Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Viongozi wa serikali, vyama vya siasa, wananchi, wanachama wa vyama mbalimbali kila mmoja amebaki anaduwaa na kila mmoja analaani kilichotokea Ndago.
Sio mara ya Kwanza mauaji na kuumizwa kwa wananchi kutokea kwenye mikusanyiko au harakati za siasa Tanzania mpaka sasa inaanza kuwa ni kama jambo la kawaida.
Igunga tulishuhudia wananchi wakiumizwa, wakiuwawa, Meru nako mauaji yamekuwa yakitokea kipindi cha harakati za siasa na watu kupoteza maisha eti kwa sababu watu wanataka kushinda uchaguzi.
Mimi moja kwa moja nawalaumu polisi, usalama wa taifa, DPP na viongozi wote wa serikali, hatuwezi kuendelea kuuwawa na kuteswa ili watu waendelee kufanya siasa vile watakavyo. Tangia vifo hivi vimeanza kutokea sijasikia aliyefungwa kwa kuuwa wananchi wasio na hatia na wale wote waliondaa vikundi vya kuleta fujo kurusha mawe, mishale, kutumia mapanga na risasi kwa sababu yeyote ile.
Singida inasadikika Mweka hazina wa CCM Mwigulu Nchemba yuko nyuma ya mauji wa kada ya chama chake baada ya kuwatumia vijana ili kuvuruga kwa makusudi mkutano wa CDM. Swali hapa ambalo linanikwaza je usalama wa Taifa walikuwa wapi mbinu hizi zikipangwa iwe ni kweli au ni kikundi kingine?? Je Polisi walikuwa wapi kulinda usalama ikizingatiwa wanahitajika kuwepo kila mikutano hii ikifanywa ili kulinda amani na kukamata wahalifu pamoja na hawa warusha mawe na kuuwa wananchi??
Kwa nini kila anapohusishwa Mwigulu watu wanakufa ?? Kila aliposhika mikoba ya CCM kusaidia kushinda wamekufa watu??? Je kwa nini uchunguzi usifanywe ili ijulikane na watu waache tabia ya kuhisiana ???
Nani kweli yuko nyuma ya mauji haya ya Singida??? Kweli Polisi na CCM hawajui??? Kweli CDM hawajui??? Kweli usalama wa Taifa hawajui???
Ninalaani kwa nguvu zangu zote kifo cha kada wa CCM na nina muomba Mungu yeyote aliyehusika kwa kushawishi, kulipa wananchi au vijana kuwapa vijana bangi, pombe ama kitu chochote au maneno yeyote ili walete fujo zilizozaa mauji haya aadhibiwe na hiyo siasa iwe mwisho wake.
Amani ya kweli na upendo havitajengwa kama tutaendelea kupandikza chuki baina ya jamii, Jirani kwa jirani nk.
Sio mara ya Kwanza mauaji na kuumizwa kwa wananchi kutokea kwenye mikusanyiko au harakati za siasa Tanzania mpaka sasa inaanza kuwa ni kama jambo la kawaida.
Igunga tulishuhudia wananchi wakiumizwa, wakiuwawa, Meru nako mauaji yamekuwa yakitokea kipindi cha harakati za siasa na watu kupoteza maisha eti kwa sababu watu wanataka kushinda uchaguzi.
Mimi moja kwa moja nawalaumu polisi, usalama wa taifa, DPP na viongozi wote wa serikali, hatuwezi kuendelea kuuwawa na kuteswa ili watu waendelee kufanya siasa vile watakavyo. Tangia vifo hivi vimeanza kutokea sijasikia aliyefungwa kwa kuuwa wananchi wasio na hatia na wale wote waliondaa vikundi vya kuleta fujo kurusha mawe, mishale, kutumia mapanga na risasi kwa sababu yeyote ile.
Singida inasadikika Mweka hazina wa CCM Mwigulu Nchemba yuko nyuma ya mauji wa kada ya chama chake baada ya kuwatumia vijana ili kuvuruga kwa makusudi mkutano wa CDM. Swali hapa ambalo linanikwaza je usalama wa Taifa walikuwa wapi mbinu hizi zikipangwa iwe ni kweli au ni kikundi kingine?? Je Polisi walikuwa wapi kulinda usalama ikizingatiwa wanahitajika kuwepo kila mikutano hii ikifanywa ili kulinda amani na kukamata wahalifu pamoja na hawa warusha mawe na kuuwa wananchi??
Kwa nini kila anapohusishwa Mwigulu watu wanakufa ?? Kila aliposhika mikoba ya CCM kusaidia kushinda wamekufa watu??? Je kwa nini uchunguzi usifanywe ili ijulikane na watu waache tabia ya kuhisiana ???
Nani kweli yuko nyuma ya mauji haya ya Singida??? Kweli Polisi na CCM hawajui??? Kweli CDM hawajui??? Kweli usalama wa Taifa hawajui???
Ninalaani kwa nguvu zangu zote kifo cha kada wa CCM na nina muomba Mungu yeyote aliyehusika kwa kushawishi, kulipa wananchi au vijana kuwapa vijana bangi, pombe ama kitu chochote au maneno yeyote ili walete fujo zilizozaa mauji haya aadhibiwe na hiyo siasa iwe mwisho wake.
Amani ya kweli na upendo havitajengwa kama tutaendelea kupandikza chuki baina ya jamii, Jirani kwa jirani nk.