Ndoa Yangu haina mapenzi

Jikaze na huyo huyo mkeo kama vile unakunywa klorokwini! Siku moja mapenzi yatarudi!
 
avatar kuonesha msisitizo kwamba aliyemchoka mwenzie sio mume ni mke.....
@Max duh sijakusoma kihivi longi sana mkubwa!!!
thanks I will keep that in my mind till the time comes!!!
 
Mkuu,

Tatizo lako si la mmoja. Yawezekana wanaoandika hapa wanaandika bila kujua umeathirika vipi kisaikolojia.

Mimi ni mtu mwenye ndoa na ningependa nikushauri kwa ninavyoona inafaa (kama ninavyoiishi ndoa yangu).

Mosi; popote penye tatizo pana chanzo. Hujatufahamisha chanzo cha wewe kumchoka ni kipi, unakijua lakini inaelekea imekuwa ngumu kukiweka bayana, ingekuwa rahisi kwetu kuweza kukushauri kulingana na chanzo cha tatizo.

Pili; kuchokana kwenye ndoa kunatokana na mambo mengi, yawezekana mwenzi wako amebeba ujauzito au kajifungua hivyo yuko kwenye kipindi kigumu kimatamanio, hapa unatakiwa kumvumilia, ni kipindi cha mpito. Yawezekana unamhisi mwenzio kuwa na mahusiano na mtu/watu kitu ambacho ni obvious mapenzi kwako pia yatashuka. Yawezekana pia wewe binafsi umeruhusu mambo ambayo unajua wazi kuwa yatapunguza mapenzi yenu. Ukifanya kazi muda mrefu bila kupumzika ni wazi hata mwili unachoka na unajikuta una muda mdogo sana wa kuwa na mwenzi wako, unaanza kupoteza hamu nae.

Tatu; kama mmefunga ndoa kihalali; kumbuka ahadi zenu za ndoa, ulisema utampenda katika shida na raha, huu ndio wakati wa shida, unatakiwa kuitekeleza ahadi yako sasa! Lakini pia, hata kama hamjafunga ndoa kihalali ila mnaishi kama mme na mke; lazima kuna kitu kiliwafanya mkafikia maamuzi haya, hamkulazimishwa na mtu. Uliona katika viumbe wote huyo ndiye anafaa kuwa mwandani wako; kabla hata ya kutueleza ulitakiwa kuwa umeyaongea na mwenzi wako na kutafuta suluhu ya matatizo yenu.

Mkuu; ndoa ni tamu sana, ina raha mno! Inahitaji kuelewa kuwa mapenzi huchochewa ili yaendelee kukua na kuchanua, wewe ndiye unatakiwa sasa baada ya kubaini kuwa umepungukiwa mapenzi kujifunza ni kipi kizuri kwa mwenzi wako na kuhakikisha unakuwa unakiona kila wakati. Sitaki kuamini ulimpenda sababu ya sura au maumbile tu; kuna mvuto flani ulikupeleka kwake. Pata muda, mwende nje ya maeneo yenu mnapoishi (outing) mkakae na kujaribu kula vilivyopikwa na wengine huku mkifurahia pamoja; jaribu kuilazimisha furaha ikibidi lakini hatma yake utagundua tofauti.

Yawezekana pia chanzo ni kubadilika tabia kwa mwenzi wako na unamfichia siri; hapo ndipo pia unatakiwa kumweleza katika faragha juu ya tatizo lake. Usimweleze kwa kumgombeza au kwa sauti kubwa; kuwa na hekima, mwambie polepole huku ukimweleza unampenda kiasi gani na mabadiliko unayoyaona yanavyokuathiri sana mpaka kupoteza hamu yako kimapenzi kwake.

Mkuu, naweza kuandika mengi lakini bila kujua chanzo inakuwa ni kumpigia mbuzi gitaa, hebu kuwa wazi kidogo tuinusuru ndoa yako, ni ya thamani kwako na thamani kwetu pia kwani mkiparana, wanaoumia ni watoto ambao huenda wakahangaika mitaani na watakaokutana nao ni sisi (Jamii).

Ahsante

kwakweli nakushukuru kwa kusoma ushuri wako nimehisi kupunguza kitu maana umegusa mambo mawili kama sio matatu ambayo nadhani ni chanzo cha kuchoka ila nashukuru umenipa pia mwanga Ahsante sana tena sana mungu akuongoze uwe mshauri mwema
 
Mkuu mapenzi unayajenga mwenyewe, sivyo utaishia kuishi na mkeo kwa mazoea tu! (and this makes most of the holy unions)
 
najisikia kumchoka mwenzangu bila sbbu yuko sawa kila k2 ila sina ham naye tena kama zamani tulipokuwa wachumba najitahidi nashindwa sina nyumba ndogo ila natamani wakti mwingine ila cjawahi fanya ila mwenzangu wa ndoa nimechoka kabisa hajanikosea haja badilika ila nahisi kumchoka nisaidieni nifanyeje jamani?
Naona hujawa muwazi na mkweli. Lazima una sababu au kisa kinacho kufanya umchoke mwenzako hata kama sababu hiyo haina maana sana. Vinginevyo wewe ni UNIQUE duniani. Kama wewe ni mkristo piga magoti umwombe mungu aitoe hiyo pepo ya chuki bila sababu na uendelee kuishi na mkeo maana alichokiunganisha mungu binadamu hawezi kukitenganisha. Kama wewe ni mwisilamu oa mke mwingine ili kuepuka dhambi ya zinaa na pengine HIYO itakupa nafasi ya kugundua kwamba mkeo wa kwanza ni bora na utaendelea naye pia.
 
Mie sikushangai Ngoma zom........
Ila jaribu kumuomba mwenzi wako akupe muda hata wa wezi mmoja ukae peke yako kama likizo au anything .ujaribu kurefresh mind yako hayo ndo maisha ya ndoa yana mambo mengi na majaribu ya kila namna...
Pia nadhani kuna mambo hujasema kuhusiana na mwenza wako
 
najisikia kumchoka mwenzangu bila sbbu yuko sawa kila k2 ila sina ham naye tena kama zamani tulipokuwa wachumba najitahidi nashindwa sina nyumba ndogo ila natamani wakti mwingine ila cjawahi fanya ila mwenzangu wa ndoa nimechoka kabisa hajanikosea haja badilika ila nahisi kumchoka nisaidieni nifanyeje jamani?

ndugu... ndoa siyo kitanda cha mawaridi kisichokuwa na miiba.
Ndoa tunaingia kwa pupa bila kutafakari hasa nini maana ya kuji- commit kwa mtu mmoja kwa maisha yetu yote.Unasema umemchoka mwenzio japo hajakufanyia lolote baya! Hii ni ajabu maana kuchokana kwenye ndoa mara nyingi huletwa na mambo tunayofanyiana ya kuumiza au kukera yenye kujirudiarudia.Huwezi wewe kuamua kumchukia mtu uliyempenda kiasi cha kufunga naye pingu za maisha pasina sababu kubwa ya msingi - sababu inayotikisa mizizi ya uhusiano.Huwezi wewe kumchoka kipenzi chako aliyekuwa anakufanya uzuzuke kila ukimuwaza bila chanzo chochote. Avatar yako inaoonyesha wewe ni mwanamke. Mara nyingi wanawake huwa na commitment ya ajabu sana kwenye ndoa zao.Ukiona mwanamke kaamua kufanya tofauti na alivyoji commit ujue kuna kisa au jambo lenye kugusa moyo zaidi ya kugusa hisia za mwili.
1. jE, uliiingia kwenye ndoa shauri ya kitu - na hicho kitu sasa hakipo?
2. Umeshajiweka kwenye viatu vya mwenzio ukajipima kuona kama ungefanyiwa hivyo wewe ungejisikia vipi?
3. Ndoa yako ina umri wa zaidi ya miaka 5? kama hapana, uliingia kwenye ndoa kwa sababu gani - ulifuata mkumbo?
4. Maisha siyo kujisikia vizuri tu wewe binafsi. Ni pamoja na kujitoa kwa sababu ya furaha ya wengine.Je wewe unajitoa au ni mtu mbinafsi mwenye kujifikiria wewe mwenyewe tu?
5. Unadhani ukibadilisha na kuwa na mwenza mwingine, utaweza kudumu naye au ndio baada ya muda naye utamchoka maana wewe humchokaga mtu hata kama hajakufanyia baya lolote. Mwisho wako utakuwa vipi?
6.Ukitizama umri wako, inaelekea wewe bado ni kijana sana.Je ukiwa na umri mkubwa bado utakuwa na hulka hiyo ya kumchoka mwenzio?...
TAFAKARI...............
 
ndugu... ndoa siyo kitanda cha mawaridi kisichokuwa na miiba.
Ndoa tunaingia kwa pupa bila kutafakari hasa nini maana ya kuji- commit kwa mtu mmoja kwa maisha yetu yote.Unasema umemchoka mwenzio japo hajakufanyia lolote baya! Hii ni ajabu maana kuchokana kwenye ndoa mara nyingi huletwa na mambo tunayofanyiana ya kuumiza au kukera yenye kujirudiarudia.Huwezi wewe kuamua kumchukia mtu uliyempenda kiasi cha kufunga naye pingu za maisha pasina sababu kubwa ya msingi - sababu inayotikisa mizizi ya uhusiano.Huwezi wewe kumchoka kipenzi chako aliyekuwa anakufanya uzuzuke kila ukimuwaza bila chanzo chochote. Avatar yako inaoonyesha wewe ni mwanamke. Mara nyingi wanawake huwa na commitment ya ajabu sana kwenye ndoa zao.Ukiona mwanamke kaamua kufanya tofauti na alivyoji commit ujue kuna kisa au jambo lenye kugusa moyo zaidi ya kugusa hisia za mwili.
1. jE, uliiingia kwenye ndoa shauri ya kitu - na hicho kitu sasa hakipo?
2. Umeshajiweka kwenye viatu vya mwenzio ukajipima kuona kama ungefanyiwa hivyo wewe ungejisikia vipi?
3. Ndoa yako ina umri wa zaidi ya miaka 5? kama hapana, uliingia kwenye ndoa kwa sababu gani - ulifuata mkumbo?
4. Maisha siyo kujisikia vizuri tu wewe binafsi. Ni pamoja na kujitoa kwa sababu ya furaha ya wengine.Je wewe unajitoa au ni mtu mbinafsi mwenye kujifikiria wewe mwenyewe tu?
5. Unadhani ukibadilisha na kuwa na mwenza mwingine, utaweza kudumu naye au ndio baada ya muda naye utamchoka maana wewe humchokaga mtu hata kama hajakufanyia baya lolote. Mwisho wako utakuwa vipi?
6.Ukitizama umri wako, inaelekea wewe bado ni kijana sana.Je ukiwa na umri mkubwa bado utakuwa na hulka hiyo ya kumchoka mwenzio?...
TAFAKARI...............
duh! huyu dada yuko level nyengine, hii ushauri imetulia sana aisee, ushauri kama hii ughaibuni wanalipia bana! senksi kwa kuiweka free.
 
mama signatory yako mbona nzuri sana
ingia kimaombi zaidi utauona muujiza
Ee bwana utete nao wanao teta nami pigana nao wanao pigana nami... Zab 35:1-28:)
 
Back
Top Bottom