AMARIDONG
JF-Expert Member
- Jun 24, 2010
- 2,502
- 180
napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wana jf wote na hasa wasimamizi na wakuu wa jukwaa letu hili lenye mafunzo, manufaa,faida na fahari kubwa kwa jamii yetu.
binafsi nimejiunga na jukwaa hili mwaka huu ila nimefurahi sana kuwa mmoja wa wana jf na nimefurahi zaidi kujifunza na kufundisha kupitia jukwaa hili.mara nyingi najiuliza ni kwa nini jukwaa hili halikuwepo siku za ujana wetu?
napenda kuwapongeza wasimamizi wa jukwaa hili kwa umakini na mmefanya kazi yenu kwa uangalifu wa hali ya juu,ni kweli pamoja na kuwa nimejiunga mwaka huu ila nimewahi pigwa ban kama mbili hivi kutokana na mawazo fulani au misimamo fulani ambayo niliiamini,nashukuru kwa hilo na ninaomba muendelee na ukali na umakini huo kwani hii ndio njia pekee inayotujenga na kutufanya kuleta mawazo bora na imara wakati wote.
napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba msamaha wale wote niliowakosea kwa namna moja au nyingine kwa mwaka wote,na hii maalumu pia kwa wakuu wa jukwaa letu najua nimewaudhi mara kadhaa na mpaka mkanipiga ban kadhaa naomba mnisamehe sana.
nawaahidi kuwa sasa nimekomaa na ninajua maana ya jukwaa letu na mchango wake kwa jamii yetu na ninaahidi kwa mwaka ujao nitakuwa makini na naamini 2011 sitapigwa ban hata moja.
napenda pia kuwaambia kuwa kesho nasafiri kwenda kijijini kwetu marangu sembeti kwa ajili ya sikukuu ya kuzaliwa mwokozi wetu na sikukuu ya mwaka mpya hivyo sitakuwepo hapa mpaka mwakani,nitajitahidi kusoma jf kupitia simu yangu mara zote nikipata nafasi nitachangia ila itakuwa mara chache sana.
mwisho nawatakia wana jamii forum wote sikukuu njema na za furaha sana
ahsanteni tuonane mwakani.
binafsi nimejiunga na jukwaa hili mwaka huu ila nimefurahi sana kuwa mmoja wa wana jf na nimefurahi zaidi kujifunza na kufundisha kupitia jukwaa hili.mara nyingi najiuliza ni kwa nini jukwaa hili halikuwepo siku za ujana wetu?
napenda kuwapongeza wasimamizi wa jukwaa hili kwa umakini na mmefanya kazi yenu kwa uangalifu wa hali ya juu,ni kweli pamoja na kuwa nimejiunga mwaka huu ila nimewahi pigwa ban kama mbili hivi kutokana na mawazo fulani au misimamo fulani ambayo niliiamini,nashukuru kwa hilo na ninaomba muendelee na ukali na umakini huo kwani hii ndio njia pekee inayotujenga na kutufanya kuleta mawazo bora na imara wakati wote.
napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba msamaha wale wote niliowakosea kwa namna moja au nyingine kwa mwaka wote,na hii maalumu pia kwa wakuu wa jukwaa letu najua nimewaudhi mara kadhaa na mpaka mkanipiga ban kadhaa naomba mnisamehe sana.
nawaahidi kuwa sasa nimekomaa na ninajua maana ya jukwaa letu na mchango wake kwa jamii yetu na ninaahidi kwa mwaka ujao nitakuwa makini na naamini 2011 sitapigwa ban hata moja.
napenda pia kuwaambia kuwa kesho nasafiri kwenda kijijini kwetu marangu sembeti kwa ajili ya sikukuu ya kuzaliwa mwokozi wetu na sikukuu ya mwaka mpya hivyo sitakuwepo hapa mpaka mwakani,nitajitahidi kusoma jf kupitia simu yangu mara zote nikipata nafasi nitachangia ila itakuwa mara chache sana.
mwisho nawatakia wana jamii forum wote sikukuu njema na za furaha sana
ahsanteni tuonane mwakani.