Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Mbwa wamevamia Kata ya Old Korogwe Wilayani hapa na kula mahindi mabichi na kuzusha hofu kwa wananchi kwamba huenda wakasababisha jaa.Mjumbe wa serikali ya Mtaa wa Old Korogwe, Kasimu Lupatu wamefanya uharibifu mkubwa baada kula mashina 936 ya mahindi kwenye shamba la mtu mmoja aliemtaja kwa jina moja la Musa. Mwenyekiti alisema hii hali hatuielewi, mbwa kula mahindi tunaona ni kitu cha ajabu wakati yakiwa shambani, wanashambulia mahindi mabichi kwa kuyaangusha na kuyala na hata mimi nilifuatwa kuwashuhudia, alisema Lupatu mjumbe wa mtaa wa Old Korogwe. Pia alifanya utafiti kwenye kwenye kijiji cha Mabatini walikuta kinyesi cha mbwa hao kikiwa ni mahindi na magunzi hivyo kujiridhisha kwamba wanakula mazao hayo.SOURCE: MWANANCHI JUN 18 2011