Curriculum Specialist
JF-Expert Member
- Oct 8, 2007
- 2,731
- 749
Tafsiri ya viongozi wa serikali hii juu ya maandamano ya CHADEMA imekuwa ni chama cha vurugu na kinachovunja amani! Je Police hawa na viongozi wanasemaje juu ya maandamano ya Amani ya waislam, je wanaweza thubutu kusema uislam ni dini ya vurugu kwasababu imefanya maandamano tena yasiyokuwa na kibali? Je wanasemaje juu watu kutokupigwa, kujeruhiwa au kuuwawa? Je hii haithibitishi kwa wazi kabisa police waliotumwa ndo huwa wanasababisha uvunjifu wa amani na utulivu wanapoingilia maandamano ya amani wa wafuasi wa CHADEMA? Asanteni ndugu zangu waislam kwa kuwaaibisha wauaji!