Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,885
- 6,885
Kwa miaka kadhaa baada ya Gaddafi kuitungua ndege ya abiria ya Marekani PAN AM ambayo ilipita juu ya anga la Libya, hatimaye ndege hazikuwa huru kuvuka bahari ya kati, zimekuwa zikiambaa kupitia Palestina, Israel na kisha kuingia Ulaya. Sababu ni kumwogopa Gaddafi asijekutungua tena.
Nimeshuhudia siku hizi ninaposafiri ndege za abiria kukatisha anga la Libya na kuvuka bahari ya kati huku tukiangalia visiwa vya Malta, Sisilia hadi tunakuwa juu ya anga la Italia.
Gaddafi licha ya kuwafanyia mazuri Walibya, kimataifa alikuwa tishio na kukosa raha ndege zinapopita karibu na mipaka ya nchi yake.