Ndege za Tanzania na Africa si salama!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,605
8,744
Mimi kama Mtanzania na Mwafrica nimesikitishwa sana na kuridhika kwa viongozi wetu Africa na Tanzania kuhusu usalama wa ndege zinazotumiaka Africa. Ndege ya ATC imeanguka Kigoma lakini sijasikia Kiongozi yeyote kasema lolote hata Zitto ambaye ametokea Kigoma na mpinzania hajasema lolote!!. Sababu kubwa ni kwamba hakuna mtu aliyekufa lakini tumeona Nigeria, COngo na Tanzania ndege zinaanguka kila siku kwasababu Africa imekuwa jalala la ndege za zamani. Hii ni sababu mojawapo ya kupinga ATC kuwa ya serikali kwani serikali haiwezi kujichunguza yenyewe! je waliopata ajali wamelipwa nini? ndege ilikuwa ya mwaka gani, Nigeria mfano ndege ilikuwa ya miaka 22! kwanini wakati kisheria ndege inatakiwa kuwa na miaka 20 tu!. Je kama ndugu yako akiwa kwenye ndege ungefanyaje?. Je kuna sheria gani za kulipa waathirika au mpaka wafe?. Upinzani sasa unafanya nini ikiwa ndege zinaanguka halafu wanaona kama ni kawaida tu!
 
Hiyo inshu ya ndege ni sehemu tu ya uozo uliopo kwenye nchi zetu za kiafrika, kuna mambo ambayo ukielezwa unaweza ukaikana nchi yako hadi hapo utakapobadili uamuzi. Viongozi wetu sijui wamechakachuliwa akili au wanakuwa kama hawafuatilii jinsi mambo yanavyoenda kwenye mabara mengine! Kwa ufupi, vitengo mhimu kama usalama wa taifa, diplomasia pamoja na nyinginezo vinatakiwa viwe na smart people who will dedicate their lives for the nation siyo hawa F6 leavers wengi wao wachumia tumbo.
Hizo ndege huenda hakuna hata mawasiliano ya maana, na kama yapo zikiwa na tatizo kuna vitengo vya maana vilivyotayari kuokoa kama ikitoa vimepata taarifa kabla ya ndege haijaanguka achilia mbali basi na hiyo! je kuna professional people wanaoweza kuzikagua na kuziona kweli zinafaa kuingizwa au wizi wizi, ujanja ujanja? Kama wapo, huwezi kuta wanashirikishwa kuzikagua, utakuta wanapewa wahuni wenye kwenda training za miaka 2 au mwaka 1 anakuwa na certificate of aero --inspection which is not concrete.
Viongozi wetu hawataki challenges za kuzisaidia nchi zao, wanaongoza kwa kuiga. Wanajua ukiwa kiongozi kuna kujenga barabara, mahospitali, mashule na kuwapa misaada watu kama chakula nk kumbe ni zaidi ya hapo. We need visionarist people (leaders) ambao watasema "we must move from point A to point B" even if someone will die. Na baada ya point B then point C and so on. Kiufupi hakuna kipaumbele.
 
Back
Top Bottom