nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Tuesday, September 15, 2011, 13:28
Rai-Makala
KIKAO cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakachofanyika mjini Dodoma Novemba 21 na 22, mwaka huu kinatarajia kutoa majibu juu ya masuala mbali mbali ambayo yamechangia vurugu, kurushiana maneno makali na kuhujumiana ndani ya chama hicho .
Kikao hicho kitakachofanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, pamoja na mambo mengine kitapokea taarifa ya hali ya kisiasa itakayosomwa na Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje na Siasa, January Makamba.
Tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 CCM haijatulia. Makundi ambayo Mwenyekiti Rais Kikwete aliomba yavunjwe, ndio kwanza yameongeza mpasuko. Hivi sasa kuna mpasuko wa kundi la Wanamtandao, mpasuko uliosababishwa na kura za maoni katika uchaguzi wa 2010.
Lakini hoja kubwa zaidi ambayo NEC ya CCM lazima itoe jibu ni hili la kuhujumiana. Sio siri tena kwamba kuna watu ambao wamepania kwamba lazima wamrithi Rais Kikwete 2015 na ndicho chanzo kikuu cha chokochoko.
Mambo mengine yatakayowekwa mezani ni pamoja na uchaguzi mdogo wa Igunga, uchaguzi ambao wachambuzi wanasema umeonyesha dhahiri kwamba CCM hamkani si shwari tena kwakuwa ilipata ushindi mwembamba licha ya kutumia nguvu kubwa na fedha nyingi.
Pia anatarajiwa kuzungumzia siasa za CCM na CHADEMA mkoani Arusha, siasa ambazo kwa kiasi kikubwa zimevuruga hali ya amani na utulivu katika mji huo wa kitalii nchini.
Mkutano huo muhimu unafanyika baada ya wenyeviti na makatibu wa mikoa wa CCM kuitwa Dar es Salaam wiki iliyopita, ambapo pamoja na mambo mengine walipendekeza viongozi wawili wa chama hicho Samuel Sitta na Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wachukuliwe hatua kwa kukihujumu chama hicho kwa makusudi.
Viongozi hao wanatuhumiwa kutoa kauli na misimamo ambayo ni yao binafsi, lakini wamekuwa wakiwahadaa Watanzania kuwa ni msimamo wa CCM, na kwamba ina baraka za chama.
Dhana ya kujivua gamba ambayo iliasisiwa na Rais Kikwete mjini Dodoma Februari 5, mwaka huu, pia inatarajiwa kutawala sehemu kubwa ya mjadala huo, hasa baada ya kupotoshwa na Nape na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati, mjini Dodoma walipozungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kikao cha NEC mwezi Februari.
Vyanzo vya habari ndani ya CCM vimesema kuwa, lengo la dhana hiyo kukipa sura mpya chama hicho, ili kiendane na wakati pamoja na kukidhi mahitaji ya wapiga kura ambao wengi ni vijana.
Lakini baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho wanatuhumiwa kubadili mantiki na dhana nzima ya kujivua gamba, kwa kuanza kuwaandama watesi wao wa kisiasa, kiasi cha kupendekeza wafukuzwe kwenye uanachama.
Kutokana na upotoshwaji huo, siasa za makundi ambazo kwa kiasi kikubwa zimekidhoofisha chama hicho, sasa zimeshika kasi na kuibua makundi mawili, wale wanaojiita wasafi na wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Katika kikao hicho, pia mgogoro uliopo ndani ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) unatarajiwa kujadiliwa, lengo likiwa kurejesha hali ya amani utulivu ndani ya chombo hicho muhimu kwa uhai wa chama hicho.
Hali mbaya ya uchumi, kuporomoka kwa thamani ya shilingi, kupanda kwa bei za vyakula, tatizo sugu la ajira miongoni mwa vijana, ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kujadiliwa.
Rai-Makala
- Kutoka wamoja au maneno ya Nyerere kutimia
- Taarifa ya hali ya siasa nchini kuwasilishwa
- Gamba, makundi, Igunga kujadiliwa
KIKAO cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakachofanyika mjini Dodoma Novemba 21 na 22, mwaka huu kinatarajia kutoa majibu juu ya masuala mbali mbali ambayo yamechangia vurugu, kurushiana maneno makali na kuhujumiana ndani ya chama hicho .
Kikao hicho kitakachofanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, pamoja na mambo mengine kitapokea taarifa ya hali ya kisiasa itakayosomwa na Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje na Siasa, January Makamba.
Tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 CCM haijatulia. Makundi ambayo Mwenyekiti Rais Kikwete aliomba yavunjwe, ndio kwanza yameongeza mpasuko. Hivi sasa kuna mpasuko wa kundi la Wanamtandao, mpasuko uliosababishwa na kura za maoni katika uchaguzi wa 2010.
Lakini hoja kubwa zaidi ambayo NEC ya CCM lazima itoe jibu ni hili la kuhujumiana. Sio siri tena kwamba kuna watu ambao wamepania kwamba lazima wamrithi Rais Kikwete 2015 na ndicho chanzo kikuu cha chokochoko.
Mambo mengine yatakayowekwa mezani ni pamoja na uchaguzi mdogo wa Igunga, uchaguzi ambao wachambuzi wanasema umeonyesha dhahiri kwamba CCM hamkani si shwari tena kwakuwa ilipata ushindi mwembamba licha ya kutumia nguvu kubwa na fedha nyingi.
Pia anatarajiwa kuzungumzia siasa za CCM na CHADEMA mkoani Arusha, siasa ambazo kwa kiasi kikubwa zimevuruga hali ya amani na utulivu katika mji huo wa kitalii nchini.
Mkutano huo muhimu unafanyika baada ya wenyeviti na makatibu wa mikoa wa CCM kuitwa Dar es Salaam wiki iliyopita, ambapo pamoja na mambo mengine walipendekeza viongozi wawili wa chama hicho Samuel Sitta na Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wachukuliwe hatua kwa kukihujumu chama hicho kwa makusudi.
Viongozi hao wanatuhumiwa kutoa kauli na misimamo ambayo ni yao binafsi, lakini wamekuwa wakiwahadaa Watanzania kuwa ni msimamo wa CCM, na kwamba ina baraka za chama.
Dhana ya kujivua gamba ambayo iliasisiwa na Rais Kikwete mjini Dodoma Februari 5, mwaka huu, pia inatarajiwa kutawala sehemu kubwa ya mjadala huo, hasa baada ya kupotoshwa na Nape na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati, mjini Dodoma walipozungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kikao cha NEC mwezi Februari.
Vyanzo vya habari ndani ya CCM vimesema kuwa, lengo la dhana hiyo kukipa sura mpya chama hicho, ili kiendane na wakati pamoja na kukidhi mahitaji ya wapiga kura ambao wengi ni vijana.
Lakini baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho wanatuhumiwa kubadili mantiki na dhana nzima ya kujivua gamba, kwa kuanza kuwaandama watesi wao wa kisiasa, kiasi cha kupendekeza wafukuzwe kwenye uanachama.
Kutokana na upotoshwaji huo, siasa za makundi ambazo kwa kiasi kikubwa zimekidhoofisha chama hicho, sasa zimeshika kasi na kuibua makundi mawili, wale wanaojiita wasafi na wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Katika kikao hicho, pia mgogoro uliopo ndani ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) unatarajiwa kujadiliwa, lengo likiwa kurejesha hali ya amani utulivu ndani ya chombo hicho muhimu kwa uhai wa chama hicho.
Hali mbaya ya uchumi, kuporomoka kwa thamani ya shilingi, kupanda kwa bei za vyakula, tatizo sugu la ajira miongoni mwa vijana, ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kujadiliwa.