GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Leo asubuhi nimemsikia Mbunge wa Sumve CCM Ricahrd Ndasa akithibitisha kuwa hataunga mkono hoja ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika endapo serikali haitapiga marufuku matumizi ya mzani wa Rula na kuidhinisha mzani wa Digital kutumika.
Ndassa aliyefuatana na Moses Machari wa Kasulu Mjini walikuwa katika Mahojiano na Kipindi cha Tuongee Asubuhi Star TV kilichokuwa kinaongozwa na Yahya Mohamed – Mwanza na Thom Chilala – Dodoma.
Katika hali inayoonekana kama ni kujichanganya kwa serikali, wabunge hao na wachangiaji wengine walihoji ukinyonga wa Wizara kwa kuahidi bei ya shilingi 1100 kwa kilo ya Pamba katika Mkutano wa nane wa wadau wa sekta ya pamba uliofanyika mwezi uliopita huko Mwanza na sasa kuidhinisha bei ya shilingi 800 kwa kilo.
Maswali magumu hapa ni:
Tunasubiri Mswaada huo utakapojadiliwa
ADIOS
Ndassa aliyefuatana na Moses Machari wa Kasulu Mjini walikuwa katika Mahojiano na Kipindi cha Tuongee Asubuhi Star TV kilichokuwa kinaongozwa na Yahya Mohamed – Mwanza na Thom Chilala – Dodoma.
Katika hali inayoonekana kama ni kujichanganya kwa serikali, wabunge hao na wachangiaji wengine walihoji ukinyonga wa Wizara kwa kuahidi bei ya shilingi 1100 kwa kilo ya Pamba katika Mkutano wa nane wa wadau wa sekta ya pamba uliofanyika mwezi uliopita huko Mwanza na sasa kuidhinisha bei ya shilingi 800 kwa kilo.
Maswali magumu hapa ni:
- Nani atawafidiwa wakulima hawa kwa pungufu la bei hii ambayo serikali ina jukumu la kusimamia soko la zao la Pamba.
- Lakini ugomvi ni hitajio la mizani 10,000 kusambazwa katika vituo vya kununulia pamba ambapo ni dhahiri hapa kuna mchezo mchafu wa Tenda na si ajabu tayari kuna bwana mkubwa kashaagiza mizani za rula ambazo zinampunja mkulima kwa asilimia 40 kwa kuwa kuna 10% hii itafumbiwa macho kama ilivyokuwa SPEED GOVERNOR.
- Ndassa atashikilia uamuzi wake au mchezo wa Milioni 50 kama zile za Jairo zitafanya kazi kumkata kauli na aishie kuunga hoja mkono kwa asilimia 100?
- Je aliyoyatamka moses Machali pia atayafanyia kazi kama alivyoahidi kumuunga mkono Ndassa au bahasha itafanya kazi?
Tunasubiri Mswaada huo utakapojadiliwa
ADIOS