ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Katika uchunguzi wa muda mrefu, inaonekana kuwa wazee wengi wa kichaga hawapo karibu sana na wake zao wa ndoa,ukiacha wale ambao huwatelekeza wake migombani (Moshi), ukitembelea majumbani huko Moshi, hata wale waliopo huko vijijini, hawalali nyumba au chumba kimoja na wenzi wao katika ndoa. Labda yawezekana kabisa mila za Kichaga haziruhusu watu wazima kuishi pamoja (kuna ule utani eti kina mama wapo busy zaidi na kusakanya fedha kuliko mapenzi), lakini kwa kiasi fulani yaonyesha wazee wengi ambao wameoa wachaga wenzao wanatumia desturi hiyo ya kikabila kufanya mambo ya kihuni katika umri wa utu uzima (kuishi na vibinti vyenye umri sawa na wana wao)na pengine wanakuwa wababe sana kwa wake zao wa ndoa, kina mama wengi kule Moshi wanaheshima kuu kwa waume zao kwa kila kitu hata akipotoka si rahisi sana kuhojiwa!!. Nina takwimu za familia nyingi tu zilizo katika mahusiano haya tata!. Labda wenzetu wanaweza kutuelimisha kwa nini ipo hivi!