Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,594
Mijadala mingi ya ndoa imeangalia sana mambo ya mapenzi na tendo la ndoa. Haya yameonekana kuwa ndiyo chanzo cha mifarakano na matukio ya kutisha kwenye ndoa. Hata hivyo watu wamekuwa hawajadili masuala yanayohusu mali zinazomilikiwa na wanandoa. Matokeo yake ni vurugu tena nyingine zenye hatari pale inapotokea ndoa kwenda halijojo au kifo cha mmoja wa wanandoa (mara nyingi wanaume). Kuna mambo mengi yanatia wasi na kustua sana.
1. Wanaume wengi wanalalamikia sheria inayowapa wanawake haki ya kumiliki 50% ya mali zilizopatikana kwenye ndoa
2. Baadhi ya wanandoa wanakuwa na mali binafsi ila hawana ujasiri wa kuwaeleza wenzao na badala yake wanaziandikisha kwa majina ya ndugu zao. Mwisho wa siku wanaweza kutapeliwa au zinapotea pale ambapo mhusika anapofariki
3. Hakuna uwazi katika baadhi ya ndoa kuhusu mapato na matumiz ya kila mwanandoa
4. Tulio wengi tunashindwa kuandika wosia na hivyo kusababisha kizazaa pale inapotokea msiba wa mwanandoa (mara nyingi wanaume).
Je, kuna ugumu gani kujadili mambo ya mali kwenye ndoa na kuweka kila kitu sawa?
1. Wanaume wengi wanalalamikia sheria inayowapa wanawake haki ya kumiliki 50% ya mali zilizopatikana kwenye ndoa
2. Baadhi ya wanandoa wanakuwa na mali binafsi ila hawana ujasiri wa kuwaeleza wenzao na badala yake wanaziandikisha kwa majina ya ndugu zao. Mwisho wa siku wanaweza kutapeliwa au zinapotea pale ambapo mhusika anapofariki
3. Hakuna uwazi katika baadhi ya ndoa kuhusu mapato na matumiz ya kila mwanandoa
4. Tulio wengi tunashindwa kuandika wosia na hivyo kusababisha kizazaa pale inapotokea msiba wa mwanandoa (mara nyingi wanaume).
Je, kuna ugumu gani kujadili mambo ya mali kwenye ndoa na kuweka kila kitu sawa?