Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Hussein Kauli (Mwananchi)
CHAMA Cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu(THTU) kimesema hakiungi mkono mgomo uliotangazwa na Shirikisho la Vyma vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwa madai kuwa kinaangalia maslahi ya taifa.
Katibu mkuu wa chama hicho, Kulu Maswanya alisema kuwa kuwa nia ya Tucta ni kupata sulahu ya matatizo sugu yanayowakabili, lakinin akaongeza kuwa njia bora ni majadiliano ya kina yatakayofanya upembuzi yakinifu.
Maswanya alisema silaha ya mgomo itakuwa na maana tu iwapo majadiliano hayo yatakayowezesha kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu, hayatafikia malengo.
Naye mwenyekiti wa chama hicho, Dk Elifuraha Mtalo alisema wameamua kutounga mkono mgomo ulioitishwa na Tucta kwa kuwa hawakushirikishwa katika kuupanga.
Alishangazwa na uamuzi wa mgomo huo uliopangwa kuanza Mei 5 mwaka huu kwa kuwa Tucta imekuwa ikishirikishwa kwenye vyombo vya maamuzi na serikali na kuleta matunda kwa wafanyakazi, ikiwemo kuundwa kwa bodi ya mishahara.
“Hali hii ya ushiriki wa Tucta katika vyombo vya maamuzi na nia ya TUCTA kuandaa mgomo inaashiria kuwa kuna tatizo la msingi; ama la mfumo wa ushirikishwaji wa wafanyakazi au ushiriki dhaifu wa TUCTA katika vyombo vya maamuzi,†alisema Maswanya.
Alisema kama tatizo ni mfumo, vyama vya wafanyakazi viwe tayari kukataa mfumo huo kwa dhamira ya wazi kwa kujiondoa kwenye vyombo vya maamuzi ili kutoa fundisho kwa serikali.
"Iwapo tatizo ni udhaifu wa ushiriki wa vyama katika vyombo hivyo, ni vyema vyama vijitathmini upya ili kuwa na ushiriki bora utakaoleta tija kwa wafanyakazi,"alisema Maswanya.
Maswanya alisema pamoja na kufikia maamuzi hayo, anakubali kuwa matatizo yaliyotolewa na Tucta ni ya msingi na yanagusa maslahi ya wafanyakazi wote na pia ni ya muda mrefu.
My Take:
yaani.. wasomi wenyewe ndio wanapata shida ya kujua kama wagome.. sitoshangaa maprofesa wa vyuo vikuu wakiandamana kuunga mkono serikali!
CHAMA Cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu(THTU) kimesema hakiungi mkono mgomo uliotangazwa na Shirikisho la Vyma vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwa madai kuwa kinaangalia maslahi ya taifa.
Katibu mkuu wa chama hicho, Kulu Maswanya alisema kuwa kuwa nia ya Tucta ni kupata sulahu ya matatizo sugu yanayowakabili, lakinin akaongeza kuwa njia bora ni majadiliano ya kina yatakayofanya upembuzi yakinifu.
Maswanya alisema silaha ya mgomo itakuwa na maana tu iwapo majadiliano hayo yatakayowezesha kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu, hayatafikia malengo.
Naye mwenyekiti wa chama hicho, Dk Elifuraha Mtalo alisema wameamua kutounga mkono mgomo ulioitishwa na Tucta kwa kuwa hawakushirikishwa katika kuupanga.
Alishangazwa na uamuzi wa mgomo huo uliopangwa kuanza Mei 5 mwaka huu kwa kuwa Tucta imekuwa ikishirikishwa kwenye vyombo vya maamuzi na serikali na kuleta matunda kwa wafanyakazi, ikiwemo kuundwa kwa bodi ya mishahara.
“Hali hii ya ushiriki wa Tucta katika vyombo vya maamuzi na nia ya TUCTA kuandaa mgomo inaashiria kuwa kuna tatizo la msingi; ama la mfumo wa ushirikishwaji wa wafanyakazi au ushiriki dhaifu wa TUCTA katika vyombo vya maamuzi,†alisema Maswanya.
Alisema kama tatizo ni mfumo, vyama vya wafanyakazi viwe tayari kukataa mfumo huo kwa dhamira ya wazi kwa kujiondoa kwenye vyombo vya maamuzi ili kutoa fundisho kwa serikali.
"Iwapo tatizo ni udhaifu wa ushiriki wa vyama katika vyombo hivyo, ni vyema vyama vijitathmini upya ili kuwa na ushiriki bora utakaoleta tija kwa wafanyakazi,"alisema Maswanya.
Maswanya alisema pamoja na kufikia maamuzi hayo, anakubali kuwa matatizo yaliyotolewa na Tucta ni ya msingi na yanagusa maslahi ya wafanyakazi wote na pia ni ya muda mrefu.
My Take:
yaani.. wasomi wenyewe ndio wanapata shida ya kujua kama wagome.. sitoshangaa maprofesa wa vyuo vikuu wakiandamana kuunga mkono serikali!