Elections 2010 NEC yabariki kampeni za CHADEMA Maswa kusitishwa

Mafuchila

JF-Expert Member
Apr 29, 2006
751
65
NEC yabariki kampeni za Chadema Maswa kusitishwa

Na Joseph Mwendapole
30th October 2010


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imebariki uamuzi wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi ya Jimbo la Maswa Magharibi mkoani Shinyanga ya kusimamisha kampeni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Mkurugenzi wa Nec, Rajab Kiravu, alisema jana kuwa NEC ilipitia kwa makini uamuzi uliochukuliwa na kamati hiyo na imeridhika kuwa hatua iliyochukuliwa ni sahihi.

"Kamati ya Maadili ya kitaifa imeridhika na hatua iliyochukuliwa baada ya kupitia kwa makini mwenendo wa shauri lile hivyo NEC imekubali chama hicho kisifanye kampeni zozote ndani ya jimbo lile," alisema.

Vile vile, Kiravu alisema Nec imepokea rasmi malalamiko ya CCM dhidi ya Chadema kutokana na mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Temeke, Dickson Amos, kumkashifu mgombea wa urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, wakati wa mkutano wa kampeni Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.

Kiravu alisema ingawa siku zimekwisha NEC itajadili malalamiko hayo ya CCM kwa kina na kisha itatoa majibu kwa chama hicho.

Akizungumzia matokeo ya urais, Kiravu alisema yatakuwa yakitangazwa kwa umma kadri yatakavyokuwa yakiletwa kutoka majimboni na baada ya majimbo yote kuwasilisha matokeo yatajumlishwa na kutangazwa.

CHANZO:
NIPASHE
 
well, mwisho wa kampeni ni leo, it makes no difference!!!
muamuzi wa mwisho ni mwananchi wa jimbo hilo.
 
Sijui Hawa NEC, yaani Lewis Makame na Rajabu Kiravu, wataaminikaje na wananchi kwamba watatendea haki kura zetu tutakazowapia Slaa. wagombea Ubunge wa Chadema na madiwani wao. Obviously biased against Chadema.
 
Hebu badilisha title ya Thread ieleweke ni MASWA pekee. Please MODS do the needful. Heading ya post hii inapotosha
 
Back
Top Bottom