Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Swali nawaulizeni, mabingwa wa kiswahili,
Wanazuoni jibuni, kwa kina kiso bahili,
Hoja zenu zipangeni, kwa vyema ilo ayali,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Ni ndege nimpendaye, kutwa yuko mawinguni,
Ndiye nimtafutaye, namsaka msituni,
Mtego niuandae, ninmase asilani,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Ala kulli hali, ndege nitamsifia,
Alhasir kauli, kwanini namsakia,
Naelezea amali, kwa jinsi namshakia,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Sekunde akishatua, fumba fumbua karuka,
Mtini akishatua, mbawaze zapeperuka,
Mtego keshagundua, adonoa kwa dhihaka,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Mtegoni hanasiki, machale yamemcheza,
Najiona mwenye dhiki, ndege nambembeleza,
Arijojo hashikikiki, wenzangu wananibeza,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Nilidhani nimenasa, kumbe amenizugia,
Kaniacha napepesa, ndege amenikimbia,
Wajuzi wenye kuasa, majibu nasubiria,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Na. M. M. Mwanakijiji
Sauti ya Kijiji
Wanazuoni jibuni, kwa kina kiso bahili,
Hoja zenu zipangeni, kwa vyema ilo ayali,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Ni ndege nimpendaye, kutwa yuko mawinguni,
Ndiye nimtafutaye, namsaka msituni,
Mtego niuandae, ninmase asilani,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Ala kulli hali, ndege nitamsifia,
Alhasir kauli, kwanini namsakia,
Naelezea amali, kwa jinsi namshakia,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Sekunde akishatua, fumba fumbua karuka,
Mtini akishatua, mbawaze zapeperuka,
Mtego keshagundua, adonoa kwa dhihaka,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Mtegoni hanasiki, machale yamemcheza,
Najiona mwenye dhiki, ndege nambembeleza,
Arijojo hashikikiki, wenzangu wananibeza,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Nilidhani nimenasa, kumbe amenizugia,
Kaniacha napepesa, ndege amenikimbia,
Wajuzi wenye kuasa, majibu nasubiria,
Ndege asiyetulia, huyo anategwa vipi?
Na. M. M. Mwanakijiji
Sauti ya Kijiji