Ndesamburo achemka, out of touch!

Buyaka

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
1,643
1,786
Ni pale aliposema bungeni kwamba, viongozi wakitaka kujua hali halisi ya maisha ya Watanzania basi wapite na helikopta wataona kwa karibu, kwa mfano kuna watu mpaka leo hii wanaishi maporini, hawajulikani ni kina nani, na ukipita na gari au ndege huwezi kuwaona, na si vizuri kuwaacha nyuma wengine kimaendeleo, ni lazima tuendelee kwa pamoja.

Ulikuwa ni kama mpira wa kona alivyoshukiwa na mbunge wa CCM na washangiliaji, au niseme gombania goli , kipa mmoja washambuliaji kibaaao!


Wabunge wa CCM wakamuuliza Mheshimiwa Ndesamburo, nyinyi CHADEMA si mnafagilia kupunguza gharama za serikali kwa viongozi kutumia vyombo vya usafiri vya nafuu, sasa gari na helikopta kipi aghali? CCM wakadai kwamba kwa kweli hakuna chama mbadala kama wabunge wenyewe wa CHADEMA ndio wana mawazo hayo.

Lakini hata hivyo kuna hoja za maana alizotoa, kama alivyomlipua Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kwamba ni failure lakini amongezewa muda baada ya umri wa kustaafu kufika, kinyume na sheria. Alimtaka aondolewe haraka wa sababu ni mzee na hana utaalam maalum unaohalalisha kumuongezea muda kama sheria inavyotaka.
 
Vijana mtatupa shida sana nyie! Ukiwa kwenye gari unafikiri unaweza kuona walao km 1 from main road. Yaani CCM wanaona uzuri wa uso wanafikiri hata kifuani na sehemu zilizofunikwa na nguo ni nzuri vivyo hivyo! Helicopter hukuwezesha kufika pale ambapo hayo ma kilimo kwanza hayawezi kufika. Ngoja tuone kama kuna likilimo kwanza litakalofanyiwa service ya shilingi laki tano baada ya kumilikishwa hayo magari! Nakwambia nguo za ndani zitawabana!
 
Hao wabunge wa CCM wanaendeshwa na unafiki, kwani helkopta ngapi. kwani sasa kuna V8 ngapi, Kipi kitasaidia wananchi walio wangi. Vichwa vya nazi. Nashukuru mimi sio mbunge ningekuwa napigwa ban kila siku.
 
wabunge wa CCM waache upotoshaji;hoja ya desamburo ni ya msingi kuna mahala tanzania ambako hakufikiki kwa barabara.kuna sehemu nyingi tu naushahidi vipo vijiji hata kilosa mkurugenzi wa halmashauri hajawahili kufika .Hivyo dhana ya sesa pesa ni serkali kungalia nmna ya kufikia vijiji ambavyo havifikiki kirahisi kwa usafiri wa kawaida.Mkumba aache upotoshwaji hao ndo wakuondolewa uchanguzi unaokuja , sababu ya kuwa na upeo mfupi wa kuelewa.
 
Ni pale aliposema bungeni kwamba, viongozi wakitaka kujua hali halisi ya maisha ya Watanzania basi wapite na helikopta wataona kwa karibu, kwa mfano kuna watu mpaka leo hii wanaishi maporini, hawajulikani ni kina nani, na ukipita na gari au ndege huwezi kuwaona, na si vizuri kuwaacha nyuma wengine kimaendeleo, ni lazima tuendelee kwa pamoja.

Ulikuwa ni kama mpira wa kona alivyoshukiwa na mbunge wa CCM na washangiliaji, au niseme gombania goli , kipa mmoja washambuliaji kibaaao!


Wabunge wa CCM wakamuuliza Mheshimiwa Ndesamburo, nyinyi CHADEMA si mnafagilia kupunguza gharama za serikali kwa viongozi kutumia vyombo vya usafiri vya nafuu, sasa gari na helikopta kipi aghali? CCM wakadai kwamba kwa kweli hakuna chama mbadala kama wabunge wenyewe wa CHADEMA ndio wana mawazo hayo.

Lakini hata hivyo kuna hoja za maana alizotoa, kama alivyomlipua Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kwamba ni failure lakini amongezewa muda baada ya umri wa kustaafu kufika, kinyume na sheria. Alimtaka aondolewe haraka wa sababu ni mzee na hana utaalam maalum unaohalalisha kumuongezea muda kama sheria inavyotaka.

Helicopter inatumiwa kipindi kifupi sana cha chaguzi
katika matumizi nitapingana kama kuna waliovalia njuga hili.
Tunaona matumizi mabovu kila siku safari za viongozi haziishi ndani na hata nje ya nchi. Hata vikao vyakawaida vya chama wanakodi ndege kwa garama kubwa. Ukifatilia sana ufujaji wa pesa za umma achilia mbali pesa tunazoibiwa kwenye mikataba unaweza kuanza kuteseka na magonjwa ya moyo sasa hivi
 
Kama kawa wabunge wa magamba lazima wahache hoja ya msingi
na kujikita kwenye mambo yasiyo na maana sana..yote kupotosha umma!
Kila bidhaa ina expiry date, ccm imekwisha ku expire tunasubiria muda
ufike tuipeleke dampo!
 
Hata ramani za mipango miji siku hizi tuwe tunapiga kwa gari?
 
gari lina nafasi yk na helcopter ina nafasi yake, ni swala la uelewa tu
Ukweli ccm wajinga tu! Kuna maeneo mengi sana nchi hïi gari haiwezi kufika kilahisi na kwa haraka, kwanini wasitumie ukizingatia mda ni gharama sana, masikini magamba hawaoni hili!
 
Achen ushamba nyie dhaifu, hiv maufisadi mnayofanya hamuon km mna weza kununua hata elkopita 50. Mmeuza machimbo kwa wazungu, mnauza wanyama kila siku nje hizo pesa mnapeleka wapi?. Halafu leo mnamshangaa ndesambulo anapoongelea helkopita.
 
Nafikir. We ndo umechemka...aliposema watumie Helicopter sio maana,Viongozi wa Serikali,Mkuu wa Wilaya,Mkuu wa Mkoa,RCO,Mkurugenzi wa. Manispaa na watendaji wengine woote wanunuliwe Helicopter.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
kwanza helikopta ni ya ndesa sasa ushabiki wa nini?

Mzee Ndesa ni mkweli kwa nafsi yake! Honest to his own self! Yeye husafiri kwa helikopta kwenda mjengoni, anaona mengi na amesema. Sasa badala ya kumsikiliza wanaanza kumwangalia amevaa nguo gani. Udhaifu mkubwa huu.

Ujumbe ni dhahiri kabisa, kuna umasikini wa kutisha! Ameona na ametuambia tusiangalie tu barabarani kuna watu wetu wako maporini. Lkini angalia mitizamo ya kisiasa.

Hivi bei ya Helikopta na Shangingi- ni nani atatusaidia kulinganisha? Maana serikali ingekuwa na Helikopta kila Mkoa, hata majanga mengi tungeweza kusaidia. Lakini leo hii kuna ajali highway, mpaka ipatikane njia mbadala ya kumkimbiza majeruhi ni shughuli! (NAJUA NIMECHANGANYA MBOGA HAPA, LAKINI USHABIKI WA KISIASA UNAFILISI HOJA HARAKA MNO, NA NAONA KARIBU NAAMBUKIZWA HUU UGONJWA)
 
Hakuchemka ni sawa kwani alikwisha fanya utafifi wa kutosha katika hili,nafikili tumfuate hatutanabaishe vema hoja yake.
 
Ni pale aliposema bungeni kwamba, viongozi wakitaka kujua hali halisi ya maisha ya Watanzania basi wapite na helikopta wataona kwa karibu, kwa mfano kuna watu mpaka leo hii wanaishi maporini, hawajulikani ni kina nani, na ukipita na gari au ndege huwezi kuwaona, na si vizuri kuwaacha nyuma wengine kimaendeleo, ni lazima tuendelee kwa pamoja.

Ulikuwa ni kama mpira wa kona alivyoshukiwa na mbunge wa CCM na washangiliaji, au niseme gombania goli , kipa mmoja washambuliaji kibaaao!


Wabunge wa CCM wakamuuliza Mheshimiwa Ndesamburo, nyinyi CHADEMA si mnafagilia kupunguza gharama za serikali kwa viongozi kutumia vyombo vya usafiri vya nafuu, sasa gari na helikopta kipi aghali? CCM wakadai kwamba kwa kweli hakuna chama mbadala kama wabunge wenyewe wa CHADEMA ndio wana mawazo hayo.
Lakini hata hivyo kuna hoja za maana alizotoa, kama alivyomlipua Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kwamba ni failure lakini amongezewa muda baada ya umri wa kustaafu kufika, kinyume na sheria. Alimtaka aondolewe haraka wa sababu ni mzee na hana utaalam maalum unaohalalisha kumuongezea muda kama sheria inavyotaka.

Wewe mlete thread ndio umechemka, hujajishughulisha kufikilia hata sekunde moja, umebeba zima zima kuja kulibwaga hapa, next time usirudie, alaaaa
 
Ndo muone matamanio ya CDM ni kila kiongozi kuwa na helcopta yake zinazotumia umeme
 
Back
Top Bottom