Mjumbe wa Kamati kuu CDM na mbunge wa Moshi mjini Philemon Ndesamburo amezindua mfuko maalum wa kuwasaidia wanachama na viongozi wa chama hicho wanaobambikiwa na kufunguliwa kesi kila mahali ili kuwakatisha tamaa.
Ndesamburo ametaja kesi kadhaa zinazowaandama wanachama wake kama za maandamano ya Arusha na kesi polisi wanayoiandaa kumbambikia Mbunge Nassari.
Ndesamburo alitoa tamko hilo wakati akizindua tawi jipya la CDM mjini Moshi na kukabidhi kadi zaidi ya 50 kwa wanachama waliohama CCM na kujiunga CDM katika operesheni maalum ya Vua Gamba Vaa Gwanda.
SOURCE:ITV HABARI
Ndesamburo ametaja kesi kadhaa zinazowaandama wanachama wake kama za maandamano ya Arusha na kesi polisi wanayoiandaa kumbambikia Mbunge Nassari.
Ndesamburo alitoa tamko hilo wakati akizindua tawi jipya la CDM mjini Moshi na kukabidhi kadi zaidi ya 50 kwa wanachama waliohama CCM na kujiunga CDM katika operesheni maalum ya Vua Gamba Vaa Gwanda.
SOURCE:ITV HABARI