KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 537
Usiku wa kuamkia leo nimeota ndoto. Tulikuwa Mimi na Kikwete kwenye kingo ya mto mmoja mkubwa. Ng'ambo kulikuwa na kundi kubwa la watu wakisikiliza kampeni za kikwete. Kama kawaida yanke akamwaga ahadi yake kwa wale watu kuwa atawajengea daraja mahali pale. Ilipofika wakati wa kuondoka kilichonishangaza ni kuwa huyu Kikwete hakuwa na wasaidizi wala maboardguard. Wakati wa kupanda kingo ya mto aliteleza hivyo nikalazimika kumyanyua mabegani akafanikiwa kutoka na akatokomea bila hata kuniaga. Baada ya muda kidogo zilitelemshwa kamba nyingi na watu ambao siwafahamu ili nikamate mojawapo niweze kutoka kirahisi na kuingia kwenye jengo moja kuwa ambalo lipo karibu na huo mto. Kabla sijakamata ile kamba akatokea mtu mwingine ambaye ni mwanamke akanioshesha njia mbadala ambayo haikuitaji kupanda ile kingo ya mto. Wakati nafikiria ni wapi ili njia aliyonionyesha yule mwanamke itanipeleka, ghafla donto yangu ikaisha.