Mlalahoi naona una hasira sana na mimi tena yaelekea hupendi nizungumze nachokiamini sawaaaa mkuu, mimi nilichosema kuwa huu ni muda wa mabadiliko na mimi nakubali halihalisi wewe unataka kunilazimisha mimi na wana jf wengine kuwa mimi ni mtu mwenye fikra mgando tena kwa kutumia ushahidi wa maandiko yangu yaliyopita sasa naona hapa kuna hisia kuliko uhalisia ina maana wewe ungekuwa ofisini siku niliyochukua kadi ya chama fulani ungeninyima ? kwasababu nilikuwa mwana ccm? ...rejea Biblia takatifu..Bwana kama wewe ungehesabu maovu yetu nani angesimama?.. kisha rudi unihukumu vinginevyo jaribu kunisoma fanya utafiti kisha utabaini sasa hivi mimi ni mtu wa namna gani na mwenye mtazamo gani?
Mkuu umejitahidi kuwa muungwana. Ni wengi waliokuwa wamebeba bendera (CCM) wasiyojua rangi yake. Hivyo mtu akiongoka kama huyu jamaa, tunatakiwa kumpa nafasi na kuangalia mwenendo wake. Upepo wa mabadiliko umeshafika mbali, hata JK anatamani kuwa CDM sema ndo mwenye bendera. Si mnaona anavyojitahd kutekeleza ilani ya CDM? Big up Kambota..!