Ndesamburo anunua helkopta za kampeni Chadema

lakini ujumbe si niliufikisha mkuu
kama tunataka kuweka upinzani uwe strong lazima tukosoe nao wanapokosea ili wanaojiita CCM wasiwe napakukimbilia

Hakuna aliyekukataza kupinga au kukosoa upinzani (btw -- wanakosolewa sana hapa). Tatizo ni pale unapolazimisha watu kuandika kile unachotaka wewe (wakati huo huo ukitoa madai ya uongo kuwa upinzani haukosolewi hapa JF).
 
vyama vyote vya siasa duniani vina wafadhili wake, na ndio wafadhali wakubwa wana sauti zaidi kwenye vyama hivyo na huzawadiwa nafasi mbalimbali tena kwa uwazi. Lakini kwenye nchi za kidemokrasia mfadhili ni lazima awe yule ambaye hana tuhuma za ufisadi au uvunjaji wa sheria au kuhusishwa na mambo yaliyo kinyume. Ndio maana kwenye nchi kama Marekani mfadhili akigundulika kuwa si "msafi" mgombea au kiongozi hulazimika kurudisha ufadhili wake!

Nadhani ni lazima pia awe mwamanchi anaetambuliwa kikatiba kuwa ni mwananchi wa nchi siyo jitu kutoka nje sijui Iran, Pakistan anakuja kuwa mfadhili wa chama!
 
*Zitaanza uchaguzi wa serikali za mitaa

Boniface Meena, Moshi

MBUNGE wa Moshi Mjini,Philemon Ndesamburo(Chadema), amenunua helkopta mbili kwa ajili ya kukisaidia chama hicho katika kampeni za chaguzi mbalimbali hapa nchini.

Moja ya helkopta hizo tayari iko hapa nchini na nyingine itawasili Jumatatu (kesho) na tayari mbunge huyo ameshapata vibali vya kuziruhusu helkopta hizo kutumika hapa nchini.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Ndesamburo alikiri kuwa amenunua helkopta hizo, ili kukipunguzia chama chao gharama kubwa za kukodi wakati wa kampeni.

Hatua hiyo ni kubwa zaidi kwa Chadema, chama ambacho kimekuwa kikijitahidi kujiimarisha na kuongeza nguvu hasa wakati wa uchaguzi.

Tangu mwaka 2005 wakati wa Uchaguzi Mkuu, Freeman Mbowe alipogombea urais kwa mara ya kwanza, chama hicho kilitumia helkopta ya kukodi.

Hata katika baadhi ya chaguzi ndogo za ubunge zikiwemo za jimbo la Busanda na Tarime, chama hicho kilitumia helkopta za kukodi kwa ajili ya kufanyia kampeni.

Lakini safari hii, chama hicho kimeamua kumiliki helkopta yake huku Ndesamburo akisisitiza: "Vibali vyote nimeshapata kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga na vile vile vya kuitoa hiyo moja Nairobi na kuifikisha hapa Jumatatu".

Alisema kuwa helkopta hizo zitaanza kufanya kazi katika kampeni za serikali za mitaa katika majimbo yote ya Mkoa wa Kilimanjaro na baadaye katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana ni kuwa Chadema imesimamisha wagombea zaidi ya robo tatu katika kila jimbo mkoani Kilimanjaro.

Katika Jimbo la Moshi Mjini, chama hicho kimesimamisha wagombea 60Â na Jimbo la Rombo kimesimamisha wagombea 52.

Uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo huku idadi ya wapigakura ikiwa ndogo kinyume na matarajio.

Hali hiyo imesababisha baadhi ya vyama kujipanga kikamilifu ili kuhakikisha wanakwepa kile wanachoita hujuma dhidi ya CCM.

Uchaguzi huo ni muhimu kwa vyama vya siasa kujipatia mtaji na kujiimarisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ambao unatarajiwa kuwa na mchuano mkali.

Viongozi wa serikali za mitaa wana nguvu na ushawishi mkubwa wa kimaamuzi katika uchaguzi mkuu wa wabunge na Rais, kwani wapigakura wengi wako kwenye maeneo yao. Pia ngazi ya uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu katika maamuzi ya maendeleo ya nchi kutokana na watu wengi kuishi vijijini ambako pamoja na mambo mengine kuna shughuli nyingi muhimu za uchumi hasa kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa taifa.


Wamechoka kukodisha?
hongera sana CHADEMA!
 
kwani CHADENA ikisaidia albino ni NGO?
CCM wameshafulia wametulia hela zetu tunataka kuona vyama vya upinzani vitumie pesa kwa utaratibu mzuri.

Watumie pesa zipi na za nani? Ndesa kanunulia hela zake helkopta, sio za walipa kodi wala si za wanachama kama ccm walivyofanya. Kwa hiyo huna haki ya kumhoji. Ukiwakabidhi nchi ndio uhoji matumizi ya hela ya serikali.
 
Kwa taarifa yako wabunge wa kuchaguliwa wa CHADEMA ni mmoja tu ambaye ni mchagga - Ndesamburo. Arfi anatoka Mpanda, Mwera anatoka Tarime, Zitto anatoka Kigoma na Slaa anatoka Karatu. Kwa viti maalum - Halima Mdee sio mchaga, ni Mpare na Mama Maulidah Komu alikuwa mgombea mwenza kwa tiketi ya urais 2005. Hivi mpaka leo bado hujui kuwa mgombea mwenza lazima awe anatoka visiwani? Au utasema Tume ya uchaguzi iliipendelea CHADEMA?
.

Thanks Mkuu, watu wanakurupuka bila data.
Kwa ufafanuzi uliotoa sioni hiyo hoja ya Chadema na wachagga inatoka wapi. Au wana maana Mbowe kuwa Mwenyekiti ndio kuifanya chadema ya wachaga?
 
Wamejitahidi inaonyesha wana mipango endelevu ingewezakana wangepata nyingine kama nne hivi ili wawafike wengi huko vijijini ambao wanafikiri mwalimu Nyerere bado yuko hai na kwa hiyo imani yao chama chake cha CCM ndio mtawala halisi
 
Mzee Ndesa si fisadi.
Welcome to JF Semenya naona umejiunga juzi juzi tu.

Jasusi,
Hapa naona umechemsha. Kujiunga juzi juzi kwa Semenya kuna uhusiano gani na hoja yake? Let the guy empty his brain in the forum where we dare to talk. After all, how do you know that Mzee Ndesa is clean? How many TZ businessmen are clean?
 
Unless Mzee Ndesamburo amezinunua hizi kopta kwa uamuzi binafsi, otherwise huu utakuwa ni utumiaji mbaya wa pesa. Je baada ya uchaguzi zitauzwa au atazi-paki?

Natumaini huu uamuzi ulikuwa ni wa Mzee Ndesamburo peke yake na sio wa chama, maana kwa chama huu utakuwa ni ufujaji mkubwa wa pesa.

Huwezi kununua limo kwa ajili ya harusi ya week end moja, unless ziwe zinakuwasha.
 
Unless Mzee Ndesamburo amezinunua hizi kopta kwa uamuzi binafsi, otherwise huu utakuwa ni utumiaji mbaya wa pesa. Je baada ya uchaguzi zitauzwa au atazi-paki?

Natumaini huu uamuzi ulikuwa ni wa Mzee Ndesamburo peke yake na sio wa chama, maana kwa chama huu utakuwa ni ufujaji mkubwa wa pesa.

Huwezi kununua limo kwa ajili ya harusi ya week end moja, unless ziwe zinakuwasha.

Huwezi kulinganisha helikopta na limo linganisha helikopta na Fuso. Helikopta ni chombo cha kazi sio cha starehe. Kwa mantiki hiyohiyo ya kutumia helikopta wakati wa uchaguzi unaweza kuitumia kujenga chama baada ya uchaguzi. Hata hivyo kuna demand kubwa ya helikopta nchini na Ndesamburo ameliona hilo. Ni biashara nzuri na sio sahihi kusema ni utumiaji mbaya wa pesa.


.
 
Unless Mzee Ndesamburo amezinunua hizi kopta kwa uamuzi binafsi, otherwise huu utakuwa ni utumiaji mbaya wa pesa. Je baada ya uchaguzi zitauzwa au atazi-paki?

Natumaini huu uamuzi ulikuwa ni wa Mzee Ndesamburo peke yake na sio wa chama, maana kwa chama huu utakuwa ni ufujaji mkubwa wa pesa.

Huwezi kununua limo kwa ajili ya harusi ya week end moja, unless ziwe zinakuwasha.

Mkuu Makaayamawe sijakuelewa unamaanisha nini
Yaani pesa zake (Ndesamburo) kaamua kuzitumia tatizo liko wapi?
 
Huwezi kulinganisha helikopta na limo linganisha helikopta na Fuso. Helikopta ni chombo cha kazi sio cha starehe. Kwa mantiki hiyohiyo ya kutumia helikopta wakati wa uchaguzi unaweza kuitumia kujenga chama baada ya uchaguzi. Hata hivyo kuna demand kubwa ya helikopta nchini na Ndesamburo ameliona hilo. Ni biashara nzuri na sio sahihi kusema ni utumiaji mbaya wa pesa.


.

Mkuu Nyumbu,
Iwe ni Limo au Fuso, itakuwa ni biashara kichaa kuyanunua kama kazi yake ni ya siku chache tu. Ndio maana nimesema kama Ndesamburo amekinunulia chama hizo kopta baada ya kujadiliana na uongozi wa chama juu ya nini awasaidie, basi amekosea kwani hiyo pesa ingeweza kutumika vema zaidi.

Lakini kama kopta ni zake binafsi na atakiazima tu chama, basi amefanya la maana. Jinsi atakavyozitumia baada ya uchaguzi ni juu yake.
 
Mkuu Makaayamawe sijakuelewa unamaanisha nini
Yaani pesa zake (Ndesamburo) kaamua kuzitumia tatizo liko wapi?

Mkuu MwalimuZ,
Kama kopta ni zake binafsi na anakiazima tu chama, basi hiyo haina shida maana ni mali binafsi. Tatizo ni kama amekinunulia chama, wakati chama kinahitaji pesa ili kukipanua vijijini.
 
Mkuu MwalimuZ,
Kama kopta ni zake binafsi na anakiazima tu chama, basi hiyo haina shida maana ni mali binafsi. Tatizo ni kama amekinunulia chama, wakati chama kinahitaji pesa ili kukipanua vijijini.

Nakubaliana na wewe,sijui viongozi wa Chadema wanatoka sayari gani, kukua kwa chama kunategemea ufikaji ujumbe kila kona ya nchi kwa kutumia baisikeli,pikipiki na labda magari.Kuruka kwa helikopta wakati wa uchaguzi na kuwatimulia wananchi vumbi nyingi kamwe hautafanikisha kukiendeleza chama na kuwashawishi kukipigia kura.
 
Nakubaliana na wewe,sijui viongozi wa Chadema wanatoka sayari gani, kukua kwa chama kunategemea ufikaji ujumbe kila kona ya nchi kwa kutumia baisikeli,pikipiki na labda magari.Kuruka kwa helikopta wakati wa uchaguzi na kuwatimulia wananchi vumbi nyingi kamwe hautafanikisha kukiendeleza chama na kuwashawishi kukipigia kura.

Mhh, kweli?
 
.... kukua kwa chama kunategemea ufikaji ujumbe kila kona ya nchi.....

Nakubaliana na wewe hapo na hiyo ndio sababu CHADEMA inatumia helikopta. Kwanza, Watu wa vijijini wanashawishika zaidi kwa kuwasikiliza viongozi wa kitaifa sio walewale viongozi waliowazoea. Ukimpeleka kwa baiskeli au pikipiki hawatamsikiliza, watampuuza. Ndivyo Watanzania tulivyo. Lazima aende kwa gari. Helikopta inafika kwa urahisi zaidi na inafika sehemu ambazo gari haifiki. Pili, Kwenye kijiji cha watu elfu moja ukienda na baiskeli, pikipiki au gari hata utangaze mkutano namna gani hutapata watu zaidi ya mia lakini ukienda na helikopta unapata zaidi ya watu mia tisa. Wataishangaa helikopta kwa dakika kumi halafu wataanza kujiuliza huyo aliyekuja nayo ni nani na anatafuta nini? Watakusikiliza. Kwa wiki mbili zijazo kijiji kizima kitakuwa kinaongelea ujio wako tu! Ukicheza karata zako vizuri Ujumbe unafika KISAWASAWA.

.
 
Wamefanya vizuri sana kwa ajili ya hilo maana kuna ulazima sana katika kujua mambo na kujitayarisha kwa ajili ya mwakani
 
Back
Top Bottom