Mimi kama Mtanzania na Mwafrica nimesikitishwa sana na kuridhika kwa viongozi wetu Africa na Tanzania kuhusu usalama wa ndege zinazotumiaka Africa. Ndege ya ATC imeanguka Kigoma lakini sijasikia Kiongozi yeyote kasema lolote hata Zitto ambaye ametokea Kigoma na mpinzania hajasema lolote!!. Sababu kubwa ni kwamba hakuna mtu aliyekufa lakini tumeona Nigeria, COngo na Tanzania ndege zinaanguka kila siku kwasababu Africa imekuwa jalala la ndege za zamani. Hii ni sababu mojawapo ya kupinga ATC kuwa ya serikali kwani serikali haiwezi kujichunguza yenyewe! je waliopata ajali wamelipwa nini? ndege ilikuwa ya mwaka gani, Nigeria mfano ndege ilikuwa ya miaka 22! kwanini wakati kisheria ndege inatakiwa kuwa na miaka 20 tu!. Je kama ndugu yako akiwa kwenye ndege ungefanyaje?. Je kuna sheria gani za kulipa waathirika au mpaka wafe?. Upinzani sasa unafanya nini ikiwa ndege zinaanguka halafu wanaona kama ni kawaida tu!