NEC: Hatujapata taarifa za Kafumu kuvuliwa ubunge

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imesema bado haijapata taarifa rasmi za hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora iliyomng'oa ubunge wa Igunga, Dk Dallaly Peter Kafumu.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Nec, Julius Mallaba alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii.

"Hatuwezi kutangaza kuwa jimbo la Igunga liko wazi hadi hapo tutakapopata nakala ya hukumu hiyo, tumezisikia habari za kutenguliwa ubunge wa mbunge huyo kupitia vyombo vya habari," alisema Mallaba.

Alisema tume inaweza kulitangaza jimbo hilo kuwa wazi baada ya kuipata hukumu hiyo.
Hata hivyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Igunga, kimesema kimeanza kuipitia kwa umakini hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora ili kubaini upungufu uliopo.

Chama hicho ambacho Dk Kafumu alikuwa ni mbunge wake, kimesema kikibainisha upungufu uliomo kwenye hukumu hiyo, kitakata rufaa.

Katibu wa CCM wa Wilaya ya Igunga, Mary Maziku alisema wanawatumia wanasheria wao kuipitia hukumu hiyo.
"Tuna uhakika kwamba tutakata rufaa hivi karibuni baada ya wanasheria wetu kumaliza kuipitia hukumu hii kwa sababu tunataka kuwa na uhakika na uamuzi tutakaouchukua," alisema Maziku aliyekuwa akizungumza kwa njia ya simu.
Maziku alisema, "tukimaliza kuipitia hukumu hii na siku ya kukata rufaa tutawajulisha lakini haitachukua muda mrefu kuanzia sasa."

Kauli hiyo imekuja baada ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nauye kutangaza uamuzi wa chama hicho kukata rufaa kwa sababu ya kutoridhishwa na hukumu iliyotolewa na Jaji wa Mahakama hiyo, Mary Shangali.

Nape alisema chama kimeitafakari hukumu ya kesi hiyo na kujiridhisha kuchukua uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya hukumu ya kesi hiyo.

Hata hivyo jana, Nape alipoulizwa kuhusu maendeleo ya kusudio la kukata rufaa alisema, "bado nawasiliana na wanasheria wa chama, kwa sasa sina taarifa za kukueleza."
Hivi karibuni Jaji Shangali alitoa hukumu iliyotengua ushindi wa Dk Kafumu baada ya kuridhishwa na madai saba kati ya 17 yaliyowasilishwa katika mahakama hiyo na mlalamikaji aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema, Joseph Kashindye.

Dk Kafumu wa CCM alitangazwa kushinda kiti na msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Igunga katika uchaguzi mdogo uliofanyika Septemba mwaka jana baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Rostam Aziz.
 
Inamaana NEC hawasikilizi redio wala kusoma magazeti?
Anyway watapata tuu taarifa rasmi.
 
Ysaani nchi hii imeoza sana. Sasa hawana taarifa maana yake nini?
 
Makosa yoote yaliyomtoa kafumu yalifanywa na chama na siyo kafumu. Ngoja wamkatie rufaa, inaonekana jamaa anapelekwa kama roboti hata hajielewi.
 
Kwa mwenendo huu hakuna haja ya kuwa doctor (Hivi ni 'Ph. D holder au ni Doctor wa namna gani!)
 
Hawa jamaa mbona hawaeleki, wanasema hawajaridhika na uamuzi watakata rufaa, huku wanadai wanasubiri wanasheria wao, which is which?
 
Tanzania tuna tatizo kubwa sana la watu/taasisi kukaa na kusubiri kila kitu kiletwe kwenye sahani. Tumeona polisi inavyotaka 'muathirika' awe ndio mpelelezi badala ya wao kufanya kazi hiyo, sasa NEC nayo inasubiri iletewe kila kitu. Kama hao wakubwa wamesikia taarifa inayohusu ofisi yao kwenye vyombo vya habari, wameshindwa kitu gani kuwasiliana (kwa barua) na ofisi husika ili wapate barua 'maalum?
 
Watakata rufaa lakinu yawezekana kwamba wanataka tuu kupunguza facts zilizowadondosha lakini hawawezi kushinda hata chembe
 
Nimeongeza wasiwasi wangu wa kutoiamini TUME ya UCHAGUZI (NEC) kama ni kwa ajili ya maslahi ya Taifa. Nashangaa wanavyosema hawana taarifa za mahakama juu ya utenguzi wa ushindi wa Dr. Kafumu wakati washatkiwa wengine katika kesi ile walikuwa ni Mwanasheria mkuu wa Serikali na msaidizi wa uchaguzi huo (Protace Magavane). Ninamashaka kunakitu kinatengenezwa nyuma ya pazia ili kuleta mizengwe katika hukumu hii.
 
Inamaana NEC hawasikilizi redio wala kusoma magazeti?
Anyway watapata tuu taarifa rasmi.

Huwa mnakurupuka bila kusoma? hiki nini?, nimekitoa hapo post #, ngoja nikukuzie labda una matatizo ya kuona:

"Hatuwezi kutangaza kuwa jimbo la Igunga liko wazi hadi hapo tutakapopata nakala ya hukumu hiyo, tumezisikia habari za kutenguliwa ubunge wa mbunge huyo kupitia vyombo vya habari," alisema Mallaba.
 
Usiwatukane Mkuu. Kiutaratibu ni lazima wataarifiwe rasmi na siyo kusikiliza redio na kusoma magazeti.

Nape alipokuwa analiongelea kwa nia ya kukata rufaa alishapewa nakala ya kushindwa sio?
Hatuwezi kuuheshimu utaratibu unaopingana na comon sense.

Barua rasmi, matokeo rasmi, kauli rasmi huku muda unasonga!
Iko siku mtashtukia tumefoleni tunataka kuingia bungeni kushiriki maamuzi ya jimbo letu bungeni. Manake hii sheria kipofu haiwezi kuona athari za kutokuwakilishwa bungeni. Sheria inaonekana kuogopa mtu na kupuuza watu.
 
NEC haraka ya nn

hatuwezi kuvumilia kutokuwakilishwa na muwakilishi halali,

na bado wanaendelea kuonyesha wanavyotudharau! Kimsingi hawataki, na sheria kukaa kimya, tuwe na mwakilishi wetu.
 
Huwa mnakurupuka bila kusoma? hiki nini?, nimekitoa hapo post #, ngoja nikukuzie labda una matatizo ya kuona:

“Hatuwezi kutangaza kuwa jimbo la Igunga liko wazi hadi hapo tutakapopata nakala ya hukumu hiyo, tumezisikia habari za kutenguliwa ubunge wa mbunge huyo kupitia vyombo vya habari,” alisema Mallaba.

wameiomba nakala hiyo kama utaratibu wa mahakama unavyoelekeza?
Ameonyesha nakala ya barua ya kuomba nakala ya hukumu!
 
wameiomba nakala hiyo kama utaratibu wa mahakama unavyoelekeza?
Ameonyesha nakala ya barua ya kuomba nakala ya hukumu!

Kwanini wao waiombe? kwa kusikia magazetini? funguka kidogo!
 
Kwanini wao waiombe? kwa kusikia magazetini? funguka kidogo!

Kama ni kweli "justice delayed is justice denied" hoja yangu inazidi kuwa kweli,

"tactic delay"
hakimu/jaji anaposoma hukumu, hiyo hukumu inamlenga mtuhumiwa, na habari hiyo humuhusu yeyote atakayehusika.
 
Hivi katika hili ni nani anayeiomba nakala ya hukumu? Chukulia ccm hawana mpango wa kukata rufaa, so hawana kazi na hiyo nakala ya hukumu hivyo wasiiombe Mahakama. Na Chadema ambao ni interested part ktk kesi wao wakaiomba na kupewa, then wakaiwasilisha kwenye Tume ya Uchaguzi. Je, Tume itaipokea na kuifanyia kazi nakala ya hukumu kutoka mikononi mwa Chadema? Kama sivyo, then wao Tume wataletewa na nani hiyo hukumu bila kuiomba? Tujadili kisomi zaidi.
 
Back
Top Bottom