Ndoa kazi...!

mie nimeolewa kwa zaidi ya miaka 10. Mwanzoni nilikuwa mkweli sana kuhusu financial zangu kwa mume wangu..yani kila ninachokipata namwambia halafu tunajadili cha kufanyia..niliamini na mwenzangu yuko hivyo, lkn baadae nikaja kugundua kuwa haniambii ukweli kuhusu kipato chake(baada ya kugundua asset zake ambazo alinificha) na mambo kadhaa ambayo aliyafanya bila kunishirikisha..tuliongea ili tuyamalize na kila mmoja wetu asimfiche mwenzie, aliomba msamaha na akaahidi kujirekebisha lkn hajajirekebisha..kila mara nimekuwa nikigundua/nikiambiwa mambo anayofanya kimya kimya.. Nikimuuliza amekuwa akitahayari tu hana la kusema..nikasema hakuna haja ya kugombana kwa sbb ya kipato cha mtu, nami si ninacho cha kwangu?...nami nikawa naficha kipato changu, simwambii na wala hajui nina shilingi ngapi..nimefungua account bank nyingine naweka huko akiba na wala hajui(ile bank anayojua anayo na password na yuko free akitaka hela nampa kadi).. Nimejenga nyumba 1, hajui na sasa nategemea kujenga nyingine(sitegemei kumwambia vile vile).. Matumizi ya nyumbani nachangia km kawaida tena mara kibao namkopesha kwani mwenzangu hajui bajeti mara kwa mara anaishiwa hata ya mafuta(anaamua kupanda daladala)..
Kwa hivo tatizo ni nyie wanaume sio wakweli..wanawake ni wakweli pale mnapowashirikisha na wanajua bajeti..ni mara chache sn utakuta mwanamke kaishiwa hadi nauli

vipi siku ukipata ajali ukatoweka duniani au umeugua ghafla na madaktari wamesema upelekwe india? Mumewe kucheki acc hakuna kitu anabaki anakulilia na wewe huna fahamu.....
Me nikushauri tu kaeni chini muongee muelewane itapendeza sana vinginevyo haya siyo maisha
 
... wengi wamejadili hapa lakini hoja ya taarifa za kweli juu vipato vya wandoa ni jambo la msingi sana, hasa ukizingatia hali ya sasa "inflation".haingii akilini, kumkopea mume kwa mkea huku wakiwa hawajui fedha zimetoka wapi!
 
Dada yangu alikuwa kwenye similar situation.

Na ana mkwanja wa nguvu na mumewe ana zake. Kutokana na matatizo ya ukoo upande wa mume wake ndoa yao imekuwa na ups and downs za nguvu (japo mume wake ni the most faithful husband). Ikafika kipindi mwanaume kipato karibu chote anapeleka kwa dada zake, mama yake etc bila kumshirikisha dada...akawa anasomesha watoto lukuki wa ndugu zake.

Sister akahamua kila mtu kivyake when it comes to finacne. Kajenga majumba kibao...yeye na mumewe wana nyumba moja tu waliyoshirikiana kujenga...mumewe kajiridhikia.

Ila sisi tulimwambia amwambie mumewe kuhusu mali zake zote even if ziko kwenye jina lake...kwani kuna leo na kesho watu wakijua hiyo weakness wataja dhulumu watoto wake.

Kwenye mali hakuna cha sijuhi namshirikisha kaka sijuhi dada, namficha mume; nshaona wengi wanakufa wajomba wanatia ndani mali za watoto. I trust my hubby than my ndugu when it comes to my properties kwani najua hawezi kuwachukia hence kuwadhulumu watoto wetu.

Sister japo ni mkali na ashauriki especially ukizingatia washauri wenyewe ni wadogo zake...lakini hili lilimuingia na kwa sasa mume wake ameshajua mkewe ana mali kiasi gani.

Let him know hata kama hatakuwa na say kwenye hizo mali.

mie nimeolewa kwa zaidi ya miaka 10. mwanzoni nilikuwa mkweli sana kuhusu financial zangu kwa mume wangu..yani kila ninachokipata namwambia halafu tunajadili cha kufanyia..niliamini na mwenzangu yuko hivyo, lkn baadae nikaja kugundua kuwa haniambii ukweli kuhusu kipato chake(baada ya kugundua asset zake ambazo alinificha) na mambo kadhaa ambayo aliyafanya bila kunishirikisha..tuliongea ili tuyamalize na kila mmoja wetu asimfiche mwenzie, aliomba msamaha na akaahidi kujirekebisha lkn hajajirekebisha..kila mara nimekuwa nikigundua/nikiambiwa mambo anayofanya kimya kimya.. nikimuuliza amekuwa akitahayari tu hana la kusema..nikasema hakuna haja ya kugombana kwa sbb ya kipato cha mtu, nami si ninacho cha kwangu?...nami nikawa naficha kipato changu, simwambii na wala hajui nina shilingi ngapi..nimefungua account bank nyingine naweka huko akiba na wala hajui(ile bank anayojua anayo na password na yuko free akitaka hela nampa kadi).. nimejenga nyumba 1, hajui na sasa nategemea kujenga nyingine(sitegemei kumwambia vile vile).. matumizi ya nyumbani nachangia km kawaida tena mara kibao namkopesha kwani mwenzangu hajui bajeti mara kwa mara anaishiwa hata ya mafuta(anaamua kupanda daladala)..
kwa hivo tatizo ni nyie wanaume sio wakweli..wanawake ni wakweli pale mnapowashirikisha na wanajua bajeti..ni mara chache sn utakuta mwanamke kaishiwa hadi nauli
 
mie nimeolewa kwa zaidi ya miaka 10. mwanzoni nilikuwa mkweli sana kuhusu financial zangu kwa mume wangu..yani kila ninachokipata namwambia halafu tunajadili cha kufanyia..niliamini na mwenzangu yuko hivyo, lkn baadae nikaja kugundua kuwa haniambii ukweli kuhusu kipato chake(baada ya kugundua asset zake ambazo alinificha) na mambo kadhaa ambayo aliyafanya bila kunishirikisha..tuliongea ili tuyamalize na kila mmoja wetu asimfiche mwenzie, aliomba msamaha na akaahidi kujirekebisha lkn hajajirekebisha..kila mara nimekuwa nikigundua/nikiambiwa mambo anayofanya kimya kimya.. nikimuuliza amekuwa akitahayari tu hana la kusema..nikasema hakuna haja ya kugombana kwa sbb ya kipato cha mtu, nami si ninacho cha kwangu?...nami nikawa naficha kipato changu, simwambii na wala hajui nina shilingi ngapi..nimefungua account bank nyingine naweka huko akiba na wala hajui(ile bank anayojua anayo na password na yuko free akitaka hela nampa kadi).. nimejenga nyumba 1, hajui na sasa nategemea kujenga nyingine(sitegemei kumwambia vile vile).. matumizi ya nyumbani nachangia km kawaida tena mara kibao namkopesha kwani mwenzangu hajui bajeti mara kwa mara anaishiwa hata ya mafuta(anaamua kupanda daladala)..
kwa hivo tatizo ni nyie wanaume sio wakweli..wanawake ni wakweli pale mnapowashirikisha na wanajua bajeti..ni mara chache sn utakuta mwanamke kaishiwa hadi nauli


Kwanza nikukaribishe sana kamusi kwenye hii mijadala isiyokuwa na mwisho. Na pili nikupongeze kwa kuweka michango mizuri sana.

Katika ndoa zetu, kuna mambo mengi ambayo tungekuwa tunapata feedback kama hii labda zingetusaidia sie wenyewe au wale wanaotarajia kuungana nasi kwenye hii taasisi ya ndoa, ambayo kwa ujumla ni complex sana!

Nakubaliana na ulichokifanya kwani mwenye lawama ni huyo mwenzako. Hata hivyo naomba nikiri kuwa, wanaume mara nyingi tunajidai kuwa ni wajanja...ila linapokuja suala la mahusiano, wanawake ni wajanja karibia mara 100 zaidi yetu.

Wewe mwache huyo aendelee kuficha ila siku atakapogundua ulivyo smart, ataishia kuona aibu na asipate mahali pa kuficha hata uso wake!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
sio kwamba ni siri hivyoo, ni mr tu ndio hajui, ila ndugu zangu (wachache) nimewaonyesha na wanajua, marafiki zangu ( wachahe waaminifu) nimewaambia na nimewaonyesha..na pia nimeandika usia in case nitakufa leo, so watoto wangu hawatadhulumiwa...km Mungu atanipa umri na ikiwa tutakuwa bado pamoja nitamwambia baadae lkn sio leo..

ujue hata mie sipendi kabisa na wkt mwingine nafsi inaniambia si umwambie tu!! lakini actually ni yy ndie aliyenifundisha..mimi nilikuwa sijui kuficha kipato changu, na km ni kuongea tumeshaongea lkn habadiliki..na hii imesaidia sn kupunguza ugomvi wa mara kwa mara na tumekuwa na amani..kwani mimi nimekuwa mpoole simuulizi wl sikasiriki ninapojua mambo yake(kwani nami nina yangu).

kuna siku nilimtest nikamwambia nimenunua shamba (ni kweli nilinunua kimya kimya) akamind sn, na akapunguza kutoa matumizi ya nyumbani na ada za shule za watoto (ili mimi nitumie za kwangu nisiwe na akiba au nisiweze kufanya mambo yangu) nikasema sasa huyu dawa yake ni kunyamaza tu
anyway time will tell may be one day atabadilika au mimi nitabadilika but for the time being hali ndio iko ivo..
 
mie nimeolewa kwa zaidi ya miaka 10. mwanzoni nilikuwa mkweli sana kuhusu financial zangu kwa mume wangu..yani kila ninachokipata namwambia halafu tunajadili cha kufanyia..niliamini na mwenzangu yuko hivyo, lkn baadae nikaja kugundua kuwa haniambii ukweli kuhusu kipato chake(baada ya kugundua asset zake ambazo alinificha) na mambo kadhaa ambayo aliyafanya bila kunishirikisha..tuliongea ili tuyamalize na kila mmoja wetu asimfiche mwenzie, aliomba msamaha na akaahidi kujirekebisha lkn hajajirekebisha..kila mara nimekuwa nikigundua/nikiambiwa mambo anayofanya kimya kimya.. nikimuuliza amekuwa akitahayari tu hana la kusema..nikasema hakuna haja ya kugombana kwa sbb ya kipato cha mtu, nami si ninacho cha kwangu?...nami nikawa naficha kipato changu, simwambii na wala hajui nina shilingi ngapi..nimefungua account bank nyingine naweka huko akiba na wala hajui(ile bank anayojua anayo na password na yuko free akitaka hela nampa kadi).. nimejenga nyumba 1, hajui na sasa nategemea kujenga nyingine(sitegemei kumwambia vile vile).. matumizi ya nyumbani nachangia km kawaida tena mara kibao namkopesha kwani mwenzangu hajui bajeti mara kwa mara anaishiwa hata ya mafuta(anaamua kupanda daladala)..
kwa hivo tatizo ni nyie wanaume sio wakweli..wanawake ni wakweli pale mnapowashirikisha na wanajua bajeti..ni mara chache sn utakuta mwanamke kaishiwa hadi nauli

Uwiii,naogopaje sasa,ukifa ghafla mali zako si zitapotea!maana hata ndugu yako anaweza wadhulumu watoto wako,yani ni hatari sana,jirani yangu kuna nyumba imeshaezekwa ina 8 year sijawahi muona hata mwenye nyumba,inasemekana alishakufa na mumewe alikuwa hajui,3years ago kahamia mganga wa kienyeji,yani mtaa mzima kina mama tunasali mganga ahame but wapi,nyumba ishachakaa kabisa.
Mwingine fundi aliemjengea ndio kahamia,na inasemekana fundi ndio aliyemuua baada ya kugundua hakuna mtu anajua kama anajenga,dada wa marehemu amehangaika sana kuifuatilia nyumba imeshindikana maana hana document zinazoonyesha marehemu ndio mmiliki,yani ni story ndefu.
 
Kwanza nikukaribishe sana kamusi kwenye hii mijadala isiyokuwa na mwisho. Na pili nikupongeze kwa kuweka michango mizuri sana.

Katika ndoa zetu, kuna mambo mengi ambayo tungekuwa tunapata feedback kama hii labda zingetusaidia sie wenyewe au wale wanaotarajia kuungana nasi kwenye hii taasisi ya ndoa, ambayo kwa ujumla ni complex sana!

Nakubaliana na ulichokifanya kwani mwenye lawama ni huyo mwenzako. Hata hivyo naomba nikiri kuwa, wanaume mara nyingi tunajidai kuwa ni wajanja...ila linapokuja suala la mahusiano, wanawake ni wajanja karibia mara 100 zaidi yetu.

Wewe mwache huyo aendelee kuficha ila siku atakapogundua ulivyo smart, ataishia kuona aibu na asipate mahali pa kuficha hata uso wake!!

Babu DC!!

asante sana babu dc, maisha yanakufanya mtu ubadilike na kuwa mtu mwingine kabisa..na ni vema ktk ndoa km utaweza kupunguza migogoro isiyo ya lazima..kwanza unatakiwa umsome mwenzako yukoje, halafu na wewe akuelewe ili muweze kuishi kwa pamoja..ikiwa mtakubaliana well and good, mtakwenda barabara moja, lkn ukiona mwenzako haelekei hata baada ya majadiliano mengi, huna haja ya kuendelea na ugomvi usio na maana sbb huyo hatabadilika kamwe( as for my husband) kwa ivo unatakiwa utafute njia ya kuishi naye kama alivyo bila mikwaruzo(ishi naye hivyo hivyo na mapungufu yake) lkn akili kichwani mwako..vinginevyo km ni mdada basi kila siku utafungasha virago kurudi nyumbani au utaishia kununa(on daily basis) na hapo tena ndoa itakuwa ngumu
 
kweli kusoma c kuelewa.,mkuu sijakupata kabisa.nahisi kama ulikuwa unadesa mahala halafu jamaa akafunga desa lake!
Nina urafiki sana na mdada
mmoja ambaye ameolewa, mdada huyu tunafanya naye benki moja hivi. mume
wake tuna urafiki pia lakini sio kihivo kama mke wake, nadhani ni
kwasababu tunafanya naye ofisi moja. Wiki iliyo pita shemeji alinikopa
laki! nikaahidi kumpatia jioni, kwakuwa mke wake yupo maternity live,
naye kwa bahati alinipigia simu akiniomba nimuangalizie balance kwenye
account yake, nilishikwa na butwaa kuona salio la ukweli. Nikajua hapa
kuna tatizo.

Nilimkopesha shemeji laki moja akaniahidi atanirudishia baada ya wiki.
Sikuishia hapo, nili mpigia mkewake simu nikimuazima laki moja
nimrudishie baada ya wiki, bila tatizo, akanipatia.

They are very happy family!!!!!!!
 
Kamusi na mwenza wake wanafanya maigizo.

Hawako kwenye ndoa hao.

Kufichana kwenye ndoa hakuhusiki hata kidogo.
yaani wapo pamoja kitandani tu ,baada ya hapo kila mtu kimpango wake...hana tofauti na mimi
 
Ndiyo BADILI TABIA,

Ila ni sawa kweli jamaa akakope kwa mtu ambaye yuko karibu na mke wake??

Bado hapa kuna katatizo hata kama hatujui tatizo lenyewe ni lipi!!

Babu DC!!

Dark City,
wapo wytu wa namna hiyo, hushangaza ila ndivyo walivyo, wanaona kukopa kwa mke ni kama kuonyesha udhaifu fulani, hivyo asilani hawakubali.....

kamusi nimekupenda bure,
si kwa style yako ya maisha bali kwa kusimama mwenyewe na kuinvest, inasikitisha kuona mwanaume anakuachia ada makusudi akidhani utarudi nyuma lakini ukweli hizo mali zitawanufaisha wote na watoto pia, naamini ndani ya moyo wake ataona umuhimu wake.....

Back to Dark City,
unajua wanaume mna udhaifu wa kuficha mali zenu?
Nimeona familia iliyosambaratika, watoto wameambulia nyumba moja tu aliyojenga mama yao, majumba na pesa za baba yao hawajapata hata ndururu kutokana tu na tabia ya mume kuficha mali, mali zote aliwapa ndugu wamtunzie alipokufa mke na watoto walidhurumiwa.....
 
Last edited by a moderator:
duuuh nimeamini kuna watu wabinafsi
hivi ndoa ni nini?@Kamusi

ndoa ni maelewano kati ya wa2 wawili, sasa km mmoja haonyeshi ushirikiano unataka huyo mwingine afanyaje?

kwa kweli issue za finance ni wa2 wachache sn wanasema kweli katika ndoa, wengi hawasemi kweli..(hasa wanaume)

na wakati mwingine inabidi tukubali kutokukubaliana, ili maisha yaendelee, otherwise itakuwa kila siku ni migongano isiyokwisha

nikwambie ukweli tu ndugu yangu, kwa sasa familia yangu imekuwa na amani(ilikuwa kila siku tunakalishana vikao na mr na kugombana kuhusu tabia yake hii) lkn nilipoamua kubadilika na kumuacha aniambie analotaka na asiloniambia simuulizi(ila nami nafanya yangu) basi tunaishi vizuri, what else should i do?
 
Ni kweli huwezi ku share na mtu msiri. Ila si lazima uwe na wewe msiri...ila siku m-suprise jinsi ulivyojijenga...utaona kama hatafuti kupinga urafiki. Afu mtolee nje mwambie nilitaka tu uwe informed...ila kwa tabia yako endeleea kutafuta kivyako vyako na mimi kivyangu vyangu.


Mimi nina hasira mbaya mbona hata akisusa kutoa ela ya matumizi ndani kama ninayo wala mshipa wa roho haustuki...atakomaje??? Atakuwa anakuta tu nimeroast mpaka mwenyewe aone ugwadu kula. Unamlisha kuanzia yeye mpaka watoto.Lol.
Una assume huna mume.

ndoa ni maelewano kati ya wa2 wawili, sasa km mmoja haonyeshi ushirikiano unataka huyo mwingine afanyaje?

kwa kweli issue za finance ni wa2 wachache sn wanasema kweli katika ndoa, wengi hawasemi kweli..(hasa wanaume)

na wakati mwingine inabidi tukubali kutokukubaliana, ili maisha yaendelee, otherwise itakuwa kila siku ni migongano isiyokwisha

nikwambie ukweli tu ndugu yangu, kwa sasa familia yangu imekuwa na amani(ilikuwa kila siku tunakalishana vikao na mr na kugombana kuhusu tabia yake hii) lkn nilipoamua kubadilika na kumuacha aniambie analotaka na asiloniambia simuulizi(ila nami nafanya yangu) basi tunaishi vizuri, what else should i do?
 
mie nimeolewa kwa zaidi ya miaka 10. mwanzoni nilikuwa mkweli sana kuhusu financial zangu kwa mume wangu..yani kila ninachokipata namwambia halafu tunajadili cha kufanyia..niliamini na mwenzangu yuko hivyo, lkn baadae nikaja kugundua kuwa haniambii ukweli kuhusu kipato chake(baada ya kugundua asset zake ambazo alinificha) na mambo kadhaa ambayo aliyafanya bila kunishirikisha..tuliongea ili tuyamalize na kila mmoja wetu asimfiche mwenzie, aliomba msamaha na akaahidi kujirekebisha lkn hajajirekebisha..kila mara nimekuwa nikigundua/nikiambiwa mambo anayofanya kimya kimya.. nikimuuliza amekuwa akitahayari tu hana la kusema..nikasema hakuna haja ya kugombana kwa sbb ya kipato cha mtu, nami si ninacho cha kwangu?...nami nikawa naficha kipato changu, simwambii na wala hajui nina shilingi ngapi..nimefungua account bank nyingine naweka huko akiba na wala hajui(ile bank anayojua anayo na password na yuko free akitaka hela nampa kadi).. nimejenga nyumba 1, hajui na sasa nategemea kujenga nyingine(sitegemei kumwambia vile vile).. matumizi ya nyumbani nachangia km kawaida tena mara kibao namkopesha kwani mwenzangu hajui bajeti mara kwa mara anaishiwa hata ya mafuta(anaamua kupanda daladala)..
kwa hivo tatizo ni nyie wanaume sio wakweli..wanawake ni wakweli pale mnapowashirikisha na wanajua bajeti..ni mara chache sn utakuta mwanamke kaishiwa hadi nauli
Nimeipenda post yako ila imenitia uchungu...kifupi kwenye ndoa wanaume ndio tatizo sana.!
 
Nimeipenda post yako ila imenitia uchungu...kifupi kwenye ndoa wanaume ndio tatizo sana.!


Hiyo conclusion yako umeitoa wapi?

Usiombe usikie story za wanaume wanaoteseka kwenye ndoa...Bahati nzuri wanaume huwa hawasemi yanayowakuta!

Babu DC!!
 
Back
Top Bottom