2012 inasikitisha. Tarrifa zilizotolewa na Naibu Waziri wa Elimu Ndg.Phillipo Mulugo kuwa tume ilijiridhisha kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye mfumo wa computer inazua maswali mengi kuliko majibu. Matokeo ya uchunguzi huu yametoa taswira halisi ya Necta. Katika hali ya kawaida,makosa hufanywa na kila binadamu,lakini pia degree,frequency na mazingira ya kosa ni kitu kingine. Ni jambo ambalo haliingii akilini makosa yafanyike halafu chombo husika kikae kimya hadi watu waandamane ndio haki itolewe. Waislam wamelalamika miaka mingi sana juu ya baraza la mitihani kumezwa na mfumo unaowanyima haki wanafunzi wa kiislam na hata shule za kiislam. Lakini hawajawahi kupewa majibu zaidi ya kukejeliwa,kudharauliwa,na kuitwa majina mabaya. Leo serikali inakuja na majibu mepesi kuwa ni hitilafu ya computer,sijui formula iliyotumika kukokotoa nk. Haya sio majibu ya kutolewa na Waziri,kila mtu anafahamu computer hufanya kazi kutokana na instructions za binadamu. Huwezi kuingiza wrong formula halafu utegemee majibu sahihi,garbage in garbage out!. Tena cha kushangaza system imechagua somo la dini moja tu la "Islamic knowledge",somo lenye vigezo sawa na somo wanalofanya wanafunzi wa dini nyingine la "Divinity".

Hatuwezi kuridhika na majibu mepesi kiasi hiki kwa makosa ya kudhamiria kiasi hiki. Sensitive issues kama matokeo ya mitihani sio kitu cha kufanyia masihara. Hii kazi haifanywi na mtu mmoja,ni jopo la watu,tena wanaofanya kazi independently,na mwisho lazima matokeo yawe reviewed na watu makini. Iweje leo Waziri aseme ni kosa la Mkurugenzi mmoja. Hatuwezi kuridhika kwa kumfukuza kazi mtu mmoja,tunataka uozo uliopo Necta uondolewe,haki itendeke na tena haki ionekane kutendeka!

T
ujiulize maswali haya.
1:Utaratibu wa Necta ukoje kabla ya kuchapisha matokeo ya mtihani.
2:Ikiwa hii si mara ya kwanza kwa Waislam kulalamika juu ya mfumo kandamizi uliopo Necta,ni hatua gani zilishachukuliwa ku-address uozo huo.
3:Kwa nini watu walewale waliolalamika miaka mingi juu ya mfumo kandamizi wamekuwa proved victims wa mfumo tajwa.
4:Kama wamekiri somo moja tu kuathirika na "hitilafu kwenye mfumo wa computer",tena somo ambalo hufanywa na wanafunzi wa dini moja tu,is there any validity of the results for the rest of the subjects?


Kwa majibu ya Ndg.Mulugo,matokeo ya kidato cha sita yanakosa uhalali wa kuitwa matokeo,na hasa kwa wanafunzi wa Kiislam(huu ni mtazamo wangu).Kuchapisha upya matokeo ya somo moja la Islamic Knowledge hakuniondolei hofu juu ya madhila wanayofanyiwa Waislam na shule za kiislam na baraza la mitihani. Hatuwezi kuamini kirahisi kuwa makosa yalifanyika kwenye somo moja tu,na hasa ikizingatiwa nature ya kosa lenyewe limekuwa "too selective".Tunatakiwa tujiridhishe beyond reasonable doubt kuhusu muundo wa Necta,ufanyaji kazi wake,watumishi wake,usahishaji mitihani,na uchapishaji wa matokeo ya mitihani.
Nawasilisha!
 
Hivi mpaka muambiwe kwa namna gani ndiyo muelewe? Mmeambiwa kwamba, awali somo la Islamic Knowledge lilikuwa na mitihani mitatu, hivyo program ya kukokotoa wastan ilikuwakuwa inagawanya kwa tatu...Lakini kuanzia mwaka jana, somo hilo lina mitihani miwili tu...sasa kilichotokea ni kosa la kitaalam yaani: hawakubadilisha ile program ya kukokotoa wastani wa mitihani mitatu kitu kilichopelekea hata huu mtihani huu wa islamic knowledge ambao una mitihani miwili kukokotolewa wastani wake kama vile kuna mitihani mitatu. Kwanini mnahangaika na kitu kilichotolewa maelezo ya kujitosheleza mara elfu?
 
Ndugu wadau,
Ripoti ya tume iliyochunguza tuhuma dhidi ya upotoshaji wa matokeo ya mtihani wa somo la Islamic knowledge kidato cha sita mwaka 2012 inasikitisha. Tarrifa zilizotolewa na Naibu Waziri wa Elimu Ndg.Phillipo Mulugo kuwa tume ilijiridhisha kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye mfumo wa computer inazua maswali mengi kuliko majibu. Matokeo ya uchunguzi huu yametoa taswira halisi ya Necta. Katika hali ya kawaida,makosa hufanywa na kila binadamu,lakini pia degree,frequency na mazingira ya kosa ni kitu kingine. Ni jambo ambalo haliingii akilini makosa yafanyike halafu chombo husika kikae kimya hadi watu waandamane ndio haki itolewe. Waislam wamelalamika miaka mingi sana juu ya baraza la mitihani kumezwa na mfumo unaowanyima haki wanafunzi wa kiislam na hata shule za kiislam. Lakini hawajawahi kupewa majibu zaidi ya kukejeliwa,kudharauliwa,na kuitwa majina mabaya. Leo serikali inakuja na majibu mepesi kuwa ni hitilafu ya computer,sijui formula iliyotumika kukokotoa nk. Haya sio majibu ya kutolewa na Waziri,kila mtu anafahamu computer hufanya kazi kutokana na instructions za binadamu. Huwezi kuingiza wrong formula halafu utegemee majibu sahihi,garbage in garbage out!. Tena cha kushangaza system imechagua somo la dini moja tu la "Islamic knowledge",somo lenye vigezo sawa na somo wanalofanya wanafunzi wa dini nyingine la "Divinity".

Hatuwezi kuridhika na majibu mepesi kiasi hiki kwa makosa ya kudhamiria kiasi hiki. Sensitive issues kama matokeo ya mitihani sio kitu cha kufanyia masihara. Hii kazi haifanywi na mtu mmoja,ni jopo la watu,tena wanaofanya kazi independently,na mwisho lazima matokeo yawe reviewed na watu makini. Iweje leo Waziri aseme ni kosa la Mkurugenzi mmoja. Hatuwezi kuridhika kwa kumfukuza kazi mtu mmoja,tunataka uozo uliopo Necta uondolewe,haki itendeke na tena haki ionekane kutendeka!

T
ujiulize maswali haya.
1:Utaratibu wa Necta ukoje kabla ya kuchapisha matokeo ya mtihani.
2:Ikiwa hii si mara ya kwanza kwa Waislam kulalamika juu ya mfumo kandamizi uliopo Necta,ni hatua gani zilishachukuliwa ku-address uozo huo.
3:Kwa nini watu walewale waliolalamika miaka mingi juu ya mfumo kandamizi wamekuwa proved victims wa mfumo tajwa.
4:Kama wamekiri somo moja tu kuathirika na "hitilafu kwenye mfumo wa computer",tena somo ambalo hufanywa na wanafunzi wa dini moja tu,is there any validity of the results for the rest of the subjects?


Kwa majibu ya Ndg.Mulugo,matokeo ya kidato cha sita yanakosa uhalali wa kuitwa matokeo,na hasa kwa wanafunzi wa Kiislam(huu ni mtazamo wangu).Kuchapisha upya matokeo ya somo moja la Islamic Knowledge hakuniondolei hofu juu ya madhila wanayofanyiwa Waislam na shule za kiislam na baraza la mitihani. Hatuwezi kuamini kirahisi kuwa makosa yalifanyika kwenye somo moja tu,na hasa ikizingatiwa nature ya kosa lenyewe limekuwa "too selective".Tunatakiwa tujiridhishe beyond reasonable doubt kuhusu muundo wa Necta,ufanyaji kazi wake,watumishi wake,usahishaji mitihani,na uchapishaji wa matokeo ya mitihani.
Nawasilisha!
Tumewazoea.Mmmezoea sana kulalamika mnaonewa mnaonewa mmekuwa kama watoto wadogo hata watoto wadogo hawako hivyo.Ndio maana waarabu hadi leo wameshindwa kuwa na umoja na matokeo yake nchi za magharibi zinawaburuza wanavyotaka.Mlianza na na Raisi wa Iraq mkaja kwa Gadafi matokeo au faida yake iko wapi.Hakuna mtu asiyefanya makosa hapa duniani na kufanya kosa si kosa ila linakuwa kosa ukirudia tena hilo kosa.
 
Hivi mpaka muambiwe kwa namna gani ndiyo muelewe? Mmeambiwa kwamba, awali somo la Islamic Knowledge lilikuwa na mitihani mitatu, hivyo program ya kukokotoa wastan ilikuwakuwa inagawanya kwa tatu...Lakini kuanzia mwaka jana, somo hilo lina mitihani miwili tu...sasa kilichotokea ni kosa la kitaalam yaani: hawakubadilisha ile program ya kukokotoa wastani wa mitihani mitatu kitu kilichopelekea hata huu mtihani huu wa islamic knowledge ambao una mitihani miwili kukokotolewa wastani wake kama vile kuna mitihani mitatu. Kwanini mnahangaika na kitu kilichotolewa maelezo ya kujitosheleza mara elfu?

we unadhani wao wajinga kutogundua hilo kabla
 
Yani mshajengeka kwamba mnachakachuliwa kila kitu, hqwa watu ni wagumu kuelewe!!!
 
Hivi mpaka muambiwe kwa namna gani ndiyo muelewe? Mmeambiwa kwamba, awali somo la Islamic Knowledge lilikuwa na mitihani mitatu, hivyo program ya kukokotoa wastan ilikuwakuwa inagawanya kwa tatu...Lakini kuanzia mwaka jana, somo hilo lina mitihani miwili tu...sasa kilichotokea ni kosa la kitaalam yaani: hawakubadilisha ile program ya kukokotoa wastani wa mitihani mitatu kitu kilichopelekea hata huu mtihani huu wa islamic knowledge ambao una mitihani miwili kukokotolewa wastani wake kama vile kuna mitihani mitatu. Kwanini mnahangaika na kitu kilichotolewa maelezo ya kujitosheleza mara elfu?
Hili linaeleweka. Ukitizama kwa makini tatizo hili unaona kuwa hakuna "effective controls". Kukosekana huko kwa effective controls kunafanya mtu ajiulize, je kuna makosa mangapi ya namna hiyo yanatokea au yatatokea tena? Maana masomo na hata namba ya hizo papers potentially ni vitu vinavyobadilika achilia mbali mifumo yenyewe ya computer! Vipi kuhusu usahihishaji......controls zipo effective kwa kiasi gani? Zinaweza kuzuia makosa (ya 'kibinaadamu'!) kwa kiasi gani?
 
Hebu tuwe objective kidogo wajameni. Hivi haya malalamiko yote ambayo yanatolewa na hawa ndugu zetu, ni kwamba hayana mantiki? Mtu anaamua tu kulalama out of the blu? Ilitokea kidato cha 4, sasa cha 6 kwa somo hili moja. Hamuoni kuwa kuna tatizo. Is it possible kwamba average ya masomo mawili igawanywe mara tatu, na mhusika asigundue hilo. Vipi pale wanapofanya review kabla ya kutangaza rasmi matokeo? Hawafanyi tathmini na kubaini kwanini wanafunzi wamefaulu sana au kufeli sana somo fulani. Mtu akilia kuwa anaonewa, hebu msikilize kwanza kama hoja za msingi zipo. Kama hazipo, potelea pote. Ila ni dhahiri kuwa kuna tatizo linalowahusu Waislamu na jamii (dunia) inafumba macho na kuziba masikio. For what reasons, God knows.
 
Hivi mpaka muambiwe kwa namna gani ndiyo muelewe? Mmeambiwa kwamba, awali somo la Islamic Knowledge lilikuwa na mitihani mitatu, hivyo program ya kukokotoa wastan ilikuwakuwa inagawanya kwa tatu...Lakini kuanzia mwaka jana, somo hilo lina mitihani miwili tu...sasa kilichotokea ni kosa la kitaalam yaani: hawakubadilisha ile program ya kukokotoa wastani wa mitihani mitatu kitu kilichopelekea hata huu mtihani huu wa islamic knowledge ambao una mitihani miwili kukokotolewa wastani wake kama vile kuna mitihani mitatu. Kwanini mnahangaika na kitu kilichotolewa maelezo ya kujitosheleza mara elfu?

Hata mwanzoni Waislam walipolalamika kuwa wamefelishwa,na kujiaminisha zaidi kutokana na matokeo mabaya ya somo la Islamic Knowledge majibu yalikua mepesi kama yako. Walidiriki hata kuwajibu Waislam mtihani wa Islamic Knowledge husahihishwa na Walimu wa Kiislam hivyo haiwezekani wakafelishwa,but now they have been proved wrong! Sasa na wewe unakuja na majibu yaleyale yenye mwelekeo uleule.

Hii formula haikutolewa siku ya kuchapisha matokeo,au siku ya ku-compile matokeo. Kulikuwa na maandalizi ya kutosha kabla na baada ya kusahihisha mitihani.Tena nakukumbusha,hakuna kazi au ripoti makini isiyokuwa na "check". Ina maana Waislam wasingelalamika nchi nzima ilikuwa imedanganywa.! Jaribu kuwa mwepesi wa kuelewa kama unaweza mkuu!
 
Hebu tuwe objective kidogo wajameni. Hivi haya malalamiko yote ambayo yanatolewa na hawa ndugu zetu, ni kwamba hayana mantiki? Mtu anaamua tu kulalama out of the blu? Ilitokea kidato cha 4, sasa cha 6 kwa somo hili moja. Hamuoni kuwa kuna tatizo. Is it possible kwamba average ya masomo mawili igawanywe mara tatu, na mhusika asigundue hilo. Vipi pale wanapofanya review kabla ya kutangaza rasmi matokeo? Hawafanyi tathmini na kubaini kwanini wanafunzi wamefaulu sana au kufeli sana somo fulani. Mtu akilia kuwa anaonewa, hebu msikilize kwanza kama hoja za msingi zipo. Kama hazipo, potelea pote. Ila ni dhahiri kuwa kuna tatizo linalowahusu Waislamu na jamii (dunia) inafumba macho na kuziba masikio. For what reasons, God knows.

shukran sana mkuu, we ndo umeongea kwa busara, wengine wanaropokwa na kukejeli.
Huo ndo ukweli, linapokuja suala linalo husu waislam kila mmoja analifumbia macho na kuwalaumu waislamu kuwa wamezidi kulalamika.
Hii dhulma tunayofanyiwa mwishowake wala hauko mbali na itakuwa na madhara makubwa kwa jamii yote.

Tuache unafiki wa kufumbia macho mambo kamahaya, penye ukweli uongo hujitenga.

Koment za kejeli zinayotolewa na baadhi ya wanajamvi zinadhihirisha yalojificha ktk mioyo yao.
 
mkuu MchukiaUonevu, tatizo watu wamezoea kuwakandamiza waislamu na kuwadhulumu.
Wanapaswa wakumbuke waislamu wa sasa sio wale wa mwaka 60, wanajhtambua zaidi na wanajua wanachofanya.
Mwisho wa mambo kama haya ni mbaya sana na utaleta madhara kwa taifa letu.
 
Hivi mpaka muambiwe kwa namna gani ndiyo muelewe? Mmeambiwa kwamba, awali somo la Islamic Knowledge lilikuwa na mitihani mitatu, hivyo program ya kukokotoa wastan ilikuwakuwa inagawanya kwa tatu...Lakini kuanzia mwaka jana, somo hilo lina mitihani miwili tu...sasa kilichotokea ni kosa la kitaalam yaani: hawakubadilisha ile program ya kukokotoa wastani wa mitihani mitatu kitu kilichopelekea hata huu mtihani huu wa islamic knowledge ambao una mitihani miwili kukokotolewa wastani wake kama vile kuna mitihani mitatu. Kwanini mnahangaika na kitu kilichotolewa maelezo ya kujitosheleza mara elfu?

Huo wote uliouongea "collectively" unaitwa neno la kiswahili "U Z E M B E " na mtu akiwa mzembe lazima awajibike! na si kitu cha ajabu! wamewajibika wengi hasa upande wa wenzetu kule visiwani kwa kuwa wale waungwana, huku kwetu bara mtu mpaka AWAJIBISHWE!
 
Huo wote uliouongea "collectively" unaitwa neno la kiswahili "U Z E M B E " na mtu akiwa mzembe lazima awajibike! na si kitu cha ajabu! wamewajibika wengi hasa upande wa wenzetu kule visiwani kwa kuwa wale waungwana, huku kwetu bara mtu mpaka AWAJIBISHWE!
Muhusika mkuu kwenye hicho kitengo cha ukokotoaji ameshawajibishwa...unataka nani mwingine aondoke/asimamishwe kazi? Shukuru Kawambwa , Mlugo au Ndalichako???
 
Basi fanyeni mnachotaka. Mnatukera mnavyotuletea hapa malalamiko yenu. Mkishauriwa mnakuwa wabishi...fanyeni mnachotaka...yameshatokea!

Tuyapeleke wapi zaidi ya hapa ?

logo_m.jpg


WHERE WE DARE TO TALK OPENLY....twende wapi? au hii forum ya kwenu peke yenu? tujuze basi!
 
Muhusika mkuu kwenye hicho kitengo cha ukokotoaji ameshawajibwa...unataka nani mwingine aondoke? Shukuru Kawambwa , Mlugo au Ndalichako???

Ndalichako ! kwa sababu huyu amefanya makusudi ili shukuru kawamba aonekane mzembe! wewe hukumsikia Rais wetu mpenzi Dkt Jakaya Kikwete akisema kuna wakurugenzi na watendaji serikalini wanafanya hila ili wakuu yaani mawaziri waondoshwe?! mimi naamini maneno haya ya Muheshimiwa Rais, huyu Mama lazima aondoke !
 
Hakuna kitu kama hicho. KIKULACHO KIMO NGUONI MWAKO...Tafakari

kivipi mkuu, kwani necta nao ni waislamu?
Polisi walowakamata waislamu na kuwanyima dhamana nao vp?
Mauji ya mwembe chai na znz nayo vp?
Kwakifupi hakuna muislamu wa kweli anae dhulumu au kuonea kwani ni kinyume na msingi wa uislamu.
Au fafanua mkuu, labda mi sijakuelewa.
 
Sep 14th, 2012

Tanzania |


The Head of Research, Evaluation and Computer Services at the National Examination Council of Tanzania (NECTA), Mr Joseph Mbowe, will face administrative action following a blunder in the marking of the Islamic Knowledge subject in the Form Six National Examinations this year.


Addressing journalists , the Deputy Minister for Education and Vocational Training, Mr Philip Mulugo, said that a probe team has established that the technical fault stemmed from a computerized system."In the past few years, the students taking the subject would attempt three papers and the tallying system was set for three papers.

However, this year the papers were reduced to two, and the system was not apparently reset to reflect two papers hence the poor results," Mr Mulugo explained.He said that the Department of Research, Evaluation and Computer Services should have made initial trials to ensure the computerized system was set to work for only two papers, hence the need to take appropriate action against the culprit.


A probe committee formed by the Ministry of Education and Vocational Training to look into the problem found out that it was not a human but technical fault that resulted in the poor performance in the subject.Mr Mulugo said that NECTA has already corrected the mistake and that all the students who sat for the Islamic Knowledge subject have received their new results.


"Immediately after we realized that problem, the Council was directed to compute the results afresh and the students have already received the results," he explained.The minister called upon the all stakeholders including heads of schools whose students sat for the exam and communities to accept the probe team's finding - that it was a technical fault and not a malicious move.


He said that the ministry will work on recommendations made by the probe team including conducting frequent assessments of the computerized system to ensure they function properly.The deputy minister noted that the probe committee was cross-cutting comprising members from the University of
Dar es Salaam, the Ministry of Education and Vocational Training (Mainland and Zanzibar) Islamic Education Panel and the Head of Islamic Schools Council.


Early last June, scores of Muslims gathered at Kidongo Chekundu grounds near Mnazi Mmoja in the city to call upon the government to compel NECTA administration to take responsibility, including the Executive Secretary, Dr Joyce Ndalichako, for the blunder.Meanwhile,
Tanzania Islamic Peace Foundation (TIPF) has warned Muslims countrywide to shun religious organizations that threaten peace and tranquility.


The TIPF's Director, Mr Sadiki Godigodi, made the remarks in
Dar es Salaam yesterday in relation to a demonstration expected to be held today by an Islamic organization led by Sheikh Issa Ponda to call for disbanding of the National Examination Council of Tanzania.Mr Godigodi said that there was no need to blame the examination board over a problem that has already been solved.


In another development, the
Tanzania Teachers' Union (TTU) has called for formation of a team to discuss teachers' grievances besides the discussions at the Commission of Mediation and Arbitration (CMA).


The TTU President, Gratian Mukoba, told a news conference in
Dar es Salaam that formation of the team, like that formed by Prime Minister Mizengo Pinda to discuss grievances of medical doctors, would provide solutions to some issues which need to be implemented during the current financial year."We are optimistic that the team could complete its work within two weeks and its resolution will be registered with CMA," Mr Mukoba said.


By ROSE ATHUMANI, Tanzania Daily News


 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom