Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Nchi inakoelekea si salama-Askofu
Na Benjamin Masese
KIONGOZI wa kundi la waumini waliojitenga na Kanisa la Anglikana la Tanzania, Askofu Ainea Kusehna amesema kuwa nchi inapoelekea sasa si salama kutokana na
baadhi ya viongozi kuchaguliwa kwa rushwa huku wakinyosheana vidole.
Askofu Kusehna alisema hayo katika ibada maalumu iliyofanyika Mbezi Beach, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wote wa kanisa hilo la Anglikana la Kiinjilisti Tanzania (KAKT) kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.
Katika ibada hiyo Askofu Kusehna alisema matatizo manne yanayoikabili nchi na watu wake ikiwa ni pamoja na rushwa, tamaa ya fedha na mali, madaraka na ukubwa pia tamaa ya starehe.
Askofu Kusehna alisema makanisa yatasarambatika na taifa kuhangamia ikiwa watu wake hawatabadilika na kuacha uchu wa madaraka ya rushwa na kufuata haki inayoinua taifa lolote la demokrasia.
Alisema kuwa asilimia kubwa ya maaskofu na viongozi wa serikali wanachaguliwa kwa rushwa na kuwa yupo tayari kuwataja viongozi wa dini pale inapohitajika katika vikao vyao vya majadiliano.
"Mkisikia maaskofu wakitajwa, tambueni si wote ni maaskofu kutokana na matendo yao maovu ya rushwa, na ndio wa kwanza kuwanyoshea vidole wengine bila kujitambua kuwa wao wameoza.
"Sisi tunatakiwa kuwa nuru kwa jamii pia kuwa mfano wa chumvi inayoleta ladha katika chakula, hebu niwaulize leo, sisi ni chumvi katika jamii?" alihoji. .
Aliongeza kuwa kizazi hiki cha maaskofu ni cha usanii, na hakiwezi kutoa neno la Mungu linaloburudisha na kubadili mtazamo katika jamii, bali wanatoa somo linaloweza kuwalinda wao, huku wakiunga mkono kuwepo kwa ushoga na usagaji.
Akizungumzia usajili wa kanisa hilo alisema kuwa kumekuwepo na mikakati kabambe kutoka kanisa la Anglikana Tanzania ya kuchafua kundi hilo ili likose usajili, na kuwa tayari wamepata nyaraka zao zilizopelekwa Wizara ya Mambo ya Ndani zikidai kwamba kikundi hicho kinatumia vichochezi vya kikabila, jambo ambalo ni hatari linaweza kudhoofisha mtengamano na umoja wa makanisa na nchi nzima.
Askofu Kusehna alisema kuwa nyaraka hizo ziliandikwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Valentino Mokiwa kwenda kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha ambaye alimjibu kwa kumhakikishia kanisa hilo halitasajiliwa.
Aliongeza kuwa tuhuma zingine ni pamoja na kudaiwa kutumia nembo ya Anglikana, vitabu vyake vya ibada, nyimbo na liturgia, kinyume cha sheria, wakati likiwa halijasajiliwa.
Askofu Kusehna alihitimisha kwa kutoa tamko kwamba hakuna anayestahili kumnyoshea mwingine kidole iwe serikali, polisi, viongozi wa dini au wananchi kwa kuwa wote wana makosa, na pia wote wanatakiwa kujisafisha kuanzia kwenye chimbuko la matatizo hayo.
Na Benjamin Masese
KIONGOZI wa kundi la waumini waliojitenga na Kanisa la Anglikana la Tanzania, Askofu Ainea Kusehna amesema kuwa nchi inapoelekea sasa si salama kutokana na
baadhi ya viongozi kuchaguliwa kwa rushwa huku wakinyosheana vidole.
Askofu Kusehna alisema hayo katika ibada maalumu iliyofanyika Mbezi Beach, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wote wa kanisa hilo la Anglikana la Kiinjilisti Tanzania (KAKT) kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.
Katika ibada hiyo Askofu Kusehna alisema matatizo manne yanayoikabili nchi na watu wake ikiwa ni pamoja na rushwa, tamaa ya fedha na mali, madaraka na ukubwa pia tamaa ya starehe.
Askofu Kusehna alisema makanisa yatasarambatika na taifa kuhangamia ikiwa watu wake hawatabadilika na kuacha uchu wa madaraka ya rushwa na kufuata haki inayoinua taifa lolote la demokrasia.
Alisema kuwa asilimia kubwa ya maaskofu na viongozi wa serikali wanachaguliwa kwa rushwa na kuwa yupo tayari kuwataja viongozi wa dini pale inapohitajika katika vikao vyao vya majadiliano.
"Mkisikia maaskofu wakitajwa, tambueni si wote ni maaskofu kutokana na matendo yao maovu ya rushwa, na ndio wa kwanza kuwanyoshea vidole wengine bila kujitambua kuwa wao wameoza.
"Sisi tunatakiwa kuwa nuru kwa jamii pia kuwa mfano wa chumvi inayoleta ladha katika chakula, hebu niwaulize leo, sisi ni chumvi katika jamii?" alihoji. .
Aliongeza kuwa kizazi hiki cha maaskofu ni cha usanii, na hakiwezi kutoa neno la Mungu linaloburudisha na kubadili mtazamo katika jamii, bali wanatoa somo linaloweza kuwalinda wao, huku wakiunga mkono kuwepo kwa ushoga na usagaji.
Akizungumzia usajili wa kanisa hilo alisema kuwa kumekuwepo na mikakati kabambe kutoka kanisa la Anglikana Tanzania ya kuchafua kundi hilo ili likose usajili, na kuwa tayari wamepata nyaraka zao zilizopelekwa Wizara ya Mambo ya Ndani zikidai kwamba kikundi hicho kinatumia vichochezi vya kikabila, jambo ambalo ni hatari linaweza kudhoofisha mtengamano na umoja wa makanisa na nchi nzima.
Askofu Kusehna alisema kuwa nyaraka hizo ziliandikwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Valentino Mokiwa kwenda kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha ambaye alimjibu kwa kumhakikishia kanisa hilo halitasajiliwa.
Aliongeza kuwa tuhuma zingine ni pamoja na kudaiwa kutumia nembo ya Anglikana, vitabu vyake vya ibada, nyimbo na liturgia, kinyume cha sheria, wakati likiwa halijasajiliwa.
Askofu Kusehna alihitimisha kwa kutoa tamko kwamba hakuna anayestahili kumnyoshea mwingine kidole iwe serikali, polisi, viongozi wa dini au wananchi kwa kuwa wote wana makosa, na pia wote wanatakiwa kujisafisha kuanzia kwenye chimbuko la matatizo hayo.