Nchi ya watu wa kulalamika,yenye viongozi wagonjwa,walevi wa madaraka,wenye kutupuuza

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
Heshima Mbele,
Jana nilikuwa naongea na mpwa wangu kuhusuiana na mipango yake ya shule hasa ya chuo kikuu anakosoma,katika maelezo yake alilaumu jinsi ya ufundishaji katika vyuo,mpwa wangu aliniambai kuwa hawapi elimu kwa vitendo na ndiyo inachangia wao kutokuwa na uwezo wa kujieleza na kujiamini.

Maelezo haya yalivuta hisia zangu sana,nikakumbuka mambo mengi sana ya zamani na pia tabia ya sasa ya watanzania ya kulalamika tu bila kuchukua hatua madhubuti za kukabiliana na matataizo yaliyopo hapa nchini

Mtakumbuka toka miaka ya tisini mpaka elfu mbili,wanachi wengi wa nchi hii imekuwa na watu wa kulalmika elimu yetu haiwezi kuendelea kwa kuwa elimu yetu haijali elimu kwa vitendo.tumeendelea kulia kulia sana na hili jambo bila ya sisi wenyewe kujaribu kutatua tatizo lenyewe kwa kuanzakubadilika.Tunajua tatizo ni nini ila tumebaki kulalamika tu!

Tabia hii imeka vichwani mwetu na imejengeka mpaka sasa,tumekuwa watu wa kuilaumu serikali tu,tumekuwa tukiwalaumuwatu flani kwa kutufikisha hapa.

Je tumefanya nini kuondokana na tatizo hili?uwezo tunao na sijui tunangoja nini?tumekuwa wa tu wa kulalamiak tu na baadaey tunarudisha watu wale wale na kibaya zaidi wasiojua kwa nini wao ni viongozi(Rejea chenge aliyesema kamuulizeni Rais kwa nini alinichagua)


  1. Tumelalamika kuhusiana na IPTL wakasikiliza na baadaye wakatupuuza
  2. Tumelalamika kuhusiana RDC wakatusikiliza na baadaye wakatupuuza
  3. Tumelalamika ujenzi wa BOT-Twin Towers ,wakatuikiliza ila wakatupuuza
  4. Tumelalamika kuhusu EPA,wakatusikiliza,wakaweka usanii alafu wakaamua kutupuuza
  5. Tumelaamaika kuhusu na Dowans,wakatusikiliza ila badaye watatupuuza
  6. Tumelalamika kuhusu Import Suuport,wakaamua kukaa kimya na kutupuuza
  7. Tumelalamika maisha magumu na wao wanaendelea kufuja pesa zetu kwa safari ila wanapuuza

Ndiyo tupo kwenye nchi ambayo viongozi wakishachukua madaraka wanatoa ahadi nyingi ila badaye wanatupuuza na kutudharau kwa kuwa watanzania ni mandondocha sasa hivi wamerudi mikoani huko kuwaomba kura,wameamua kuwa karibu na nyie kwa kuwa kampeni ni 2010.

Naomba sa kutoa wito kwa wanachi wote

1.Kwanza Tuanze upya mwaka 2010,tiusahau yote na tukubali sawa walituibia,kama anavyosema mwanakijiji siku zote tuanze uoya na tukubali kuna sehemu tulikosea,imetosha sasa na nina amani kabisa akili mnazo na uwezo mnao,kama mnahitaji maisha bora ni wakati huu sasa kuweka wabunge ambao wataleta maendeleo.

2.Kataa kabisa kupigia kampeni watu ambo pesa yao ni ile imetokana na kodi yako,usipokee Rushwa kwa kuuza haki yako,hata kama ni chaguo la Rais kataa kabisa mawazo yake na huu uwe mwanzo wa Tanzania ile uipendayo!

Enyi wanachi mlio wakimya,wapole,mlio na uwezo wakushika yale mnayoona ni madogo na kusahu makubwa nawaapieni Kama ukishindwa kuamua

1.Mtaendelea kupuuzwa na kuhudumia wagonjwa!

2.Mtaendela kuishi maisha ya kifukara na kimasikini milele

3.Mtandelea kupuuzwa!

4.Dhahabu na utajiri wote uliopo nchini utachukuliwa na wageni

Tuacheni kuilalamika,tuchukue hatua na kuhakikisha tunaanza upya 2010.

Nawatakieni maandalizi mema na naomba CCM ijetenge ili kufanikisha hili!
 
Last edited:
dah!!
hii imetulia, unajua tulio wengi tunalalamika huku tukisubiri mtu flan ndo alete mabadiliko,
kmbe mabadiliko na maendeleo yanaanzia kwako na si kusubiri mtu mwingine.
hapa mwisho mwadishi kasema ccm ijitenge ili kufanukisha hili, SIJAKUPATA KAKA! fafanua
 
Edson,

Tunahitaji chama chenye sura ya kitaifa,chama cha wazalendo wenye upeo mkubwa

Tunahitaji watu ambo watakuwa wawazi na siyo watu wahuni wa kupenda kutukuzwa

Nahisi bado katika upinzani hakuna watu wa kutosah kuwe akukamata hatamu hivyo wale ambao wana mlengo sahihi wanaweza toka CCM na kujiunga na sisi wanamapinduzi
 
Gembe

Muda mrefu sana nilikuwa sikuelewi....sasa naona umeogoka unaongea lugha tunayopenda kuisikia...pamoja tunaweza...good post well constructed...moyo wa uzalendo...bravo
 
Hii style ya Thailand vipi? yaani maandamano hadi to bring down serikali!! Je Watz wana hii courage?
 
kwa hilo kaka nimekuelewa vizuri,
tatizo la upinzani ni kwamba ndani ya vyama kuna walafi wa madaraka, wanapigana wao kwa wao, wanatukanana, wanalilia madaraka nk. hii inatoa mwanya kwa ccm ku take over. kuna kitu cha ziada kinapaswa kufanyika kwa watanzania wote,kila mtu atambue na ajitambue na adhamirie kuweka mabadiliko hasa kwa wabunge watakaowachagua
 
Naaamini tukisimama pamoja na kuungana wenyewe kwa pamoja tunaweza.Tunaweza kuweka viongozi wasio kuwa na tamaa na si walafi.
 
Naaamini tukisimama pamoja na kuungana wenyewe kwa pamoja tunaweza.Tunaweza kuweka viongozi wasio kuwa na tamaa na si walafi.
 
Hii iko constructive zaidi. Wengi ukiwakuta kijiweni ni wakali kama pilipili kuongelea uozo uliopo, lakini wakienda mtaa wa pili wakipewa kitu kidogo wataanza kupiga kampeni na kudai kuwa hakuna siasa safi kama za chama tawala, mifano ipo mingi, watu waliokuwa wanasema vizuri kama akina Lamwai baadae wameona heri kumtumikia kafiri. Hilo ndio tatizo letu, tunajali maslahi binafsi kuliko ukombozi wa moja kwa moja wa taifa hili. Kupenda madaraka, unafiki na usaliti ndio vinavyotuumiza. Tatizo limebaki sugu hasa kwa watu ambao kidogo wameelimika, hawapendi kutake risk hata kidogo wanapenda kuandamana na watawala ili wasipoteze mkate wao. Inashangaza CCM huwa haisumbui kichwa kupata kura Dar ambako ungedhani watu wengi wameelimika, lakini sivyo kwa kuwa wengi ni wabinafsi wanaishia kupewa kidogo tu na kuuza haki yao, ukiwataja wasomi ndio kabisa. Wengi hulalamika baada ya kura kupita. Haitoshi kulalamika, tunafanya nini kuuweka madarakani uongozi ambao ni responsible na accountable kwa wananchi? Mabadiliko yoyote yataanza na wewe!!
 
Heshima Mbele,
Jana nilikuwa naongea na mpwa wangu kuhusuiana na mipango yake ya shule hasa ya chuo kikuu anakosoma,katika maelezo yake alilaumu jinsi ya ufundishaji katika vyuo,mpwa wangu aliniambai kuwa hawapi elimu kwa vitendo na ndiyo inachangia wao kutokuwa na uwezo wa kujieleza na kujiamini.

Maelezo haya yalivuta hisia zangu sana,nikakumbuka mambo mengi sana ya zamani na pia tabia ya sasa ya watanzania ya kulalamika tu bila kuchukua hatua madhubuti za kukabiliana na matataizo yaliyopo hapa nchini

Mtakumbuka toka miaka ya tisini mpaka elfu mbili,wanachi wengi wa nchi hii imekuwa na watu wa kulalmika elimu yetu haiwezi kuendelea kwa kuwa elimu yetu haijali elimu kwa vitendo.tumeendelea kulia kulia sana na hili jambo bila ya sisi wenyewe kujaribu kutatua tatizo lenyewe kwa kuanzakubadilika.Tunajua tatizo ni nini ila tumebaki kulalamika tu!

Tabia hii imeka vichwani mwetu na imejengeka mpaka sasa,tumekuwa watu wa kuilaumu serikali tu,tumekuwa tukiwalaumuwatu flani kwa kutufikisha hapa.

Je tumefanya nini kuondokana na tatizo hili?uwezo tunao na sijui tunangoja nini?tumekuwa wa tu wa kulalamiak tu na baadaey tunarudisha watu wale wale na kibaya zaidi wasiojua kwa nini wao ni viongozi(Rejea chenge aliyesema kamuulizeni Rais kwa nini alinichagua)


  1. Tumelalamika kuhusiana na IPTL wakasikiliza na baadaye wakatupuuza
  2. Tumelalamika kuhusiana RDC wakatusikiliza na baadaye wakatupuuza
  3. Tumelalamika ujenzi wa BOT-Twin Towers ,wakatuikiliza ila wakatupuuza
  4. Tumelalamika kuhusu EPA,wakatusikiliza,wakaweka usanii alafu wakaamua kutupuuza
  5. Tumelaamaika kuhusu na Dowans,wakatusikiliza ila badaye watatupuuza
  6. Tumelalamika kuhusu Import Suuport,wakaamua kukaa kimya na kutupuuza
  7. Tumelalamika maisha magumu na wao wanaendelea kufuja pesa zetu kwa safari ila wanapuuza

Ndiyo tupo kwenye nchi ambayo viongozi wakishachukua madaraka wanatoa ahadi nyingi ila badaye wanatupuuza na kutudharau kwa kuwa watanzania ni mandondocha sasa hivi wamerudi mikoani huko kuwaomba kura,wameamua kuwa karibu na nyie kwa kuwa kampeni ni 2010.

Naomba sa kutoa wito kwa wanachi wote

1.Kwanza Tuanze upya mwaka 2010,tiusahau yote na tukubali sawa walituibia,kama anavyosema mwanakijiji siku zote tuanze uoya na tukubali kuna sehemu tulikosea,imetosha sasa na nina amani kabisa akili mnazo na uwezo mnao,kama mnahitaji maisha bora ni wakati huu sasa kuweka wabunge ambao wataleta maendeleo.

2.Kataa kabisa kupigia kampeni watu ambo pesa yao ni ile imetokana na kodi yako,usipokee Rushwa kwa kuuza haki yako,hata kama ni chaguo la Rais kataa kabisa mawazo yake na huu uwe mwanzo wa Tanzania ile uipendayo!

Enyi wanachi mlio wakimya,wapole,mlio na uwezo wakushika yale mnayoona ni madogo na kusahu makubwa nawaapieni Kama ukishindwa kuamua

1.Mtaendelea kupuuzwa na kuhudumia wagonjwa!

2.Mtaendela kuishi maisha ya kifukara na kimasikini milele

3.Mtandelea kupuuzwa!

4.Dhahabu na utajiri wote uliopo nchini utachukuliwa na wageni

Tuacheni kuilalamika,tuchukue hatua na kuhakikisha tunaanza upya 2010.

Nawatakieni maandalizi mema na naomba CCM ijetenge ili kufanikisha hili!

tili lili lilili tilili tilili X2!
 
Hii iko constructive zaidi.

Haitoshi kulalamika, tunafanya nini kuuweka madarakani uongozi ambao ni responsible na accountable kwa wananchi? Mabadiliko yoyote yataanza na wewe!!

Mkuu wa kupiga Filimbi,

JF siku zote imekwua ni jambi la kuamsha hisia na kuwa na topic nzito na huu ni mtiiriko kuelekea 2010.Tunahitaji mabadiliko na hatuhitaji kuchoka ili kuendelezea nchi yetu.

Mkuu FMES,Mkuu Mwawado na Kada Mpinzani mnahitajika kurudi sasa na kuanza kutoa za changamoto kama za cheche.Watu wamepoa sana hapa JF na tunahitajika kuwa mdomo wa wananchi wa kule tandahimba,uyole na nyarugusu

Tatuzo siyo kulalamika tu,tatizo pia lipo kwenye viongozi tulio nao hasa wale ambao wanapenda 'cheap Politics' bila ya kuwa na sera madhubuti.

Tunahitaji kutambua ni viongozi wa aina gania ambao tunawataka kwa hivi sasa,wawe a na sifa gani na hapo hapo tujue tutawapataje?kuwepo na program ndefu ya kupata wagombea ubunge 2010!

Je kwa kutumia vyama vyetu vya siasa au kutengeneza aina ya viongzoi tunawaotaka?wansasiasa ambao watakuwa tayari kupigania maslahi ya nchi yetu bila kuchoka na wenye sera za kimaendeleo!

viongozi ambao wanajua kuongoza mambo na kufuatilia kila jambo bila kurukia rukia masuala yasiyo ya msingi.

CHADEMA mlikuwa na Mpango mzuri sana wa kumobilize Vijana ..Umeishia wapi kwa sasa?

KWa kifupi tunahitaji viongozi wa kisasa zaidi


 
Hii style ya Thailand vipi? yaani maandamano hadi to bring down serikali!! Je Watz wana hii courage?

Hii idea naiunga mkono.

Actually, mie ningependekeza a Tanzanian style: wananchi wote wanagoma kwa kubaki majumbani au kukaa tu vijiweni mpaka serikali inacollapse.

Miserikali ya Kiafrika haithamini haki za binadamu. Tukiandamana mitaani itaagiza miaskari itumiminie mirisasi na kutupiga mibuti na mirungu na kuturushia mibomu ya machozi ovyo.

Physical courage with mental vitality.
 
Problem is KIDUMU, hapo kinapodumishwa sasa ....!


Problem sio KIDUMU, problem ni ujinga wetu. Tukiweza kujielimisha, kutambua maslahi yetu kama taifa na kukishikia kiboko KIDUMU (au serikali/chama chochote), tutaendelea mpaka tutajishangaza wenyewe na kila mtu!
 
Gembe heshima mbele mkuu, nimekusoma na kukuelewa. Ni muhimu kwasisi sote kwanza kuelewa CCM wana mbinu gani za kuwawezesha kutawala milelele kama wanavyosema wenyewe!! Silaha yao kubwa waliyonayo na ambayo wanaitegemea sana ni "KATIBA" ya nchi yetu kama ilivyo sasa. Katiba hii ni katiba inayokidhi malengo ya CCM na ndiyo maana hata siku moja CCM haitakubali katiba ibadilishwe ili iendane na mfumo wa kidemokrasia wa vyama vingi; na ndio maana CCM mpaka sasa inapinga kuwapo kwa wagombea "Independent" ingawaje mahakama zote za nchi zimeruhusu uwepo wao!! Nadhani hatua ya kwanza kama tunataka kujikomboa ni kuhakikisha kwamba hatushiriki katika uchaguzi wowote bila ya katiba kukidhi mazingira ya demokkrasia ya vyama vingi hata ikibidi kususia chaguzi zote!! Tukikubali kwenda kwenye chaguzi na katiba kama ilivyo sasa CCM watatuchinja kama kuku na vyama vya upinzani uchwara vitaambulia ruzuku na huo utakua mwisho wa mchezo, na mafisadi watazidi kupeta na wadanganyika tutakufa kibudu!!
 
said:

JF siku zote imekwua ni jambi la kuamsha hisia na kuwa na topic nzito na huu ni mtiiriko kuelekea 2010.Tunahitaji mabadiliko na hatuhitaji kuchoka ili kuendelezea nchi yetu.

Mkuu Gembe, kama ni kweli na wewe umeweza kuliona hili basi ni hatua nzuri na unakaribishwa kuungana na wazalendo kuendeleza libeneke - karibu. Hata hivyo ulichofanya ama unachojaribu kukifanya hakina tofauti na kile tumekuwa tukikihubiri siku zote - kutochoka katika kudai mabadiliko yatakayochochea maendeleo katika nchi yetu.

said:
Mkuu FMES,Mkuu Mwawado na Kada Mpinzani mnahitajika kurudi sasa na kuanza kutoa za changamoto kama za cheche.Watu wamepoa sana hapa JF na tunahitajika kuwa mdomo wa wananchi wa kule tandahimba,uyole na nyarugusu

Inawezekana unaamini kuwa humu ndani wapo watu ambao uwepo wao huleta changamoto zaidi - huo ni mtazamo wako na haki yako. Kwa upande wangu naheshimu mchango wa kuboresha utawala nchini kutoka kwa yeyote bila kutazama majina. Hii tabia ya kujenga matabaka ndiyo yameifikisha nchi hapa ilipo na kamwe tusiiruhusu humu JF.

said:
Tatuzo siyo kulalamika tu,tatizo pia lipo kwenye viongozi tulio nao hasa wale ambao wanapenda 'cheap Politics' bila ya kuwa na sera madhubuti.

Kulalamika ni tabia ya binadamu wakati wowote ule haki inapotolewa kwa kujali sura/wadhifa - usipolalamika ni kuwa unaruhusu hali hiyo iendelee. Sikuelewi unapotumia nano 'cheap politics' na kwa nani. Mtu ambaye amekaa madarakani miaka zaidi ya 30 bila kuleta maendelao, akimwita anayetaka kumwondoa madarakani mroho wa madaraka - hiyo naiita 'cheap politics'. Akitishia kuwa bila yeye amani itatoweka kama vile anayo hatimiliki, hiyo nayo naiita 'cheap politics'. Akibeza sera pinzani na yake ambayo imeshindwa kuboresha maisha ya mwananchi, hiyo pia nitaiita 'cheap politics'. Sasa labda ueleze kinaga ubaga una maana gani na 'cheap politics' na nani unamwongelea hapa.


said:
Tunahitaji kutambua ni viongozi wa aina gania ambao tunawataka kwa hivi sasa,wawe a na sifa gani na hapo hapo tujue tutawapataje?kuwepo na program ndefu ya kupata wagombea ubunge 2010!

Sifa ya viongozi tunaowataka tunazijua na namna ya kuwapata tunafahamu ila tunacholilia ni uhuru na haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Kwa kuwa tunao mfumo wa kidikteta wa chama inakuwa ni vigumu kupatikana utawala unaoheshimu usawa mbele ya sheria. Hivyo njia ziko mbili - kudai mabadiliko katika katiba kwa amani na watawala waone busara ya kuridhia hilo au wawe tayari kusubiri kinachoitwa 'mass action' - shuhudia Thailand !!

said:
Je kwa kutumia vyama vyetu vya siasa au kutengeneza aina ya viongzoi tunawaotaka?wansasiasa ambao watakuwa tayari kupigania maslahi ya nchi yetu bila kuchoka na wenye sera za kimaendeleo! viongozi ambao wanajua kuongoza mambo na kufuatilia kila jambo bila kurukia rukia masuala yasiyo ya msingi.

Wapo wanasiasa tena wengi tu walio tayari kupigania maslahi yetu bila kuchoka - bahati mbaya Mkuu Gembe wewe ni moja wa watu walioshindwa kabisa kuwaona na umeishia kuwabeza wote wanaojitokeza . Umekuwa moja wa watu wanaotetea sera nzuri za CCM ambazo ni wazi hazijaweza kutuletea matumaini yoyote kwa zaidi ya miaka 40 !! If it aint working, fix it and if it cant get fixed, get rid of it, period. Bahati mbaya umebakia kusubiri kumeguka kwa CCM kama njia ya kupata unachoamini upinzani wa kweli - kalaghabaho !!

said:
CHADEMA mlikuwa na Mpango mzuri sana wa kumobilize Vijana ..Umeishia wapi kwa sasa? KWa kifupi tunahitaji viongozi wa kisasa zaidi

Ulianza vizuri sana kwa kuiita hii nchi ya watu kulalamika lakini post yako nzima imejaa kulalamikia wengine tu. Hivi wewe uko upande gani - hebu soma uliyoyaandika:-

said:
Enyi wanachi mlio wakimya,wapole,mlio na uwezo wakushika yale mnayoona ni madogo na kusahu makubwa nawaapieni Kama ukishindwa kuamua

1.Mtaendelea kupuuzwa na kuhudumia wagonjwa!

2.Mtaendela kuishi maisha ya kifukara na kimasikini milele

3.Mtandelea kupuuzwa!

4.Dhahabu na utajiri wote uliopo nchini utachukuliwa na wageni

Tuacheni kuilalamika,tuchukue hatua na kuhakikisha tunaanza upya 2010.

Nawatakieni maandalizi mema na naomba CCM ijetenge ili kufanikisha hili!

Wewe hapa naona umejipanga kama mtazamaji tu - sasa una tofauti gani na hao wanaolalamika. Umesaidia na umeshiriki vipi katika juhudi za kumobilize vijana katika kutafuta uongozi wa kisasa.
 
Inawezekana unaamini kuwa humu ndani wapo watu ambao uwepo wao huleta changamoto zaidi - huo ni mtazamo wako na haki yako. Kwa upande wangu naheshimu mchango wa kuboresha utawala nchini kutoka kwa yeyote bila kutazama majina. Hii tabia ya kujenga matabaka ndiyo yameifikisha nchi hapa ilipo na kamwe tusiiruhusu humu JF.





Sifa ya viongozi tunaowataka tunazijua na namna ya kuwapata tunafahamu ila tunacholilia ni uhuru na haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Kwa kuwa tunao mfumo wa kidikteta wa chama inakuwa ni vigumu kupatikana utawala unaoheshimu usawa mbele ya sheria. Hivyo njia ziko mbili - kudai mabadiliko katika katiba kwa amani na watawala waone busara ya kuridhia hilo au wawe tayari kusubiri kinachoitwa 'mass action' - shuhudia Thailand !!.
Maenno mazito haya!Respect Mkuu

Wewe hapa naona umejipanga kama mtazamaji tu - sasa una tofauti gani na hao wanaolalamika. Umesaidia na umeshiriki vipi katika juhudi za kumobilize vijana katika kutafuta uongozi wa kisasa.

Mie nimebaki kuwa mshauri tu kwa sasa,ila kushiriki kwangu itakuwa ni kwa kutoa ushauri tu ,na siyo lazima kila mtu awe mstari wa mbele katika apigano ya kichini chini!

ndiyo maana kuna kina Mbowe,zitto ma wapo watu wa aina ya mimi na Mzee Mwanakijiji ila wote nia yetuni moja
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom