Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Jamani hili neno ndugu lawama kila mtu anaweza kulitafsiri kivyake lakini kwa mimi ni wale ndugu ambao hawaridhiki hawataki kufanya kazi wao kutwa kucha ni kulalamika tu na kufuatilia mienendo yako..... ndugu unataka kumsomesha unamwambia nakulipia kila kitu kuanzia ada na mambo mengine anaenda shuleni anacheza cheza hadi anafukuzwa au anafeli,, wengine ambao ni wakubwa kwako ......wao kazi ni moja tu kupiga mizinga maro oo unaoa lini.... mara umeoa mke mbaya ... mara oo umenunua nini..mara utakuja kulogwa mara wengine wamekutafutia mganga wa kienyeji.. nani anawaambia kuwa kila mtu anaishi kwa nguvu za giza?........ jamani hawa ndugu lawama nadhani hata nyie mnao au wewe ni mmoja wapo
nawakilisha ,.....
nawakilisha ,.....