Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Ni ile inayohusu kutangazwa kwa mgao wa umeme kama Janga la Taifa! Mh Mnyika alitoa hoja hiyo wakati akisoma Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na kudai kwamba Bunge lisipopitisha Azimio kambi hiyo itaitisha maandamano nchi nzima! Nionavyo mimi huyu Ndugai ametumia "technical knock out" kuizima hoja ya Mnyika kwa sababu ni Spika ndiye aliyetakiwa kuuliza kama kuna wanaounga hoja mkono na sio mtoa hoja yaani Mnyika, badala yake Ndugai amedai kwamba eti "hoja imeishia hewani" na "kujichakachua yenyewe!" Tujadili!