PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Kuna mama mmoja ameolewa kwa ndoa ya kiislamu. Ana watoto wawili. Mtoto mmoja wa kwanza kamzaa na mume wake wa Kwanza, mtoto wa pili kamzaa na mume wake wa Pili. Huyu mwanamke anafahamika kabisa katika familia zote za wanaume hao. Na anaheshimika kama mke halali. Wazazi wa familia ya mume wa Pili wanamfahamu lakini hawafahamu kuwa ameolewa sehemu nyingine. Mume wa pili anajua ameoa mke wa mtu na yuko comfortable lakini mume wa kwanza hajui lolote. Huyu mwanamke anaamua wiki hii aende kwa mume mmoja. Sehemu moja anadanganya kuwa, mfano: Nasafiri kikazi, mara leo nimefanya kazi hadi asubuhi n.k. Lakini hasa mume wa kwanza ndiye anadanganywa make hajui kuwa mkewe amelowa kwa mume mwingine. Binafsi nimemshauri amwache huyo mume wa Pili na kama ikibidi amweleze mume wake wa Kwanza kuwa mtoto wao wa Pili siyo wa mume huyo wa Kwanza, ili apelekwe kwa mume huyo wa Pili na ikibidi aachane naye kabisa lakini amegoma kabisa kusikiliza ushauri wangu. Jamani wanaJF (hasa akina dada)mnatoa ushauri gani kwa huyo mwanamke mwenzenu??? Toeni ushauri wenu nitaufikisha sasa hivi kwake. Ahsanteni!!