wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,932
- 4,534
Wanajamvi hii ni mara ya pili sasa nakuja kwenu,
Mimi ni kijana masikini ambaye nina amini ipo siku katika hii mihangaiko yangu nitafanikiwa kimaisha, huwa naota ndoto na %90 huwa zinatokea kweli, miezi mitatu iliyopita niliota pikipiki yangu inaungua moto na kweli jana mida ya saa 12 jioni wakati naifanyia service ilishika moto na kuanza kuungua bahati nzuri nikaiwahi kwa kuizima na maji hivyo haikuharibika.
Usiku wa kuamkia leo nimeota nipo na rais Kikwete pamoja na mkewe Salma tunakula, hii ikiwa ni mara ya tatu kuota nipo na Kikwete, rais Bush akiwa madarakani niliota zaidi ya mara nne nikiwa naye na mara ya mwisho nikiwa nimekaa naye ndani ya Air Force One, Obama nimeota nipo naye mara mbili, Tony Blair niliota nikiwa naye Israel katika dhifa maalumu..
Hata Mkapa, Mwinyi nimeota mara nyingi nikiwa nao, napata hasira napoamka asubuhi na kujikuta nipo na shida zangu tu, ndoto hizi zina maana gani kujirudiarudia miaka yote? Wataalamu wa ndoto mnisaidie.
Mimi ni kijana masikini ambaye nina amini ipo siku katika hii mihangaiko yangu nitafanikiwa kimaisha, huwa naota ndoto na %90 huwa zinatokea kweli, miezi mitatu iliyopita niliota pikipiki yangu inaungua moto na kweli jana mida ya saa 12 jioni wakati naifanyia service ilishika moto na kuanza kuungua bahati nzuri nikaiwahi kwa kuizima na maji hivyo haikuharibika.
Usiku wa kuamkia leo nimeota nipo na rais Kikwete pamoja na mkewe Salma tunakula, hii ikiwa ni mara ya tatu kuota nipo na Kikwete, rais Bush akiwa madarakani niliota zaidi ya mara nne nikiwa naye na mara ya mwisho nikiwa nimekaa naye ndani ya Air Force One, Obama nimeota nipo naye mara mbili, Tony Blair niliota nikiwa naye Israel katika dhifa maalumu..
Hata Mkapa, Mwinyi nimeota mara nyingi nikiwa nao, napata hasira napoamka asubuhi na kujikuta nipo na shida zangu tu, ndoto hizi zina maana gani kujirudiarudia miaka yote? Wataalamu wa ndoto mnisaidie.