Sinai
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 288
- 47
:msela::msela:Kuna jambo limetokea hapa mtaani kwetu jana. Kuna kijana mmoja ambaye kwa kweli alikuwa anajulikana kama mtu wa vimwana sana, ikafika wakati akataka kumwoa tena kwa ndoa mtoto wa mchungaji wa kanisa moja la Moroviani. Wazazi wa binti wakatoa sharti kuwa binti yao hawezi kuolewa hadi pale watakapo pima afya wote wawili kwa pamoja. Kijana hakuwa tayari, pengine kutokana na mienendo yake kuwa ya ovyo, lkn wazazi wa binti wakaforce kwa kuamini kwamba binti yao ni virgin, hivyo hana tatizo lolote! Baada ya mjadala mrefu, jana wakaamua kupima, majibu yakaonyesha binti ambaye wazazi wake wanaamini ni virgin ana HIV + na kijana yupo safi, tena baada ya kupima mara mbili ktk hospitali tofauti ikiwemo ya mkoa!!!!!!
Ndoa ilikuwa ifungwe jumamosi tarehe 12/02/2011. Sasa kijana ameamua kuachana na binti, na binti ameamua kunywa dawa za kutoa uhai, lkn hadi naandika hapa, bado kalazwa hosp. na hali yake sio nzuri, drip sita kesha maliza. Hapo nani alaumiwe? Wazazi wa binti au kijana? Je ni vizuri wazazi kumwamini binti kupita kiasi? Binti anamiaka 26, eti bado wazazi wanaamini kuwa bado hajawahi ku-do, ktk ulimwengu wa sasa lnawezekana hiyo? Nawakilisha!:msela::msela:
Ndoa ilikuwa ifungwe jumamosi tarehe 12/02/2011. Sasa kijana ameamua kuachana na binti, na binti ameamua kunywa dawa za kutoa uhai, lkn hadi naandika hapa, bado kalazwa hosp. na hali yake sio nzuri, drip sita kesha maliza. Hapo nani alaumiwe? Wazazi wa binti au kijana? Je ni vizuri wazazi kumwamini binti kupita kiasi? Binti anamiaka 26, eti bado wazazi wanaamini kuwa bado hajawahi ku-do, ktk ulimwengu wa sasa lnawezekana hiyo? Nawakilisha!:msela::msela: