Ndoa na Hali ngumu ya Uchumi

Boney E.M.

JF-Expert Member
Jan 22, 2007
425
35
Hali ya sasa kiuchumi sio nzuri hata katika vipato vyetu hapa Tz. Mara nyingi matumizi yanazidi uwezo wetu wa kipato. Inajitokeza kuwa kuna kisa 'live' cha wanandoa fulani wana tatizo kwani mahitaji ya mwanamke bado yako juu ilhali kipato kimepungua. Mke anamwambia mumewe sijui utapata wapi pesa sie tunachotaka ni maisha mazuri. Hili limepelekea hata mwanamume kunyimwa unyumba na kuleta mifadhaiko ndani ya nyumba hiyo. Je tuwashauri nini hawa wanandoa waendelee kuishi kwa amani? Mke hataki kupunguza matumizi na mume hana vyanzo mbadala vya kipato. je madai ya mwanamke ni halali?
 
ndoa zina mambo jamani, kila ndoa na lake....sasa huyu mwanamke mwenzangu kama yeye anaona kuna mpungufu mahali c wakae waeleweshane na yeye asaidie kuziba hilo gap lililopo kwasasa?.....sasa kumnyima nyumba ndio kutatua tatizo?
 
Ugumu wa hali unao wewe mwenyewe,na jinsi ya kukabiliana nao ni wewe mwenyewe.Mbona wengine wanapeta kiulaini tu.Bongo hakuna formula bwana!!Kwani kila muziki una mwimbaji wake na kila masika na mbu wake.Maisha yako ya ndoa , yangu na ya Plato ni tofauti sana hata kama ungetupa kiasi sawa cha kipato.Kila mmoja ana mtizamo wake tofauti tena basi kila mmoja ana malengo tofauti kabisa katika maisha.Waswahili wanasema ni kwa kiasi gani unavyozichanga karata zako za maisha ndipo utahesabu kufanikiwa au kufeli.
 
Kama hataki kupunguza mwache aendelee atakiona cha moto. Mwanaume wewe save kivyako ili usije adhirika then huyo mama afanya anavyotaka akifulia atatia akili.

Mwanaume kama mkeo hataki kukupa unyumba nenda katafute small house uone anavyorudi speed.

Wanawake wengine bwana wapuuzi.
 
Hali ya sasa kiuchumi sio nzuri hata katika vipato vyetu hapa Tz. Mara nyingi matumizi yanazidi uwezo wetu wa kipato. Inajitokeza kuwa kuna kisa 'live' cha wanandoa fulani wana tatizo kwani mahitaji ya mwanamke bado yako juu ilhali kipato kimepungua. Mke anamwambia mumewe sijui utapata wapi pesa sie tunachotaka ni maisha mazuri. Hili limepelekea hata mwanamume kunyimwa unyumba na kuleta mifadhaiko ndani ya nyumba hiyo. Je tuwashauri nini hawa wanandoa waendelee kuishi kwa amani? Mke hataki kupunguza matumizi na mume hana vyanzo mbadala vya kipato. je madai ya mwanamke ni halali?

...ni mahitaji gani hayo?
 
Hii inaonesha jinsi wanawake wengi walivyo hasa wale wanaowapenda wanaume kwa kile walichonacho na si kwa mapenzi ya kweli.
Njia pekee ya huyu jamaa kujinasua na huyo ATM wake ni kufind a small house faster dis gonna be da only solution!
 
Sikubaliani na ushauri wa huyo mkuu wa nyumba kuwa na nyumba ndogo. Kwa sababu tatizo kubwa hapo ni myeyuko wa uchumi wa familia(Baba). Haina ubishi kuwa kumiliki nyumba ndogo kunahitaji bajeti yake (gharama). Sasa kuwa na nyumba ndogo si kuongeza makali ya huo myeyuko wa uchumi wa familia!! Au wakuu imekaaje hii!!

Ni maoni yangu tuu!!!
 
Last edited:
Back
Top Bottom