Pierre III
Member
- Jun 1, 2010
- 34
- 0
WanaJF. Nina miezi mitano kwenye ndoa tuliyofunga kiserikali kwa sababu za kidini, kama kawaida maisha yanaendelelea vizuri bila migogoro yoyote. My wife anatabia ya kunieleza kila kitu tukiwa chumbani, yaani ni muwazi sana. Kila akikaribia siku zake anatoa tarifa, lakini mwezi ulopita aliniambia kua siku zake zimechelela isivyo kawaida yake( yaani badala ya tarehe 28 au 29 au 30 au 31 au 1). Nkamwambia labda umenasa? Alivyosikia hivyo kasema haiwezekani kupata mimba sasa hivi kabla sijapata kazi( ndo kamaliza chuo bado hajapata kazi). Ilipofika tarehe 5 akanipigia simu kua ameona siku zake, na kweli nilipofika nyumbani niliona akiweka pads. Baada ya wiki mbili nlikua sijiskii vizuri kichwa kilikua kinauma, nikachukua kibox changu cha kutunzia madawa, cha kushangaza sijakuta dawa yoyote ndo ikabidi niulize my wife zimeenda wapi? Akaniambia hajui, ila baada ya kumbana akakiri kua yeye ndo alokula hizo dawa kwani alikua anahisi maumivu makali kwenye kizazi hasa anapokua anakojoa. Nikamuuliza kulikono unaumwa lakini hukutaka nijue? Akasema aliogopa kwa sababu mimi hua namkataza kula dawa bila kushauriwa na daktari. WanaJF nina wasiwasi kua my wife katoa mimba baada ya kula zile dawa ( ila sijamwambia) je inawezekana siku za mwanamke kuchelewa kwa siku tano au sita ( 35/36 days monthly period)?