Ndolanga ni kiongozi makini kwa kuuwa soka tanzania

nguluvisonzo

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
515
71
Kulingana na maneno yake huyu jamaa alikuwa anatengeneza safu ya kurudi tena kuwa Rais wa TFF baada ya Tenga heshima na wazifa aliopewa ni hatari kwa soka ya TZ nimemsikia mara nyingi sana akihojiwa na Maulid Kitenge wa Redio One majibu aliyokuwa akiyatoa na matendo yake ni hatari sana,nilikuja kugundua huyu jamaa alikuwa akitengeneza MTANDAO kwa ajili ya kuja kuwa RAIS,hatukatai lakini njia anayotumia sio nzuri ni mabaya na hatarishi,Kamati ya Lyato imefanya kazi nzuri na ngumu sana,kwa matendo ya ndolanga inabidi huyu jamaa Ndolanga akae nje ya TFF kabisa.Je walishinda katika vyama vingine vya mikoa wanakidhi haja,taratibu na sheria ya uchaguzi au huko kote kuna mkono wa Ndolanga?
Ndolanga anapenda mambumbumbu nio wawe viongozi ili kutimiza ndoto zake,tena nasema hongera Lyato.
 
HUyu Jamaa akipata cheo hicho tuu cha Uraisi wa TFF, basi soka letu litakuwa kama la somalia, komoro, mauritania na Djibuti. walikuwa wanaajiri kocha mzalendo Kufundisha taifa stars halafu anapaata malipo ya mshara wa daftarini mkubwa kuliko wa mkononi. Huyu Ndolanga, wambura na rage hawafai kabisaa kukalia kiti cha TFF tena maisha yao yote.

Unajua yeye anweza kukipata kiti hicho, kwa sababu ya kuwanunua wenyeviti wa TFF wa mikoa ya kusini na nyanda za juu. Ndio maana walimpatia jina la tyson aliposhinda kesi yake ya kutaka jina lake liwekwe katika wagombea wa FAT mwaka 1996.

Maraisi wa TFF mikoani ni masikini sana na wao kwao maharage ni mboga ya ansa na kambale mboga ya mgeni. hivyo wakinunuliwa tuu, wanakubali kiraisi kumfuata ndolanga na hivyo kutuletea matatizo katika kujenga soka hapa nchini. jamani tuanze sasa hivi kumkataa huyu ndolanga , la sivyo kocha wa Taifa star atakuwa mtu yeyote muuza mkaa karikakoo!
 
Back
Top Bottom