Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
IKO NJE KWENYE MATENGENEZO, SERIKALI YAKWAMA KUILIPIA
na Mwandishi wetu
UKATA unaoikabili serikali, umesababisha kukwama kuilipia ndege maalumu ya Rais, inayofanyiwa matengenezo nje ya nchi, Tanzania Daima Jumatano limebaini. Kutokuwepo kwa ndege hiyo, kumesababisha Rais Jakaya Kikwete na ujumbe wake wa zaidi ya watu 14, ulioondoka nchini jana kwenda Davous, nchini Sweden, kuhudhuria mkutano wa dunia wa mambo ya uchumi, kuondoka na ndege ya Shirika la Ndege la Qatal. Habari ambazo gazeti hili imezipata, zilisema kuwa ndege ya Rais mahususi kwa ajili ya safari za aina hiyo imezuliwa nje ya nchi baada ya serikali kukwama kulipia gharama za matengenezo yake.
Kutokuwepo kwa ndege hiyo iliyonunuliwa kwa sh bilioni 40 na kuibua mzozo mkubwa wakati serikali ya awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, kunaelezwa kuwa kumeongeza gharama kubwa kwa ziara za Rais Kikwete ambaye amekuwa akitumia ndege za kawaida kwenye safari zake nje ya nchi. Habari kutoka ndani ya msafara wa Rais, zilisema kuwa zaidi ya sh milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya kugharimia ziara hiyo ya siku nne nchini Sweeden. Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema kuwa kiasi hicho cha fedha kinatumika ndani ya siku nne kuanzia Januari 25 hadi 29 ambapo Rais na ujumbe wake watakuwa wanahudhuria mkutano huo ambao wataalamu wa uchumi, wameuelezea kwamba hauna tija kwa taifa. Inaelezwa kuwa Rais Kikwete ameshahudhuria mikutano hiyo mara nyingi, lakini hakuna faida inayopatikana kitaifa baada ya serikali kushiriki katika mikutano hiyo inayoratibiwa na Wizara ya Fedha na Uchumi. Jana Rais Kikwete ameondoka, yeye na msafara wake watatumia zaidi ya sh milioni 300 kwa siku nne tu, atakazohudhuria mkutano wa uchumi, Davos nchini Sweeden. Angekuwa na ndege yake, gharama zingepungua, kilisema chanzo chetu cha habari. Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa kwa takriban miezi miwili sasa, ndege hiyo iko nje ya nchi ikifanyiwa matengenezo kutokana na kuwa na hitilafu.
Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Ndege za Serikali, Keenan Mhaiki, alikiri kuwa ndege hiyo iko nje kwa matengenezo, lakini alisema ni matengenezo ya kawaida yaliyomo ndani ya ratiba ya ndege hiyo ya kisasa. Ndege ya Rais iko kwenye matengenezo. Sio kwamba ni mbovu, hapana ni matengenezo ya kawaida ambayo yanachukua zaidi ya mwezi mmoja, alisema Mhaiki. Alipoulizwa kwamba ndege hiyo iko nje kwa muda mrefu baada ya serikali kukwama kulipa deni la matengezo yake, Mhaiki alikana na kuongeza kuwa hana taarifa za serikali kushindwa kulipia deni la matengenezo. Kwanza nikwambie tu kuwa ndege hiyo sio mbovu, lakini pia sisi hatuhusiki na malipo ya matengenezo yake, kwa kawaida ikishakuwa tayari tunapewa taarifa nasi tunaandaa utaratibu wa kuifuata, alisema.
Alipoulizwa kuhusiana na serikali kukwama kuikomboa ndege ya Rais, Waziri wa Uchukuzi, Omary Nundu, alijibu kwa kifupi kwamba hawezi kuulizwa swali hili kwenye simu. Alipotakiwa kufuatwa ofisini ili kutoa ufafanuzi, Waziri Ndundu alikuja juu na kusema yuko jimboni, hivyo waulizwe wasaidizi wake walioko Dar es Salaam. Mimi niko jimboni, pale ofisini kuna watendaji wa wizara. Mimi siyo wizara, nenda pale utapata majibu yote, alisema Waziri Ndundu
na Mwandishi wetu
Kutokuwepo kwa ndege hiyo iliyonunuliwa kwa sh bilioni 40 na kuibua mzozo mkubwa wakati serikali ya awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, kunaelezwa kuwa kumeongeza gharama kubwa kwa ziara za Rais Kikwete ambaye amekuwa akitumia ndege za kawaida kwenye safari zake nje ya nchi. Habari kutoka ndani ya msafara wa Rais, zilisema kuwa zaidi ya sh milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya kugharimia ziara hiyo ya siku nne nchini Sweeden. Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema kuwa kiasi hicho cha fedha kinatumika ndani ya siku nne kuanzia Januari 25 hadi 29 ambapo Rais na ujumbe wake watakuwa wanahudhuria mkutano huo ambao wataalamu wa uchumi, wameuelezea kwamba hauna tija kwa taifa. Inaelezwa kuwa Rais Kikwete ameshahudhuria mikutano hiyo mara nyingi, lakini hakuna faida inayopatikana kitaifa baada ya serikali kushiriki katika mikutano hiyo inayoratibiwa na Wizara ya Fedha na Uchumi. Jana Rais Kikwete ameondoka, yeye na msafara wake watatumia zaidi ya sh milioni 300 kwa siku nne tu, atakazohudhuria mkutano wa uchumi, Davos nchini Sweeden. Angekuwa na ndege yake, gharama zingepungua, kilisema chanzo chetu cha habari. Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa kwa takriban miezi miwili sasa, ndege hiyo iko nje ya nchi ikifanyiwa matengenezo kutokana na kuwa na hitilafu.
Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Ndege za Serikali, Keenan Mhaiki, alikiri kuwa ndege hiyo iko nje kwa matengenezo, lakini alisema ni matengenezo ya kawaida yaliyomo ndani ya ratiba ya ndege hiyo ya kisasa. Ndege ya Rais iko kwenye matengenezo. Sio kwamba ni mbovu, hapana ni matengenezo ya kawaida ambayo yanachukua zaidi ya mwezi mmoja, alisema Mhaiki. Alipoulizwa kwamba ndege hiyo iko nje kwa muda mrefu baada ya serikali kukwama kulipa deni la matengezo yake, Mhaiki alikana na kuongeza kuwa hana taarifa za serikali kushindwa kulipia deni la matengenezo. Kwanza nikwambie tu kuwa ndege hiyo sio mbovu, lakini pia sisi hatuhusiki na malipo ya matengenezo yake, kwa kawaida ikishakuwa tayari tunapewa taarifa nasi tunaandaa utaratibu wa kuifuata, alisema.
Alipoulizwa kuhusiana na serikali kukwama kuikomboa ndege ya Rais, Waziri wa Uchukuzi, Omary Nundu, alijibu kwa kifupi kwamba hawezi kuulizwa swali hili kwenye simu. Alipotakiwa kufuatwa ofisini ili kutoa ufafanuzi, Waziri Ndundu alikuja juu na kusema yuko jimboni, hivyo waulizwe wasaidizi wake walioko Dar es Salaam. Mimi niko jimboni, pale ofisini kuna watendaji wa wizara. Mimi siyo wizara, nenda pale utapata majibu yote, alisema Waziri Ndundu