Nchi imekosa mwelekeo

Chromium

JF-Expert Member
Apr 17, 2008
589
185
Nazungumza kwa masikitiko makubwa. Ninasononeka. Ninaandika nikilia. Navuta machozi nikitafakari pepo mchafu anawasumbua watawala wetu.

Hakuna asiyetambua kuwa nchi yetu inayumba. Nchi imekosa mwongozaji. Nchi imepoteza dira. Nchi inakwenda pasipofahamika. Nchi haieleweki inakopelekwa.

tuliowachagua, wanaiba kwa kasi mpya, wakikingiana kifua. Nchi inaliwa. Nchi inalika. Nchi inamalizwa. Nchi inafilisiwa na genge la walafi wachache wanaojidai kuwa hatuelewi wanavyoinajisi nchi yetu. Ninaumia. Ninasikitika. Ninaogopa. Mpka lini mambo haya? Mpaka lini? Kwa nini haya majitu yanajiamini hivi?

Hayo ndiyo ninayokusudia kushirikishana nani wana Jambo. Ninalo jambo la kusema. Nimeamua kutoka kichakani niseme niliyonayo. Kusema kutaniweka huru. Naomba msinielewe vibaya.

Nashindwa kuandika kwa machozi niliyonayo. Nitaendelea nikinyamaza.
 
Kweli kabisa nchi imekosa mwelekeo visheria visivyokuwepo vinajitokeza kila siku mfano hai hao wamachinga serikali haioni kuwa watu hao wanateseke kwa kuhangaishwa na site hapo wanajitafutia riziki kwa halali kabisa je,mnataka warudi katika fani zao walizokuwa nazo zamani kama wizi ungesema mateja wakamatwe kupunguza uporaji,unyang'anyaji wa wananchi kwa sababu hio si njia halali ya kujitafutia riziki aliyehusika na sheria hii anaombwa tafadhali kujirekebisha na hao city wake ninahasira nao.Usitumie cheo ulichokuwa nao kunyanyasa wenzio walio chini na unataka kuiga tamaduni/ubora wa majiji ya watu subiri kwanza mkimaliza huo ufisadi wenu ndi mtarekebisha kila sehemu kwani hujawajengea mahala pakuuzia hizo bidhaa zao sasa waende wapi kama si kusononeshana tu kimaisha.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom